Pages

Ads 468x60px

Tuesday, April 29, 2014

WAJAMENI ETI HII NINI???????

Au mimi ndo sielewi??? Hivi ndivyo tunavyopeleka wanetu wakajifunze??? aiseee sitaki kuamini huyu ni Mwalimu ninayemlipa anifundishie Mwanangu nakumwamini nikijua mwanangu yuko kwenye mikono salama...................I dont care its a public school or Private aiseeee nakulipa kwa kulipa kodi.Nimeumia sana aiseee ... yaani nimekumbuka kipindi fulani nilivyokuwa nawaacha wanangu kwa watu nilikuwa nawaamini  mi naenda kwenye mabin ,kusafisha vyoo na kulea wazee nilivyokuwa napata tabu kumuomba Mungu anisaidie nitoke kwenye hio biashara yakuwacha wanangu kwa watu na zaidi nilikuwa na nitizamia umri wa kwenda shule ufike maana huko ndo ntakuwa naamani zaidi. Kwa mpango huu mbona kama mwalimu ndo huyu!!!!!! NEEMA YA MUNGU ITUTETEE KWA KWELI......... maana duniani hakuna kimbilio ...........ninavyomwamini Mwalimu  mbona hapa nimeishiwa sasa.please tell me this is not a teacher anayewachezesha.Huyu binti hata miaka kumi amefika kweli???? mmmhhhh!!!Naamini huyu mtoto labda amejifunza kwenye mazingira anayoishi lakini sikutegemea kumuona mwalimu akifurahia hili.Aiseee kama ni kawida basi mimi mwenzenu wazamani sana aiseee yaani hapa huyu mwalimu angenieleza hiyo hadhi ya kuitwa mwalimu ilikuwaje.

Monday, April 28, 2014

SIRI...........

Nimekaa nimewaza sana leo   kwa vile jinsi neno HURUMA lilivyokuwa mzigo kwetu wanadam............... Nimejikuta nimewaza kipindi fulani nilipokuwa napitia jambo fulani neno huruma lilivyoongeza huzuni, idadi ya maadui na hata kupoteza muelekeo na hata pale nilipotakiwa kusema na Mungu wangu kwa habari ya lile ninalopitia. Ashukuriwe huyu roho mtakatifu anayejua kutuombea ipasavyo na lile jaribu likapata mlango. Kuna wakati tunaweza kujikuta tunaomba na kukemea kumbe tunapiga makelele mbele za Mungu, na kuna wakati tunafunga kumbe tumeshinda njaa................

Ninaposema hili neno lilinipa huzuni, nina maana hii, Akili yangu yote ilitegemea yoyote aliyesikia au kujua lile ninalopitia nilitarajia kumuona na huzuni kwa ajili yakunihurumia, nilishindwa kuelewa inakuwaje mimi na huzuni na kuna mtu haoni, na wala halipi uzito jambo langu. kuna mengi nilikuwa nawaza hapa mwisho wa siku  nilijitengenezea maadui mimi mwenyewe.........sikuishia hapo nilijikuta nimewabeba kwenye maombi  na asilimia kubwa ya yale maombi nilishughulikia hao maadui ambao leo naamini  hawakuwa adui kama nilivyofikiria hivyo nilijikuta napiga makelele mbele za Mungu(nilijikuta maombi yangu yanataja taja tuu majina huku Mungu akisema huyo adui gani unaye unayemtaja taja maana hata kwenye list simuoni kwa maana nyingine hana hadi yakuitwa adui wa mtoto wa mfalme kwi! kwi! kwi! nimewaza tuuuuuu..........

Ninachotaka kusema wapendwa ni hichi, Unatakiwa kulijua jaribu lako, Tambua kama linahitaji kumshirikisha mtu(rafiki,ndugu) au unatakiwa kulishughulikia wewe mwenyewe, na kama kuna mtu anatakiwa kujua unatakiwa kuwa na hekima ya hali ya juu  kujua ni mtu gani unapaswa kumshirikisha.

Nikiwa katika hali hii yakulitambua hili kama wote mjuavyo wiki mbili zilizopita kuna jambo ambalo nililipitia.Namshukuru Mungu lilinikuta wakati huu(kila jambo huja kwa wakati sahihi) maana lingenikuta wakati ule niliyo elezea hapo juu sijui leo ningekuwa wapi?????sijui ningelipokeaje????? yaani sijui kwa kweli!!!!! Hivi unaweza ukawa unapitia jambo ambalo akili haiwazi tena(imefika mwisho) badala yake hilo jambo halichukui nafasi kubwa ya Muda wako na wala akili yako kuwaza itakuwaje na imekuwaje????? kikubwa zaidi una amani na bila wasi wasi huku ukitarajia  USHINDI MKUBWA????( kuna mtu hatanielewa hapa  Mungu akupe masikio ya rohoni uelewe kama wewe umekusudiwa kuelewa hili)

 Nimejikuta nimewachambua watu wawili kwa picha tofauti, nikajifunza kitu, unapomshirikisha mtu jambo kwa mfano unapokuwa uko kwenye level ya kuchezea sh.1000  gafla ukapoteza sh.200 ukamfata mtu ambaye unategemea akuhurumie, asimame na wewe katika hilo , lakini umesahau kwamba huyu mtu anchezea sh.50 ameishi maisha yakukutamani si kwa ubaya  japo na yeye siku moja hata afike kwenye sh.500(kajifungia na hapo ndipo anapoamini mwisho wa mafanikio).
Kiukweli huyu mtu lazima kuwe kuna neema fulani ndani yake otherwise mapokeo ya mjaribu wako  yatakuwa na maelezo mengi bila majibu na mwishowe kutengeneza maadui. 
Atakwambia jamani hata hivyo mshukuru Mungu Bwana bado upo pazuri, una hichi, na hichi, na hichi yaani atakupa na mbinu zakutaka uridhike na kukubari amesahau lile neno nitakupandisha utukufu mmoja kwenda mwingine maana hakuna kushuka zaidi kuongezeka..............Usimlaumu huyu tena samehe kwa maana wewe ndo umemletea mjaribu, watu kama hawa wanatakiwa kushuhudiwa wajue uweza wa Mungu ni mkubwa kuliko  wanavyodhani, usimfanye  akaona hata hiyo ndoto yake haiwezekani, badala yake shughulikia hilo jaribu uje umshuhudie namna lilivyokuwa na namna ulivyodeal nalo. badala yakumchukia  nakumfanya kuwa adui.na ikiwezekana badala ya kumtaka yeye asimame kwa ajili ya huo mjaribu wako hebu simama nae kwenye huo mjaribu wake huku ukimsihi Mungu aliyekuwezesha wewe kufika hapo ulipo amuwezeshe na yeye tena zaidi nakuhakikishia utaona wepesi wa mjaribu wako muda unaokuja kustuka tayari umeshapata majibu yako........

Picha ya pili ni ya huyu mtu ambaye yeye ni zaidi yako, labda tuseme  anachezea sh.5000  na zaidi,huyu yeye anaamini kuongezeka na anaamini katika maongezeko kuna risks lazima ziwepo.  Ni kawaida sana  kwake kupoteza kabisa nusu ya kile alichonacho huku akitarajia kupata zaidi ya alichonacho sasa. wakati wewe umekazana kukumbatia kile ulichonacho kwa garama zozote kwa kudhani ukiruhusu kiondoke kidogo umekwisha!!! kumbe sivyo ni moja tuu ya challenge yakukupeleka zaidi. Huyu mtu ukimwambia hilo unalopitia naye lazima awe na neema fulani otherwise hutaona hata punje  ya huruma zaidi ya kukuonyesha ni kawaida. Mpendwa kama huelewi utamuweka kwenye list ya maadui nakuona kwamba huyu mtu hataki ufike alipo, anataka yeye awe juu kila siku ila usimfikie.........................

 Tambua jaribu lako, tafakari ni namna gani ikupasayo kufanya

Angalizo

 kuna mtu unaweza ukamwambia bila kujari yeye yupo kwenye nafasi gani na bado akasimama na wewe ndio maana nikasema kuna neema fulani lazima iwepo.......... Na pia kuna watu hiyo ni karama zao kusimama kwa ajili ya mtu, mfano mwanamaombi au mtumishi lakini sio kila aliye kwenye maombi ni mwanamaombi.

Na pia sijasema Muda wa kutumia mamlaka ukifika usivunje,haribu ,na kusambaratisha  maana tumepewa mamlaka.......... na sijasema tusiombe yeye autafutaye uso wa Bwana kwa bidii atamuona  IMEANDIKWA

shiiiiiiiiiiiiiiiiiiii!!!!!! nimesema siri usimwambie mtu.( mawazo yangu)

Thursday, April 24, 2014

Wednesday, April 23, 2014

MAMA WAWILI...............


 Siku nyingine, Wakati mwingine, tunazidi kukomaa tuu mpaka kieleweke  si eti wadau wa mimi????
 kama kawa moto wetu INAWEZEKANA!!!! 
  Halafu mwenzenu kuna wakati huwa nanyanyaswa  na wapiga picha  nyie acheni tuu.......... hizi picha mpiga picha alikuwa hajabarikiwa kabisa kunipiga.......... nimemuombaje sasa na kumbembeleza????? mpaka  na mapozi yalikuwa hayakubali. 




 nani kaona pengo na majembe ya Mama wawili??? ni SHIDA!!!


Monday, April 21, 2014

WATOTO WA DOT COM............

 Enzi zetu bwana,tulikuwa tukiona Baba na Mama wamekaa pamoja tulikuwa tunakimbilia vyumbani.........ila siku hizi  mmmmh!!ni full kutuvuruga  kwi! kwi! kwi!........ Tumetoka tulipotoka sie wawili moja kwa moja tukajikalisha hapo simnajua tena Baba na Mama  mipango huwa haiishi??? sikumbuki hizi dotcom  zilikuwa zinafanya nini ila nilikuwa nasikia makelele tukijua wanafanya yao........... ka muda kalienda kidogo, Mara Mum and Dad look!! kwanchu!!hee! camera woman kazini  katuvuruga, sasa sijui ndo kutafuta attention, au aliona Mama na Baba too much mipango, au aliamua kunifurahisha mpenda picha mwenzake  hata sielewi!!!!!!

ya suprise hiyo
 mpenda picha nikakumbushwa sasa  nikaanza toa maelekezo. ok take us from this angle.......... oh no!! its too dark
 Dad please  come here!!  Bwana eeh!! umeanza jua linanichoma machoni(in Dad's voice)
haya basi usiangalie jua niangalie mimi.................ha! ha! ha! ha!

Ahsante Mwanangu Careen nimepata chakushare na wadau wangu........

 na hadithi yangu imeishia hapa hapa.

Nawapenda

Sunday, April 20, 2014

TOFAUTI..................

Ngoja niwambie tofauti tuliyonayo ..................
Mungu wetu ni Mungu aliye hai,yaani ameshinda mauti  kwa maana nyingine alikufa na kufufuka na hii ndo maana kamili ya PASAKA!!!! Just incase huelewi maana!!!! au unasherekea kwa sababu watu wamesema usherekee.........

Tunapopita kipindi cha kujaribiwa imani,tunaujasiri maana tunaamini lipo tumaini............ Haijalishi limetukuta tukiwa tupo kwenye mstari ( kamsome Ayubu) au tumechepuka ( Mungu huadhibu na pia huturudia)(kamsome Daudi,wana waisraeli,...........) kikubwa ni lile TUMAINI . Hatuna sababu yakumplease mwanadam aliyeumbwa na huyu Mungu,wala miungu mfu  isiyokuwa na shukruni............. Acha kulaumu,acha kubebesha mizigo watu, wamekufanyia hivi na vile haihusu ndugu, wametumika kwani hujasoma Mungu kuna wakati alimpa Sauli moyo wa jiwe???? kila kitu kilichoruhusiwa kina sababu. acha kuchunguza chunguza Mambo ya Mungu hayachunguziki utapoteza Muda kama hunielewi Jiulize iliwezekanaje BIKIRA kawa na Mtoto, iliwezekanaje fipo ilipiga Bahari ikatawanyika, iliwezekana Daniel kamshinda Simba..... Utakuwa chizi mbona kama utatafuta hayo majibu. IMANI, IMANI, IMANI. kuza kiwango chako cha imani na JE KUNA NENO GANI GUMU ASILO LIWEZA???? YEYE ALIYESEMA ATAKUBARIKI, YUKO UPANDE WAKO,HATAKUACHA WALA KUKUPUNGUKIA.

Naona kama hunielewi?????
 nasisistiza,
 Amesema kaa mkono wangu wakuume hata niwawekapo adui chini ya miguu yako!!!!

acha kujisumbukia rafiki,yeye aliyeushinda ulimwengu atakushindia na hilo,mbona unakata tamaa,kiwango chako cha imani ki kwapi??mbona  unataka kufanana na asiyekuwa na tumaini??? unajua nini???? wewe ni full package ishi maisha yanayomfanya Mungu akajivunia ana mtoto  yuko Dunia.... no matter what she/he is still mine.  Nasema hivi MUNGU hawezi akakuacha ukaaibika  wewe ndo utakayeruhusu kuaiibika, yaani jaribu unalopitia sasa halibadilishi NENO LA MUNGU ila NENO LA MUNGU hubadilisha  jaribu unalolipitia. KULA NENO SHIBA NENO TAFAKARI NENO.

HAPPY EASTER


yote yalikwisha pale msalabani..........no kujisumbukia aiseee
Mke wa mwenyewe huyo
Mama wawili
nawapenda

Thursday, April 17, 2014

GEMMA-HOPE JOY DEDICATION'S LUNCH

 Last sunday  We were honoured to host Gemma-Hope Joy Dedication Lunch. To be honest with you,we are not taking this for granted, it means a lot to me and my family. Opening the door of our house and having that much  respond!!!!!!!!!!.................IT IS A BLESSING. 

Thank you Lisa and Ben  for trusting us........It was beautiful to meet your Mum,Dad and Sisters from Perth.Tell you what girl??? YOU ARE BLESSED!!!!!! Now i know where the beauty coming from............. 


Ben,Lisa & Gemma-Hope Joy
The venue...

yummmmmmm

Thank you all for coming.........

Tuesday, April 15, 2014

MAMA WAWILI

 Nyie niwaambieni kitu??? Ukiona akili yako imefika mwisho, hasa kwa habari ya mambo ya mwili, Ujue huo ni wakati wa kuyatafuta zaidi ya rohoni bila manung'uniko, Kiwango chako chakuutafuta uso wa Bwana kiongezeke  zaidi ruhusu utendaji wa Bwana. Maombi yako yawe yakubariki zaidi bila kulaani.Kama hunielewi soma  (LUKA 5:33-39). Tambua wakati.........Wakati kama huu jaribu kutoruhusu chozi likachukua nafasi kubwa zaidi...... jua kupambana. Jaribu kusoma na kusimamia  maandiko yanayofanania na unalopitia,zaidi chukua ule ujasiri na  kujivika ushindi wa watumishi waliopitia hilo............... HAKUNA JARIBU LISILO NA MLANGO
Niko kibusara zaidi ndo maana nimekaa.........
kuna mtu angenuna ujue nisingesimama???? haya basi

Nawapenda 



Monday, April 14, 2014

DINNER OUT.............


roho za mimi
 about to go........

 mboni ya jicho langu.......
we are here..... Thank you Mr & Mrs Barrick Mjema We are blessed to have you
hapo chacha chabies......

Uncle wa nani na nani huyu????  wacha wadeke  bwana mjomba......


 us


girls 
mapozi mengine mmmh!!!
 jamani hawa wawili wamepishana siku moja kuzaliwa sasa huwa inanichanginyi kidogo jinsi yakuiweka lakini tunamshukuru Mungu vyovyote itakavyokuwa kila mmoja wao anaenjoy.

THE END

Friday, April 11, 2014

AMEZALIWA!!!!!

Mwanaume,Baba,Rafiki amezaliwa!!!!!!!Nitakuwa nimekosa utu kama sitamshukuru mnooo Mama aliyekubari na kutumika miezi tisa kukumleta huyu kiumbe na hata leo ninasema ni zawadi ya upendeleo kwenye maisha yangu...................AHSANTE SANA MAMA MKWE WANGU Mungu azidi kukutetea ili uzidi kushuhudia na kujivunia  kwa kile ulichokubari kutumika............. HE IS A REAL MAN..... HE MIGHT NOT BE PERFECT TO EVERYONE OUT THERE  FOLKS,HE IS PERFECT FOR ME AND HE IS MINE!!!!!!!! Upendo,kujari,uchapakazi,hekima, uwajibikaji,mwanaume anayejitambuana  kujijua yeye ni nani na kujisimamia, Mwanaume anayeweza kudondosha chozi la kiume, kulifuta na kujianda jinsi yakukabiliana  na jambo,Mwanaume anayejua kutumia mamlaka aliyopewa na kuamini inawezekana ZAIDI YA YOTE NI MWANAUME MWENYE HOFU YA MUNGU........
HAPPY BIRTHDAY MY HUSBAND!!!!!!
Hardwork  
A man of future
A husband
BFF FOR LIFE

Dad wa nani na nani huyu.........

A father...........

UNAJUA NINI??????


ITS HER BIRTHDAY........................... 4years today wapendwa. niseme nini mimi kwa habari ya uzao wa viuno vyangu?????? 

them 4 different smile means  a lot to me!!!! yaani naijua kila mona wapo inamaanisha nini anapoitoa.My Christabell,Christabell wangu.Mungu akazidi kukutetea ukakue na kuongezeka.Si mimi ,si Baba yako wala Dada yako .Bali ni Mungu akafanyike kuwa kimbilio lako. Tunakupenda sana lakini tunatumika tuu................................
Ahsante MUNGU.

Thursday, April 10, 2014

WAKATI WA MAPITO............


Kumekucha wapendwa wangu, Napita mwenzenu leo hii nimepokeaje habari mbaya??????? ( si huwa nawambia na habari nzuri eeh??? hii ya leo kama bado naota vile ni mbayaaaaaaaaa kibinadamu lakini  naamini kuna mlango waakutokea) ni habari ambayo ukiweka  mezani Mtu lazima uchanganyikiwe aiseee na hata nikiwaambia  halafu nisiwape upande mwingine wa karatasi  Mnaonipenda mtaliaje sasa, mtanihurumiaje sasa  na shetani atafurahiaje sasa?????  of course nahitaji maombi yenu wandugu. Nahitaji mtu wakupiga magoti na mimi. nahitaji ule uweza upitao akili za binadamu wote.  nisingependa kuhurumiwa juu ya hili maana ninaamini kuna ushuhuda mkubwa  mbele yangu.............. unajua nini?????? maisha yangu yote sijawahi kupita kwenye mteremko kila unaloliona ndani yetu  lilichakachuliwa, kunolewa, na kupitishwa kwenye moto. nanilipo toka kwenye hilo jaribu nilisema,KAMA SI BWANA NI NANI????????? 

 Tunamshukuru Mungu sana kwa hili alituandaa bila kujielewa, hatukujua, na bado hatuelewi. Yawezekana tuwahi kuwaza kwa namna ya tofauti lakini Mungu alijua zaidi.(YEYE NI MUNGU ATUWAZIAYE YALIYO MEMA). kwa kweli alituandaaa..........

 Wapendwa wangu, ni maombi yangu kwenu,unapopiga magoti kuniombea hili kwa uaminifu naomba Mungu akafungue milango yako. milango ambayo siku kama hizi zikitokea uwe na backup aiseee,yaani awe amekuandaa fulani,(KWA KWELI JINA LA BWANA LIBARIKIWE) hata kama itakustua fulani, kwa namna ambayo mipango yako itavurugika kwa muda( simnajua Shetani anachelewesha ila hawezi kuzuia moja kwa moja)  lakini isibadilishe sura kamili.Wapendwa wangu naomba Mungu wangu aliye Hai akawawezeshe  kila mmoja wenu, akawape Hekima juu ya hili aiseee. naamini Yeye ni Mungu asiyetuacha tukaabika, lakini hizi backup ninazozisema mimi nimeona wengi wetu tumefungwa juu ya hili, tunaridhika........... na kama tumeridhika maana yake huna muda wala jitihada za kuliombea............Hivi unajua kuna vitu Mungu hawezi fanya kama hujamruhusu aingilie kati?????  OMBA KWA UAMINIFU

 Ninavyoamini mimi NITAPANDISHWA KUTOKA KIWANGO KIMOJA  KWENDA KINGINE . Hili halina mjadala hata shetani analijua, Sasa hutu tumajaribu jaribu  tunapojitokeza katikati ya mbio tunatupumzisha tuu, maana mbio zake  na vita vyake si mchezo shetani hatazamiki huko aliko........Kwani tulipataje ule ushindi msalabani???? haikuwa rahisi aiseee. najua YOTE YALIKWISHA  lakini je tunaukamilifu wakutosha kiasi kwamba tusijaribiwe???? Tunawakina Samweli  ambao tangu watoto walianza kupata misuko suko lakini wapi uliposoma ukaambiwa NDOTO ZAO HAZIKUKAMILIKA na wapi uliposoma ukaambiwa WALIOZUIA NDOTO WALIFANIKIWA MPAKA MWISHO?????? na vipi DAUDI, Sauli alifanya afanyalo, alitumia mamlaka, na hata alimwaga Damu ili kupoteza lengo kamili lililoandaliwa juu ya Daudi, vipi kwani alifanikwa???? au mbio tu za sakafuni??? sasa mimi ni nani hata niishi kimteremko?????? WAPENDWA NILAZIMA TUTAMBUE KUNA WAKATI WA KUPIKWA   sasa ni juu yako wewe umelipokeaje?????? na umejiandaje kukabiliana nalo???

 ukiniuliza nimelipokeaje??? ofcourse nimelia, mimi si mwanadamu Mbona hata Yesu alilia pale msalabani alisema kama nilivyojisemea mimi  leo mara baada ya taarifa MUNGU WANGU, MUNGU WANGU,MBONA UMENIACHA !!!!!!! ni ubinadamu tuu................



 Nina meeengi hayaishi ila  nimekaa hapa jamani najiuliza hiyo mipango tuliyokuwa  nayo kichwani in the next few months duuu!!!  naomba nikubali kwamba huu ni mpango kamili ulioruhusiwa yaani!!!!! nasikia sauti kabisa ndani yangu ikiniambia TULIA TULIA TULIA ( punguza kasi, Punguza kasi)  niaminivyo mimi hii sauti ningeisikia kabla ya hili pito ningeipotezea aiseee nakuikemea bila kujua unamkemea roho mtakatifu( imewahi kukupa hiyo????) kwi! kwi! kwi! all  we need ni hekima na jinsi yakukabiliana nalo baaaasiiii.

OTHERWISE TUPO POUA SANA. TUNAHESHIMU MAAMUZI YA MUNGU tunayaheshimu. maana YEYE NDIE ALIYETUTOA NAKUTUFIKISHA. ATUPAYE FARAJA NA KUTUSIMAMISHA TENA. YEYE ATAKAYEFANYA HILI KUWA HISTORIA NA USHUHUDA WAKUMUINUA YULE ALIYEKUSUDIWA. 

Angalizo, labda nisingetakiwa kufunguka hili, lakini nimejikuta najiuliza kama huwa nawashirikisha baraka kinamna fulani kwa nini na hili nisiliseme ili tujifunze??????. na wakati nimekaa mkao wakupokea zaidi maana naamini ni lazima kuna mlango wakutokea sasa nikija na ushuhuda ntaanzaje ili muelewe??????

 MBARIKIWE

Wednesday, April 9, 2014

OUT AND ABOUT


 Mpango ulikuwa kwenda dinner, hivyo ndivyo Baba watoto alitakiwa ajue hivyo, nyuma ya pazia nilikuwa tayari nimearrange anniversary package Hotelini, yaani ilikuwa Dinner, kulala body massage na breakfast.  Sasa si lazima niwaage wanangu wajue kabisa leo Mama na Baba hawapo lakini hofu yangu je Hawatamfanya Baba yao ashtukie?? Mida ya mchana Baba hayupo ikabidi niwaite wanangu niwaelezee kidogo nakuwambia nani leo atakuja kulala.. Mida imefika  Babysitter  huyo kaingia SUPRISE DADY AND MUMY ARE GETTING MARRIAGE!!(in Careen Voice huku Christabell anataka kuongezea jambo ) mimi na Babysitter tukabaki tunatoa macho maana siri inaelekea kuvuja tulijitahidi kuwavuruga watoto ndo hata hawatuelewe mwisho wa siku Muhusika alielewa kunakajisuprise ila hakujua kanafananaje.............. Mbaya zaidi mi natatizo moja la siri kwa Baba wawili aisee!!! yaani sijui jamani ntaangaika mpaka ntashtukiwa  so muhusika akajumlisha na jinsi ninavyojistukia baadae akanambia  nilishastukia kabla hata ya watoto, ila nilikuwa sijajua itakuwaje........... 

 vinginevyo tunamshukuru Mungu siku yetu ilienda vizuri mnoo.......... na haya ndo baadhi yamatukio

Mr &  Mrs S. Mbeyela

 spotted

tumefika
Bahati mbaya sana the Moet thing is not for Us........

Sisi hapa
 Wandugu hiyo Moet ilikuwa kwenye package yangu  japokuwa niliwachia hapo hapo ila  nina swali hivi kwa nini hii kitu inaletaga shida sana huko kwenye ma instagram???? inatofauti gani na mbege, ulanzi, safari,........ zote si pombe au mi ndo mshamba???? 

sio mpenzi wa chocolate ila hizi nilizimaliza.....


 Tukala, tukalala,tukaamka,mapemaaa mbio Breakfast kuwahi ibadani nilipofika ibadani  sasa kuna maswali niliulizwa sikuwa na jibu na  labda sikuelewa vizuri TUTAZUNGUMZA......

 Nawapenda