Pages

Ads 468x60px

Friday, April 8, 2016

HAPPY ANNIVERSARY TO US

Haya basi muendelezo wa post iliyopita........ na kesho yake ndo ikawa ile siku iliyonisukuma ndani ya moyo kufanya nilivyofanya............

Wazee ndo tushapiga nane aisee.... Duu km jana yaani hii miaka inavyokimbia sasa....SIFA ZIMRUDIE YEYE ALIYETUWEZESHA yaani hapa ni mgomo tuu mpaka kifo not otherwise hata shetani habari anayo.............. 

Basi bwana hatukuwa na something special zaidi ya special prayer before my man kwenda kututafutia hela ya kula hahahaa mkewe nikaishia kuangalia picha zetu za kumbukumbu for sure zilinipa feelings tofauti tofauti aisee.... nililia nilicheka,nilishangaa,nikawaza yaani basi tuu


 kikubwa nilichokiwaza ni jinsi gani Mungu aliruhusu hili........... jamani hii harusi nilipewa mda wa wiki kuiandaa ninavyosema kuiandaa i mean niliandaa mwenyewe..........
in short taratibu za wazazi zote zilikuwa zimekamilika  hiyo wiki tulikuwa  tumeshajipangia wenyewe harusi itafanyika ndani ya miezi sita ijayo( mtajiju km ilikuwa kubariki ama ndoa ila ndo hivyo, Bwana alitusamehe  nakutufanya upya ha!ha!ha!)..... tukiwa sasa tunaanza kutoa taarifa mara Baba watoto akapata hiyo sponser yakuja huku iliyompa km siku 10 awe ameshakuja huku........(mipango mingine inakujaga na baraka zake aisee)

Aisee mchumba wakati huo(ha!ha!ha! hivi mchumba ni yule aliyefanya taratibu zote akisubiri harusi bila kukugusa ama yule...........Ahsante kwa ajili ya msalaba maana duu sijui nani angepona aisee nawaza tuu)
 Akiwa anaenda kupanda ndege kwenda kuresign kazi yake ameniacha mimi sijui ntaanzaje ninachokumbuka kauli yake hakikisha tumefunga ndoa kabla sijaondoka ha!ha!ha!ha!


aisee jinsi Mungu alivyofanya nimetafakari sana kumbuka ndoa inatakiwa itangazwe miezi mitatu kabla,kuupata ukumbi aisee ulikuwa maarufu sana enzi hizo uko posta, ulikuwa wawakubwa enzi hizo nimeusahau jina ndaini ulikuwaga gold.......,kumpata mc ambaye hakunidissapoint,band,music, mtu wa vyakula na cake kuwaleta ndugu kutoka mikoani, nakumbuka jinsi ilivyokuwa ngumu kuwashawishi wazee,wajomba kwamba hii kitu inaenda kufanyika ndani ya siku kadhaa not a week anymore maana, sikutaka kusema chochote kabla kibali hakijatoka serikali kumruhusu mchungaji kunifungisha ndoa.........kibali kilitoka jumatano harusi jumapili ha!ha!ha!,kuwafanyia shopping i dont remember anyone helping me with this.... ninachokumbuka kuwafuata walionisimamia kwenda kumtafuta fundi juma atutengenezee gauni ndani ya siku tatu maana nilikuwa mwembamba magauni dukani hayanitoshi ha!ha!ha! fundi juma aliomba poo aiseee wakati huo huo nikamwambia Mume wake akatafute suti zao ha!ha!ha! (sikumbuki km kulikuwa na muda wakutafuta slim fit ha!ha!ha!)Baba watoto anarudi 2night before almost kila kitu kiko mezani naona akaona anipongeze mke wake na hilo gari  na kuniweka Kilimanjaro siku hizi mnaita Kempist ha!ha!ha! halikuwa kwenye akili yangu kabisa..... alinisuprise aliondokea hotelini kwenda kupanda ndege hilo balaa lakujibu maswali yaliyotokea kwa wazee aliniachia mie ha!ha!ha!  na kakitchen part nilifanyiwa baadae mikoani hahaha! no send off you know ha!ha!ha! ka account sasa tulikokuwa tunajifichia vi hela vyetu kalikuwa keupeee  nani akuchangie ndani ya wiki?? kuna wale wakaribu waliojua kwakweli walijitahidi walivyoweza na huwezi kuwalaamu nakumbuka baada ya ndoa tulienda hotelini kupumzika kabla mda wa ukumbini na kadi zetu unapiga simu halo fulani , ndugu yangu nisamehe bwa mwenzio ndo nishafunga ndoa naomba uje hapa uchukue kadi ya ukumbini ha!ha!ha!
Mawazo jinsi yakuwarudisha watu mikoani vepeeeee ha!ha!ha! nani hatakuelewa maana umefanya fujo ya ndoa ha!ha!ha!duu nimekumbuka mengi mnooo aisee

Happy anniversary to us.



Mwisho wa siku  kila mtu alikuwa suprised yaani hata mimi mwenyewe mpaka leo ukiniuliza how i did it km sio Mungu basi mi jeuri wa shukrani......


 story of our wedding!!!


ila mimi Bwana nikirembwa aisee narembeka haswaaaaaa ha!ha!ha! km nawana wakina niniii huku walivyovuta mdomo ha!ha!ha! jamani nawapenda lakini


Bwana wee shetani hawezi kulala kihivi yaani ha!ha!ha! hata km anaumwa atajikongoja tuu ajaribu ha!ha!ha!ha! eti nimeaambiwa siku hizi wanaume hawatupigi hiyo forehead eti tunajaza sana ma make up by the time amemaliza mdomo wake unakuwa km wale coca cola addict ha!ha!ha!

 enzi hizo za photo point vepe ha!ha!ha!


nilikuwa mwembamba ila nahisi kilo zilipungua zaidi fundi Juma ilibidi anipime kila asubuhi kumake sure

kwa kweli kamati yangu haikuniangusha nilivyokuwa nawapa kazi niliwaambia sina kamati kwa hiyo mpambani we ndo mwanakamati,keki,mc,................... ha!ha!ha! they did their best aisee  kwa enzi hizo lakini,sikuwa nawakumlaumu hata mmoja hakuna aliyeamini km maandalizi yalikuwa ya siku chache.


 haya basi baada yakujikumbusha namapicha nikaona nimfanyie Baba watoto kitu cha tofauti ambacho huwa sikifanya.....

kiujumla humu ndani mwangu huwezi ukanikuta nafanya kazi za nje km garden,kusafisha pool, sijui kuosha magari tunayotumia wenyewe sio biashara, so nikaona ngoja nitoe moja ya toy yake nimuoshee.......... kama unavyojua hichi kitu kinaendeshwa kwenye vumbi,mchanga au tope.......  ilikuwa inamatope ya hatari mwanamke nikaing'arisha just to say Ahsante Baba watoto kwanikubali km nilivyo, nakunivumilia maada duu!!! mi mkewe majanga sometimes ha!ha!ha!

nafikiri nilimpata maana nikitu hadimu kutoka kwa mkewe ha!ha!ha! any way ataenda kuichezea tena kwenye matope ilikuwa inahitaji a good wash before..........

 nimeloga kihivyo yaani. wanasema ukipenda kitu kwa moyo ideas huwa zinakuja and it means a lot to a person.

 nawapenda

5 comments:

  1. This is too emotional...Story yako na mimi imenipa kila aina ya feelings. Nimehuzunika na Kufurahi. But at the end Our God won.
    Hakika yeye ni Simba wa Yuda atupae kushinda na zaidi ya ushindi.
    Baraka za ndoa zisiondoke nyumbani kwako kwa jina la YESU. Mkalie pamoja, mnie pamoja na kufurahi pamoja. Amen

    ReplyDelete
  2. Mungu azidi kuwalinda katika ndoa yenu

    ReplyDelete
  3. Kila la kheri upendo na uendelee kutawala baina yenu

    ReplyDelete
  4. Mungu azidi kukubaliki, na kuwalinda katika ndoa yenu, nimeipenda story yako, but mwisho wa yote umepata ndoa njema.

    ReplyDelete
  5. Nakupenda sana wewe dada MUNGU awalinde

    ReplyDelete