Pages

Ads 468x60px

Thursday, March 27, 2014

PART 2........



 Nimepokea maoni yenu wadau, kilichonifurahisha kuna kitu tumejifunza na kukumbushwa....... na hilo ndo lengo letu BEYOU. tunata uhalisia,tumechoka na maigizo, kile ambacho mimi na wewe tumekipitia na kututesa tusingependa na mwingine apitie, na lile lililo jema tunatiana moyo na kuliombea. zaidi ni kuamini hakuna kinachoshindikana!!!! nakinawezekana kwa njia halali ni muda tuu, huku ukiendelea kufanya nini likupasalo kufanya kwa nafasi yako.................TUNAYAWEZA YOTE KATIKA YEYE ATUTIAYE NGUVU. wafilipi 4:13

 tukirudi nyuma kidogo niliwahi kusema, MAISHA YAKO YA NYUMA YANAWEZA KUWA ADUI YAKO WA MAISHA YA SASA NA YAJAYO.  Hili nimeliona katika maisha yetu, Majeraha tulioumizwa utotoni,miaka ya nyuma yamekuwa kikwazo kikubwa chakukamilisha ndoto zetu.

 Hatuhitaji kujua zaidi habari ya upande wa pili unasemaje, ninachoweza kusema yawezekana mwezetu ana majeraha makubwa mpaka akaamua kuwa hivyo alivyo ila kilichoshindikana hapo ni namna yakutibu lile jeraha ambalo ni ugonjwa wetu tulio wengi (Mungu atusaidie)

Najiuliza??? Wanawake wengi kilio chetu ni kuwa na amani..... sasa inakuwaje wakati nyumba inawaka moto ( kukosa amani ndani ya nyumba,marumbano yasiyo ya lazima) tunaweza kuvumilia kwa namna yoyote ile tena mda  mwingine tunasema nitavulimia for the sake of my kids. Uliomba  yawezekana hata kufunga kurudisha amani. kama tujuavyo Mungu wetu ana namna zake za kujibu, ameona ili amani ilirudi ndani ya nyumba ni kuchukua kile kinacholeta jeuri na majigambo (miungu vitu,) nakuwarudisha kwenye mazingira ambayo wote mtakaa chini kusikilizana na kujadili.Mfano( aliposema wasio na elimu ndo wanamtafuta Mungu mimi kwa nafasi yangu hii simuhitaji) miungu vitu. hapo hakuna nafasi ya maelewano zaidi ya kiburi na jeuri...........Mungu kajibu maombi sasa, kwa macho yakibinadamu utahisi ni jeraha zaidi lakini, ukiingia kiroho kulikuwa kuna sababu na yawezekana goti  na chozi ulilomlilia Mungu ndo majibu. Baada ya hapo unaachiwa uendelee kutumika kwa nafasi yako, kuita amani  na kuruhusu utendaji  Mungu uendelea badala yake,  roho za miungu vitu amekuingia wewe sasa ( rejea " ninaishi kwa hela ya mke wangu anayolipwa na serikali lakini hiyo hela imegeuka kuwa masimango,nakukumbushwa yale yote mabaya niliyomtendea na mara nyingine ananifukuza ndani ya nyumba")   hapa ndipo story ina badilika  JE NI KWELI TUNAVUMILA KWA SABABU YA UPENDO NA WATOTO  NAKUAMINI IPO SIKU  IMANI ITARUDI ????AU KWA SABABU YA MIUNGU VITU AMBAYO HUKUWA NAYO HAPO MWANZO SASA MMEBADILISHANA JAPO NI KIDOGO ambavyo hapo mwanzo uliviabudu kwa mateso na manyanyaso na mwenzio aliviabudu kama silaha ya kukunyanyasia na kukunyima amani???( Ukiangalia hapa hii roho inahusika pande zote)

 Ni hivi wapendwa kama kile kinachotendeka ndani ya maisha yako ni mpango kamili wa Mungu nakuhakikishia MUNGU hawezi kukuacha.  usishtuke kwa kudhani maisha yako yalikuwa yanategemea  sh. 5000 leo umerudishwa kwenye sh.1000 ukadhani Mungu amekuacha!!!! mpendwa kaa kwenye mstari hiyo sh. 1000 utaishi nayo na kukupa amani kuliko ile sh.5000 ambayo ilikunyima usingizi na kukunyima amani. YEYE NI MUNGU ATUWAZIAYE YALIYO MEMA

najiuliza tena  nina sababu gani???? ile dhambi aliyoifanya mwenzangu miaka hiyo ambayo tayari mwenyewe ameshamalizana na Mungu wake na tena yawezekana pia hata kwangu aliikiri  labda kwa namna fulani nilionyesha kusamehe inakuwaje tena baada ya muda kadhaa lile donda  linachomoza??? nazungumzia kwa yule mtu aliyetenda na kuacha haendelei( yule anayeendelea hii topic haimuhusu)

 kwa mfano  miaka fulani ilyopita jamaa alifanya mchepuko fulani ( ALIGOMA KUBAKI NJIA KUU KABISA)  kwi! kwi! kwi! lakini uligundua na kutambua yawezekana kwa namna fulani na wewe ulikuwa sababu au la ( Wapendwa shetani halali aisee) na umekuja kugundua tayari mwenzio anataka kutengeneza maana amegundua mchepuko sio. KWA NINI TUNAKUWA WAGUMU WAKUSAMEHE??? KWA NINI TUNATAKA KUTENGENEZA MALIPIZO AMBAYO YANATUVURUGA NAKUTUNYIMA AMANI????? lipi bora  kwetu????? HIVI KAMA SI NEEMA YA UKOMBOZI MIMI NA WEWE TUNGEKUWA WAPI?????

Angalizo 

Mazungumzo haya ni kwa lile kosa lililopita ila linaendelea kukumbushwa na kututolea amani zaidi  kushindwa kutimiza ndoto zetu. kwa ile inayoendelea ( mfano mchepuko daily)hako kanahitaji kajitopic kengine. ..............na pia mazungumzo haya yamenia mahusiano ya mke na Mume ili kwa pamoja tukalitimize lile kusudi lililowekwa mbele yetu kwa ajili ya utukufu wa BWANA.

wakolosai 1:21
21 Hapo kwanza ninyi pia mlikuwa mbali na Mungu na mlikuwa adui zake kwa sababu ya fikira zenu na matendo yenu maovu. 22 Lakini sasa, kwa kifo cha Mwanae aliyeishi hapa duniani, Mungu amewapatanisha naye, kusudi awalete mbele yake mkiwa watakatifu, safi na bila lawama. 23 Mnapaswa, lakini kuendelea kuwa imara na thabiti katika imani hiyo, na msikubali kusukumwa mbali na tumaini lile mlilopata wakati mlipoisikia Habari Njema. Mimi Paulo nimekuwa mtumishi wa hiyo Habari Njema ambayo imekwisha hubiriwa kila kiumbe duniani.

No comments:

Post a Comment