Pages

Ads 468x60px

Friday, July 31, 2015

THE LOOK........


Hichi kiatu nimegundua miezi miwili ijayo hakitazamiki ha!ha!ha!ha! yaani nakivaa mpaka kinaongea kha!!


 Ka dada fulani hivi kapoleeeee!!!




 Tabasamu hili liwafikie wadau wangu wote wa ukweli......... kuko kimya lakini niwathibitishie tuu!!! God is good jamani nyie!!!!!! mi mpaka naoga sometimes........ ila unajua nini ushuhuda lazima utoke, ni vile kuna muda ulioruhusiwa  na ndio muafaka kuutoa........nyie endeleeni kunichungulia. kikubwa ndugu zangu hebu acheni Mungu ashughulike na jambo lako aisee..... unaweza ukasubiri lakini kusubiri kwake huwa kuna amani fulani  hivi isio na stress, kuliko ukitegemea sana  akili zako kwanza unaweza usipate kabisa!! au utangojaa wee mpaka ukate tamaa....... Hata ukipata huwa unakuwa umeshachoka kabisa, maana umetumia nguvu nyingi....... Na wakati mwingi kinakuja sio kivile ila kwa sababu unataka kuthibitishia akili zako kimepatikana.............. Acheni Bwana Mambo ya Mungu hata kama kuna upinzani utajua tuu upinzani huu niwa akili zako na kusudi la Mungu au shetani na kuzuia ndoto zako........ Sio kila upinzani unaoupata unatoka kwa shetani waweza kuona upinzani kumbe akili yako ndo imeipa jina la upinza kumbe ni namna ambayo Bwana anasema na wewe.
Nisemaje sasa kama sio neema ya Bwana!!!!

Nawapenda Muwe na weeend njema.

Tuesday, July 28, 2015

NIPOGO........

Wapenzi wangu mnivumilie tuu mwenzenu huku kimebana mnoo nafanya kuchungulia tuu mitandaoni .Yaani ni hivi Mwaka wa fedha umeisha june sasa mama wawili  niko busy na kusugua magari nilijisahaulisha paper work  ambazo nilitakiwa kuzisubmit tangu mwezi uliopita Serikali hizi za wenzetu ukicheza kidogo hawachelewi kuja kukufungia biashara ila mi naona wamenizoea duu ni zima moto style kuanzia shule mpaka mzigoni kama unione ninavyojistress ha!hah!aha!............ Ninavyoijua hela mkinga mie nimegoma kumlipa mtu anisaidie  so usiku umegeuka mwanga kidogo ha!ha!ha! najui Biblia imesema ole wao waugeuzao usiku............. ha!ha!ha! sio kihivi ninavyofanya mimi bwana........... yangu imekaa kiasie fanya kazi na asile ki!ki!ki!(najitetea) Wakati huo huo mzigo unaendelea during the day kama kawa yaani........., Chezea hela za mabox

Haya basi muniwone segito kidogo
Excuse ze mwanga wa jua.........

ntapita tena ndani ya wiki hii ila nawapenda mjue.....

Monday, July 20, 2015

Huyu hapa eti nani??
nazidi kuwa mcharo tuu ha!ha!ha!


kununa sasa.....

Black haigomi eti eeh??

haya kwa heri........

Thursday, July 16, 2015

SAUTI.............


 Hivi imewahi kukutokea??? labda umekuwa ukitafakari juu ya kufikia mipango fulani au ndoto. Wakati mwingine unajua kabisa ili kuifikia ndoto hiyo kuna  namna nyingi ambazo labda ni lazima uzipitie,Simnajua kuna ile yakufanya kwa nafasi yako then the rest unamuachia muweza wa yote .........maana amesema twende mbele zake tuhojiane na tumpe haja za mioyo.............

 Sasa katika ile kutafakari au kujiandaa na ile nafasi yako yenye mipango mingiiiiii.......... Gafla anakuja mtu, anaongea na wewe, kwa macho ya kawaida unaweza ukadhani labda mjamaa anajua zaidi yako ha!ha!ha! lakini ukitulia  kuitafakari ile sauti ya muhusika, namna alivyokuwa akielezea na mengineyo yote bora mradi kukupa majibu ya ndoto yako aisee kuna namna fulani yakipekee, ambayo unaanza kujiuliza hivi huyu ndo ananiambia mimi au??Basi, hii siku kwangu ilikuwa kihivyo yaani Bwana alisema na mimi kupitia kinywa cha mtu!!!  we km hunielewi kasome

Yohana10:27 Kondoo wangu husikia sauti yangu nami nawajua, nao hunifuata; 28 nami ninawapa uzima wa milele. Hawataangamia kamwe wala hakuna mtu atakayewapokonya kutoka katika mikono yangu. 29 Baba yangu ambaye amenipa hawa ni mkuu kuliko wote na hakuna awezaye kuwatoa hawa kutoka katika mikono yake. 30 Mimi na Baba yangu tu mmoja.

 haikuishia hapo nikajikuta nimefunuliwa hili neno

Yoshua11
Ikawa Yabini mfalme wa Hazori aliposikia habari za mambo haya akatuma ujumbe kwa Yobabu mfalme wa Madoni, na kwa mfalme wa Shimroni na kwa mfalme wa Akshafu, 2pia kwa wafalme wa upande wa kaskazini wale waliokuwa milimani, katika Araba upande wa kusini mwa Kinerothi, nchi chini ya vilima upande wa magharibi na katika miinuko ya Nafoth-Dori upande wa magharibi, 3kwa Wakaanani upande wa mashariki na magharibi, kwa Waamori, Wahiti, Waperizi na Wayebusi, katika nchi ya vilima na kwa Wahivi chini ya Hermoni katika nchi ya Mispa. 4Wakaja na vikosi vyao vyote na hesabu kubwa ya magari ya kuvutwa na farasi, jeshi kubwa, kama wingi wa mchanga ulio pwani ya bahari. 5Wafalme hao wote wakaunganisha majeshi yao na kupiga kambi pamoja penye Maji ya Meromu, ili kupigana dhidi ya Israeli. 6BWANA akamwambia Yoshua, “Usiwaogope, kwa sababu kesho saa kama hii nitawatia wote mkononi mwa Israeli, wakiwa wameuawa. Utakata mishipa ya nyuma ya miguu ya farasi wao na kuyachoma moto magari yao.”

unajua nini  Hapa nimesoma km adui lakini nilijikuta neno adui nimelipa jina ya mipango mirefu inayoniumiza kichwa ili kufikia ndoto yangu.Naamini Yoshua aliamini kuwa ushindi ni wake maana ni dhahili kuwa Neno la Mungu halijifungi,Ahadi zake ni lazima zitimie............ kwa macho ya kawaida Yoshua lazima aliumiza kichwa. kikubwa alikaa mkao wakungoja kusikia Bwana anasema nini juu ya hilo?Hebu jiulize ndani ya masaa 24 sio kwa vita hivyo vyakuungana majeshi mengi kha!!

Halafu unajua nini sauti ya Bwana inakujaga km kwakutekenya fulani hivi, kubembeleza fulani hivi, halafu tena inakujaga na option ukijisikia kusikiliza na kuamini au upotezee ha!ha!ha!ha! 

NIMEMUONA SIMBA WA YUDA.......... SIFA NA UTUKUFU UMRUDIE YEYE MWENYEWE MAANA SIO KWA AKILI HIZI ZANGU BALI NI NEEEMA!!!
mapicha time


 mtandio umegeuka nanilii chezea fashion wewe.......



nawapenda


Wednesday, July 15, 2015

KITAA............


Nakomaa na fasheni mpendwa ha!ha!ha!

miondoko  utajua tuu niko kitaa......

 Alikuwepo

Nikadeka kidogo ha!ha!ha! chezea wewe!!!

Monday, July 13, 2015

TOTOZ DAY....................


Leo bwana nimejikuta nimeikumbuka hii familia ha!ha!ha!ha! nimekuja kupost nikakumbuka hee kumbe nina picha zao humu sikuzipost ha!ha!ha! walikuja kunitembelea wiki km moja mbili zilizopita ila ndo kwa siku moja tuuu......... Sema nini tulikuwa tunapiga story sana na bimkubwa muda wa kukumbuka Camera duuu!!! tushachelewa baadhi ya matukio.........Tatizo Bimkubwa  mi nishakwambia haya mambo yakutuonjesha haya duuu!!hatutembeleagi watu kwa kudonoa vile Bwana kha!!! Tafadhali urudi tena tukufaidi vizuri ha!ha!ha!ha!

Aunt Zawadi na wanawe........



Wale kina nani wale?


 Leo na wawili wameonekana maana siku hizi nawafichaje? naogopa mwenzenu mara moja moja sio mbaya hii ya kila siku wakikua wenyewe wanaweza kunibadilikia chezea toto za doti com. hawachelewi kukupeleka haki za watoto haha!haa! Matukio km haya @list ntakuwa nachakujitetea kulikuwa na matukio maalum yakuwatoa ha!ha!ha! maana  kina Mama na sisi tulivyokazana kuwaanika wanetu mitandaoni kha!! yuko chooni tumemuanika,anakunywa uji tumemuanika, mara pajama,yaani 4-5 times a day unatafutiza tuu ili umwanike........... Mwenzenu najifunza mdogo mdogo km ishu ni umaarufu mitandaoni ntakomaa na the look viwalo vikiisha kauka nikuvae sina shida ha!ha!ha!ha!

Hawa hapo tena.....


Kuna mtu alikuwa anaogopa hayo majamaa

Aunt Zawadi urudi tuje tumchape huyo mchina sijui muhindi ha!ha!ha!ha



Fishing time



Cristabell sio kwa uongo huo kha!! nguvu zote hizo anavuta nini sasa........... Wadanganye Shangazi  na wajomba zako humu Mama yako hujanipata bado

Pendo naye in style ha!ha!ha!

Dogo nae alionysha Aunt yake next time nikija ujue viwango vyangu ha!ha!ha


Tumawapenda Mnooo

Wednesday, July 8, 2015

YUPOGO..............

Ila kuringa ndo najua siku hizi duu!! Camera nimeizoea naona hahahaaa!

ila  jamani tuongee ukweli make up nayo imenibeba mwee!!!

 haya basi mfanye kuniungisha basi na nyie mpendeze ha!ha!ha!ha!  bonyeza link hiyo www.youniqueproducts.com/beyourose kuona siri ya urembo wangu halafu nyie mliopo Marekani, Australia, New Zealand,Canada na Uk ole wenu muingie bila kuniungisha nawapingua urafiki ha!ha!ha!ha!


ni marufuku kuvaa maua kipindi cha winter ha!ha!ha! ila sema nini Mama wawili mnyalu ushamba kawaida nimekomaa yenye roho inataka.........

 Hadi deko limeonekana chezea make up wewe????

Nawapenda

Monday, July 6, 2015

THE LOOK...................

Nimejipenda na pozi langu...........


eti hivi rangi ya zambarau ndio purple??? ha!ha!ha! 


Gauni sweta limenibeba huku kwetu baridi ya hatari basi tuu tunakomaa na fashion  ha!ha!ha!

Nawapenda

Friday, July 3, 2015

MAMA WAWILI.................

huyu nani eti??

Black huwa hakatai mtu eti eeeh???


Nawapenda..............