Pages

Ads 468x60px

Friday, March 7, 2014

TUZUNGUMZE....


Wandugu  mwenzenu mkiona siwajibu maswali mnayoni inbox  mjue nayafikiria niyajibuje na wakati mwingine nakuwa na jibu lakini huwa wasiwasi wangu nimapokeo ya muhusika....... ngoja leo nifunguke kidogo labda ntaeleweka. nilichogundua watu tunachanganya haya mambo

Wanasema pesa ni sabuni ya roho kwangu naichukulia kama pesa ni matokeo.....  nikiwa na maana hii pesa inatafutwa na hakuna aliyefikia kiwango  akasema mimi pesa basi, na ndo maana kila kukicha watu tunazitafuta. Kuna hili neno limeandikwa PESA NA DHAHABU NI MALI YA BABA NA SISI TUWARITHI . Sijui mpendwa huwa unalichukuliaje hili??? nijuavyo mimi  ni haki yangu kama mrithi kuwa na mali lakini  kuna namna inipasayo kufanya ili kuendeleza, usishangae nikawa mrithi nikashindwa kuendeleza urithi niliopewa. Kama hunielewe kasome habari ya mwana mpotevu.......... na je unajua kiwango cha pesa kipo machoni pa muhusika??? yaani pesa haitoshelezi wapendwa. Endelea kunisoma utanielewa

Ninaposema ni matokeo ninamaanisha pesa haikupi amani ya ndoa, pesa haikupi mume, pesa haimalizi kiu. usitumie pesa, kama  kigezo cha wewe kupata Mume/mke wapendwa. kwani hujasikia mke/mume hutoka kwa Mungu?? tumia muda kuomba Mungu akupe Mume aliyekuandalia kuliko kutumia macho yako  ya damu na nyama  sana, na kumnyima Mungu nafasi asiingie kufanya nafasi yake. Kwa kusema hivi naomba niwe muwazi  sisemi kwamba mama wawili nilifunga na kuomba kuomba Mume niliyenae, kiukweli ndo yangu mimi ilikuja tuu..........ninachokumbuka siku ambayo nilijikuta nimeingia kwenye mawazo ya ndoa jioni nikampigia mjamaa simu alikuwa mbali kidogo nakumueleza jinsi hilo wazo lilivyonijia tukajikuta wote hatuoni sababu yakutolitendea haki wazo, nafikiri hapo hapo tukaanza taratibu haikuchuka miezi minne nikawa tayari ROSE WA SLAY ni NEEMA TU (kwa wale mnaongojea mnaniulizaga haya maswali nafikiri hapa mnanielewa kwa nini huwa sijibu mkiwa mnataka msaada wa dizaini hii kwa kweli sijapitia kipindi hicho, huwa muoga kushauri kitu ambacho sijakipitia na  ni muhimu sana kwa mtu) na  pamoja na hayo yote sisema ndoa yangu mimi 100% ipo poua, wandugu ndoa yangu ya kawaida sana tuu, kikubwa  ni roho zetu sio hiyo wanayosema ni sabuni ya roho,  kwetu ni matokeo. 

Nazidi kusisitiza ni kweli kuna vitu vya kuangalia kwa nafasi yako kama mwanadam, kwa mfano badala yakuangalia pesa hebu angalia uwezekano wa yeye na wewe mkiwa pamoja kutengeneza hiyo pesa.Badala yakutamani kuishi ulaya ukaamua kukimbilia mzungu au yeyote aliyetoka nje ya nchi akuoe ili akupe makaratasi hebu  mwamini Mungu kwa hiyo ndoto yako akupe yule yule Mume alikuyepangia kwa pamoja  mkakamilisha hiyo ndoto yenu..... nakuhakikishia inawezekana tena sio utaondoka Tanzania kwa sababu maisha yamekushinda bali kwa sababu ni moja ya ndoto zako (NINA USHUHUDA WA HILI) kama hunielewi nenda kamsome IBRAHIMU alivyoambiwa aende nchi ya ahadi( wandugu MUNGU wetu haongopi akisema Ndio hakuna atakaye pangua)........

Najitahidi kukutoa kwenye neno Pesa kama sabuni ya roho. Kwa macho yangu nimeshudia ndoa zakutaka makaratasi  na wameyapata,ulaya ameiona, mwisho wa siku bado hana amani  nakuona makaratasi na pesa sio ndoa.( wahusika please msinielewe vibaya lakini naona ni nafasi nzuri yakutumia mifano yenu ili tuelemishe wale waliokusudiwa) juzi kati kuna kijana alikuja kuniomba kazi  ananiambia lengo kubwa kwa sababu anataka kulipa fine alikamatwa anaendesha amelewa otherwise yu ko poua kukaa nyumbani ale hela ya serikali, mwingine anakwambia anataka kwenda holiday ndo maana anatafuta kazi, sasa unajiuliza kijana kama huyu anaenda nyumbani(Tanzania) wale wanaolilia makaratasi wakayapata kupitia huyu wakaja huku halafu inakuwaje??? si bora yule binti akabaki nyumbani anauza nyanya. Wapendwa inauma sana sisi tuliopo huku tunaelewa  na ukweli hatuwapi tunawadanganya tuu Mitandaoni.

Niliposema kiwango cha pesa kipo kwa muhusika nilimaanisha hivi, Pesa haitoshelezi hivyo ukifanya kama ndo faraja yako kuliko chochote tegemea kuwa mtu wakukosa amani kila siku nielewe kwa kajimfano haka
 nakumbuka miaka minne iliyopita ( kama mjuavyo starehe yetu kubwa nikujificha kama familia) kujificha  ilikuwa inaweza kutugharimu  sana labda $1000 hiyo siku tatu mpaka nne ,chumba $100 per night inayobaki mlo, mpaka shopping  na bado tulikuwa na amani na tulikuwa  tumerudi tumerefresh wenyewe kutoka mafichoni, namshukuru Mungu sasa hivi tunaweza kwenda mpaka $ 700 per night bado hujala, na shopping hujafanya  lakini kwa sababu pesa kwetu ni matokeo hatuoni shida siku nyingine tukarudi kwa ile hotel ya miaka iliyopita bado amani itabaki pale pale isipokuwa tumecheza na matokeo ya pesa.lakini ukiwa hapo kwenye level hiyo nakuamini kama waaminivyo wengine itatufanya tuuishi kwa kukariri majengo na kukosa amani ya kile tunachokipenda (kujificha)... utakubaliana na mimi kwa nini naamini pesa nimatokeo.......na  hapa nilipo huwa najipiga picha siku moja nimelala kwa $2000per night na familia yangu, nimekusikia tuu in two years Bwana atafanya njia ( kwi! kwi! kwi!hii sasa naleta misifa eti?? mnisamehe) wandugu kikubwa nataka watu tuelewe pesa haina kiwango haitoshi hivyo haileti amani ifanye kama matokeo iwepo au isiwepo bora mradi mahitaji muhimu yanapatikana.

KHAA NIMECHOKA KUANDIKA NINAMIFANO MINGIIII

Angalizo
Sijasema makaratasi hayatakiwi ntakuwa mnafiki mbona mimi ninayo? sijasema usiolewe kwenye mgodi unaotembea ntakuwa nina wivu kwa sababu mimi naosha magari, kikubwa hivyo ndivyo ilivyotakiwa uwe?? unaishi kwa ndoto yako au unatembelea ndoto ya mwenzio yako iko pending?? au tumekukaririsha mitandaoni na mashauzi yetu tukasahau kukusaidia ni nini likupasalo kufanya na wapi tulikosea  ili na wewe usiingie.Mwisho wasiku wewe ndo ujikague maamuzi unayotaka kufanya ni sahihi au kwa sababu ya kile unachokiona kwa macho ya damu na nyama.

Mbarikiwe

1 comments:

  1. huwa unanitia moyo sana mama wawili, kila nikihitaji kupata courage ninaposhindwa kufikiria mbele zaidi kutafakari vitu kiroho huwa naingia humu , ntatafuta hata post ya zamani hata kama nilishasoma nitairudia. ili nisonge mbele, uzidi kubarikiwa. mkifanya maombi katika lile group lenu msinisahau kuniombea na mimi.

    ReplyDelete