Pages

Ads 468x60px

Thursday, November 27, 2014

ENZI ZA MWALIMU VS ENZI ZA SASA..............


 Hapo chacha raha ya picha kumbukumbu badala ya kupost nimeanza kujichungulia weee nikaamua niwashirikishe........Ha!ha!ha!
 Naona hapa niliambiwa niringe mtoto wa kike
Hapa sijui ilikuwa nakimbia au ndo mapozi

hapa ilikuwa mambo ya kimiss miss ha!ha!ha!

nimeboba kihehe chezea mimi nyie....

Mdau wewe ndo umenifanya nikaitafute hii picha ndo na nyingine zooote zikafanyika post Ha!ha!ha!





 Zifuatazo ni zama za sasa

 Kabby kake Slay hako






 miondoko sasa



Nimemiss mnyama duu hichi kiatu ndo itakuwa habari za hivi karibuni duu nilikisahau eti......








yaani hizi ni juzi juzi tuuu

Nawapendaaaaaa

Monday, November 24, 2014

MDAU..................


 Leo nimefurahishwaje sasa na mdau wangu???? Duu!!! Mnamkumbuka yule mshindi wetu tuliamua tujichange change tupate stationary??? Nguvu haikuwa sana Shukrani  kwa wale mliojitokeza lakini baadae mambo yakawa sio nakushindwa kutimiza ahadi zenu....... Sio nyinyi tuu Hata mimi mahesabu yangu hayakupangika sana kuelekea hiyo project. lakini kikubwa wengi wetu tulionyesha nia,Ninachoweza sema ile nia ulionyesha ilitengeneza kitu katika ulimwengu wa roho. Kile kidogo nilichomtumia kwa kweli amenifanya nitoe machozi kwa jinsi alivyojiongeza kiakili  na hizo breakdown alizozifanya. Amenitia moyo mnooo!!! Ndugu zangu hatuhitaji mamilion ili tufikishe ndoto zetu  amini usiamini senti tano inaweza kuileta ndoto yako kwenye uhalisia ni vile wewe unavyoichukulia hiyo senti tano...........

Mpaka sasa anachohitaji ni kodi tuu....... Ila kanimalizaje sasa kajipanga weeeee huku akiliweka moyoni mama wawili kati ya ahadi yake alipa nusu  kwa hiyo ile nusu yake ndo italipa rent duu!!! mi sinilijua nimesha samehewa??? Ha!ha!ha!ha! Nimeanzaje sasa kujieleza??/ Ndugu yangu nivumilie kidogo hutu tumiezi tugumu mwenzio ukigeuka huku siku kuu, huku ada,huku mgonjwa ,huku.........chezea kudaiwa wewe??? 

Hii pia nikuwakumbusha na wale mlio ahidi mkasajisahaulisha kama mimi hapa leo ndio nimekumbuka heee kumbe na deni??? lakini km mambo bado hayajakaa vizuri usijari............ Mungu akakukumbuke kwa ajili ya nia uliyoweka.Ubarikiwe

 Haya mimi hapa mnionage........
Sura ya kikazi simmeona na vazi lenyewe la leo simmeliona????
Mama yao

Nawapenda......

Friday, November 21, 2014

DINNER OUT...................


The Mbeyela's & Mjema's

The Mbeyela's

The Mjema's



Muwe na weekend njema Wapenzi............

Thursday, November 20, 2014

MBAVU ZANGU.....................


Haya ambao hamjaiona hii clip..... Huyu Dada hadithi nyingine aisee!!! kipaji kipo hapo amenifurahisha alivyomwambia nyumbani kwangu ndo hupiti otherwise mawe yanakuhusu kha!!!


Wednesday, November 19, 2014

MAMA WAWILI.........



Sasa hizi nywele tunafanyaje sasa khaa!!! nazipenda ila natamani new look japo ya wiki mbili tatu eti eeeh!!!! 



mapozi sio mengi nisije nikamwaga radhi  ha!ha!ha!

mazoezi yanaendelea mjue!!!!ila kumbe kweli yanahitaji commitment ya hatariiii.... mmmh!!! na mabox nayo balaa

Kwa heri basi.

Tuesday, November 18, 2014

THE LOOK..................

Pata muonekano wa moja wakaji outing  ya birthday girl.........        wanasema dalili moja ya ukubwa nikupenda rangi nyeupe kama kweli basi nimo  mapenzi ya white naona yamechukua nafasi kumoyo kwangu siku hizi..........
mimi hapa

Nimetoka kuangalia kansiime clip yake moja anasema yeye ana mguu haangaiki kuonyesha ila sie wenye fimbo full kutembea uchi ha!ha!ha! ntashare hiyo clip  this week....




Haya nawapenda......


Monday, November 17, 2014

HAPPY BIRTHDAY TO MAMA WAWILI.........

Wandugu mwezenu leo  ngoma 31 imeingi duuu!!!! kweli siku hazigandi.........utoto wote tupa kule, mkiona narudia  nafanya mambo ya kitoto humu ndani, mjue kuna stage sikuitendea haki mweee!!!!! (mnaruhusiwa kunikosoa ila, iwage kimtindo fulani mwenzenu kha!!! isiwe ndo kama mmepata sababu. Simnajua mtu unakuwa kama unamchukia mtu halafu wewe mwenyewe hujielewi kwa nini unamchukia ikipatikana sababu duu!! mbona atajuta!!! Ha!ha!ha!ha!)Usione watu mitandaoni tunafanya mambo kama hatujielewi wandugu stage!!!! hakuna kitu kibaya kama kuruka stage....... hasa kina sie tuliojitokea mashambani huko nyie acheni tuu ni sheeeder!!!!!

Anyway way am blessed kwa kweli   Tangu last weekend nasherekeshwa tuu, mazawadi, mawishes,mavyakula sasa aisee!!! zile kilo lazima ziwe zimepatikana kama bado ntaandamana aiseee!!!

Ntawarushia Muonekano waviji outing vyangu............  Bila kusahau Kumshukuru Mungu kwa ajili ya huyu Mwanaume hapa jamani ...................mambo mengine ya kichumbani zaidi lakini duuu!!! am blessed Ahsante Mungu .................Yaani ndugu zangu kama huwa mnaniombea huko please niombeeni niwe best wife (mke mwema)  tuu na mengine yatafuata.......


Nawapenda.......



















Thursday, November 13, 2014

TUZUNGUMZE.........



 Nimemaliza sehemu ya kwanza ya kitabu, Pamoja na yote kuna hili nimeona niwashirikishe.............

Anasema, kuna siku walikuwa na Dada yake mahali fulani, waliamua kwenda kujificha kwa muda baada ya muda mrefu wa maisha kuwatenganisha(umbali na majukumu). Moja ya maongezi yao ndani ya siku hiyo ilikuwa nikukumbushia jinsi walivyokuwa walivyolelewa,nani aliwafanyia nini,na vitu km hivyo............

 Maongezi yao namapokeo yalikuwa yanagongana kidogo ,hasa pale mmoja wao alipokuwa anakumbuka mambo yalioyomuhuzunisha,nani alimdharau,nani aliyemwambia maneno yanayomfanya ayakumbuke mpaka leo na kumjeruhi........Kitu ambacho kwa mdogo mtu(mtumishi) kilimpa wakati mgumu kila alipojaribu kufanya ushirikiano na Dada yake kwa wakati huo, ilikuwa bahati mbaya maana hakuweza kukumbuka na kama akikumbuka anashindwa kulielezea lilianzaje nakuishiaje hivyo ilimbidi awe anamuuliza Dada mtu, Hivi alivyosema vile ilikuwaje?alianzaje,Ulimfanyia nini, na mengineyo ili tuu, ajaribu kufanya ushirikiano........... Haikuwa kama alivyotegemea zaidi alimfanya Dada mtu akasirike nakumuona anaigiza  mwisho wa siku alijitahidi kujitetea.............. Dada mtu akamwambia UNAJIFANYA UMESAHAU SAWA NDIO MAANA ULIKUWA UNAITWA PRINCESS...............PRINCESS ni jina alilokuwa anaitwa kama nick name akiwa mdogo lakini hakuwahi kulitumia kama jina. Mara baada ya Dada mtu kumkumbusha  alijikuta ameingia kwenye tafakari ..................... Mwisho wa siku akatunga kitabu kinachoitwa PRINCESS.

 Niliwahi kuzungumzia hapa kwa habari ya kubeba mizigo, maumivu,masimango,makunyanzi ambayo yametukwamisha sana katika kutimiza ndoto zetu.Tumesahau kwamba Imeandikwa 

Msiyakumbuke mambo ya kwanza, wala msiyatafakari mambo ya zamani.
19  Tazama, nitatenda neno jipya; sasa litachipuka; je! Hamtalijua sasa? Nitafanya njia hata jangwani, na mito ya maji nyikani.

Wapendwa wangu kama tusipojifunza kuachilia........ 

Majibu ya ndoto yako yanaweza kuwa ni hadithi za kale, 

Tunajifungia milango sisi wenyewe wakati mwingine 
tunaamini Mungu amechelewa kutujibu ,kumbe ni sisi 
wenyewe tumekaa mlangoni, tumejizuiya. 

Wapenzi wangu kama nimidomo ya watu basi huwa nahisi 
leo nisingali kuwa hapa, Kusudi la Mungu ndani yako 
aliharibiwi na Mwanadamu awaye yoyote............. Niliwahi 
kusema hapa Mama alivyokuja kuna vitu alikuwa 
ananikumbusha tena hasa kwa wale ambao kwa sasa ndo 
tuko karibu mnooo!!!!  Kiukweli na mimi nilijikuta naingia 
kwenye shida kama mtumishi hapo juu, (Namuelewa kama 
mzazi ni jinsi gani aliumia hasa mtu alipomzungumzia 
mwanao negative). 


Ninachotaka kusema Damu ya Yesu imekusafisha huna 
haja  yakutafuta tafuta laana yako imetoka wapi 
 TAZAMA NITATENDA NENO JIPYA.

Tumia muda wako kumuuliza Mungu kwa habari ya kusudi la maisha yako.

HUJACHELEWA WAKATI NDIO HUU..........

NAWAPENDA

Tuesday, November 11, 2014

USHUHUDA........

Haya ndugu zangu mi ni mmoja kati wale ambao inapofikia kwenye neno la Mungu,  huwa sijishughulishi sana na vitabu zaidi ya Biblia yangu , ukiniona nimenunua ujue labda tu nilitaka  kuchangia tu nakumtia moyo muhusika, mi mwenzenu Biblia  huwa naona imejitosheleza.................. Kwa kusema hivyo sijasema tusisome vitabu vinavyoambatana lakini inabidi tuwe makini sana maana duuu!!!! wandishi siku hizi tuko wengi mjue??? Ki  ukweli unahitaji Roho wa Mungu akuongoze, ujue muandishi aliandika kwa kuongozwa au kwa hisia  na mara jingine huwa no kuongozwa wala hisia wanatumika ........mpaka ukaje kujua  umechelewa  na umeshajifunga kwenye maagano  ( nilimsikia Teddy Kalonga juzi kati yalimkuta sijui picha imeendeleaje best yangu, simuoni Instagram lakini namuelewa sana........ ni kazi sana kujua siri ya mtu anayetumika na yeye anajua kabisa yuko kikazi aiseee)

Ilishawahi kunikuta kipindi fulani kuna mtu akanishawishi kuingia kwenye maombi kwakuongozwa na kitabu cha nabii fulani hata simjui nilielekezwa ninunue online.... Duu nikaenda kununua hiyo kununua tuu masharti kitabu hakitakiwi kushare na mtu ye yoyote zaidi ya mnununuzi, na pia kuna stage ukimaliza hiki unatakiwa ununue kile mmmh!!! haya nikanunua   kilipofika nyumbani huo mwanzo tuu masharti ya Muda wakuomba ni lazima yazingatiwe,unapotakiwa kusema hiyo sara unatakiwa kutamka kwa sauti..........  mmmh!!! Biblia yangu inasema unapoomba uingie kwenye chumba chako cha ndani na Mungu wetu anasikia (kwa uelewa wangu Maombi yangu yasiwe kwanzo kwa wengine) sasa wanangu, Mume wamelala  mimi napiga kelele saa sita za usiku kisa ndo masharti ya sara,chakuchekesha zaidi ukimaliza hiyo sara hadi kizunguzungu unakipata......!!!! mpendwa huchelewi kujipa moyo duuu!! leo nimemponda shetani hadi nimesikia kizunguzungu kha!! wapendwa na sio sa nyingine!!!!!

mwenzenu mwisho wa siku nilichoma moto !!!maana siongozwi na masharti bali kwa roho mtakatifu. 


Anyway,
 Wiki mbili tatu zilizopita nilibahatika kumsikiliza huyu mtumishi wa Mungu JANINE KUBALA. usiku kabla ya siku kuna vitu fulani nilikuwa navitafakari kwa namna fulani fulani...Nilichomshangaa Mungu ile asubuhi nimeenda kumsikiliza huyu mtumishi, ni kama alitumwa aje anipe yale majibu ambayo nilikuwa nayatafakari usiku uliyopita,  na baada ya hapa alianza kutoa ushuhuda jinsi na namna ambayo Mungu alimuokoa mpaka hapa alipo.

Wapendwa wangu, huyu Dada niliona kama niliwahi kumsimulia ni jinsi gani hii Neema ya Bwana ilivyonitoa kwenye shimo la takataka yaani sijui nisemaje??? kilichonifanya nitofautishe ni yale mazingira  aliyofanya nakupitia hayo, Vinginevyo ningemdai $$$$ zakutumia ushuhuda wangu wakati sijamruhusu ha!ha!ha!  Kitu ambacho sijawahi kujionea aibu inaponibidi huwa nashare bila kumugopa wala kumuonea aibu mtu........ ila mara jingi ninapo share hasa nawapendwa wenzangu  najionaga kama mimi ndo nilikuwa mtoto mbayaaaaa....... Unajua kwa nini??? ngoja nimsome huyu Dada nijue kama niwazacho mimi na yeye ndicho alichokuwa nacho. 

ntakuja kushare hapa......

Kiukweli amenifanya nikinunue hiki kitabu chake nijue zaidi hasa pale kwenye ushuhuda. 

 Nanikikimaliza hichi ndo kitabu changu cha kwanza kukisoma nakukimaliza.

Thursday, November 6, 2014

THE LOOK...................


Nyie mwenzenu kuna kitu natamani mnoo nikizungumzie......... ila sema ndo hivyo najitahidi sana nisizungumze kwa sababu tu nimehisi,nimeona,au wakati mwingine huwa kinatakiwa kiishie kwangu mwenyewe sio lazima niwarushie si mnajua mapokeo huwa tofauti????  ila kikiendelea kukaa kichwani kesho nakizungumza........ Si mnanijua mi sipendagi masumbuko ya moyo kama nasumbuka huwa najitahidi sana kukipotezea nikiona kila nikijaribu kukipotezea bado kinakuja zaidi  na kinanifanya nijipe muda wakukitafakari basi huwa naruhusu  kukitafakari halafu namalizia kwakuzungumza ili nifunge ukurasa kabisaaaaa....


Haya  ndo muonage the look kabla gym haijatutengeneza mapaja kama Serena Ha!ha!ha!(sio mimi mdau wangu kanipa hiyo) vinginevyo lawama tutampa model wetu Flaviana lazima atakuwa ametulisha sumu!!! SIO MIMI WANDUGU mi nimekuwa inspired tuu .......Kwi!kwi!kwi!

usinione hivi no pumzi lege lege ila sasa niambie nisugue Gari wee utajuta chezea $$$$$ wewe?????




Nawapenda

Tuesday, November 4, 2014

I AM INSPIRED........................

Wandugu mmenisikia mara nyingi nikisema natamani vi kilo viwili vitatu kwenye huu mwili.......  Na kama ni kuchagua kati ya kupungua au kubaki hapa nilipo aiseee  i can do anything kuhakikisha usinishushe kwenye hivi vikilo najionaga kama niko kwenye danger zone kwi!kwi!kwi!.......... na hiyo ndosababu pekee inayonifanya nitamani nipate vikilo vingine viwili vitatu....... lakini visizidi vitano khaa!!! Msinielewe vibaya huwa napenda sana kumuona mdada ana umbo lake balaa halafu yuko curved  (yaani mbele flat nyuma mzigo wa haja) Ila sijawahi wish kuwa mimi!!! nahisi kwa sababu hata huto  tukilo tuwili ni shughuli kutupata ha!ha!ha!ha!

 Anyway sasa kuna siku nilimsikia Flaviana anasema mwili wake ndo kama wa Mama wawili hata ulishe vipi  hauna majibu ila ukiunyima kidogo ni full kuonyesha mifupa........  duu nikajipa moyo kumbe tuko wengi eeh!! mwili wa Mama wawili nikitaka kupungua nipe wiki tuu utanihurumia!!!!ndo maana huwa najiona niko kwenye danger zone...... Sasa kama mwezi nikamwona Flaviana instagram anatupia vipicha vya namna hii....... Duu!!!! nilimuoneaje huruma???  nikajisemea hata kama kazi yake inamuhitaji awe mifupa mmmh!!! nikaendelea kumchungulia nione hatima yake ...........wakati huo huo juzi kati nilitakiwa kwenda mtaa wa pili mwendo kama wa dk 5-7 nikaamua kutembea yaani nilifika hoi  nahema utafikiri nimepanda mlima kitonga!!!wakati wakurudi nilitamani hata niite tax imagine!!!!

Basi bwana nikagundua kuna haja ya mazoezi otherwise nakaribisha vingine........ So Yes nimeendelea kumfatilia nikagundua kumbe unaweza kumaintain na bado ukafanya mazoezi, Jana nikafanya maamuzi nikaingia huko kwenye mijengo nimejiandikisha nna trainer wangu mwenyewe ila amesisitiza kama nilikuwa nakula milo mitatu  nahitaji kufanya mitano snacks between the meals ndo mpango( Guess what!!! Baba wawili ananisupport na yeye ameambiwa haitaji kuvuruga mlo wake zaidi yakuongeza) so kidizaini kama wote tutakuwa tunadeal na kubuild our bodies huku tukiwa fit and health(Subirini soon mtaona ma six pack na maNick Minaji shape ha!ha!ha! joke)

 Twende kazi sasa wale wa team health, sijui fit mnipokee mwenzenu mweeee na nyie wenzangu na mimi mnaovihurumia vinyama vyenu Wandugu mpango nikuwa na afya na kuwa fit ILA ningekushauri kuwaona watalaam wenyewe maana kama mimi nimeambiwa kukimbia ni Big no!! maana sina calories zaku burn nakuongeza kiwango cha mlo kitu ambacho kama nisingewaona watalaam nisingefanya.

 Ahsante kwa woote walionishawishi maana duu kila kona kwenye mablog,insta,facebook,tweet yaani habaree ni teamfitness,teamhealth,............ nilikuwa naskip tuu nahisi hainihusu... Kwi! kwi! kwi!


NIMEKUTANA NAYO........

Nimeukuta huko kwenye wall ya mdau wangu imenigusa!!!! nimeona  nikushirikishe na wewe labda utapata kitu  au sio..........

LIFE BEGINS AT 40! So how old are you?

Huo ni msemo wanao waingereza.
Today is your future kwa taarifa yako.. Ulipokuwa mdogo ulisema nikiwa mkubwa nitakuwa na gari na nyumba nzuri wazazi wangu wataishi hivi na vile. Je unayo? Je imetokea? Maybe yes. But maybe no.
Kama haijatokea je bado hujawa mkubwa? Basi kama ni mkubwa ujue kuna kitu hujafanya.
Utasema tena nikifika miaka 40 nataka niwe na hiki na kile watoto wangu wasome international skul nk. Subiri uone miaka inavyoenda. Usishangae kufika 40 bado umeajiriwa kwa mtu na anakugombeza kwa nini mwanao anaumwa kila siku unachelewa kazini. Kazi nyingi. No bright future. No enjoyable present. Just existing and not living!
Hapo ndo unawaza kufuga ng'ombe wa maziwa kibamba kwenye kiwanja chako cha miguu 12 kwa 15! Wenzako wa umri wako hapo unasikia wameanzisha bness in Australia. Wamenunua kiwanja Mbezi Beach kwa 300M! Wanamiliki Apartment Johannesburg. Wakienda UK wanaenda kula The Ritz (Google that). Wanasomesha watoto zao the finest schools available wewe wa kwako wakati huo wamekosa nafasi Makongo wameenda Kibamba Secondary School wanapanda daladala sita kwenda na kurudi full kutukanwa na makonda.
Wenzako in their 40s wanasaidia wasio na uwezo katika jamii wewe ndo kwanza ukipokea simu kutoka kijijini una-mute! Wenzako in their 40s wakisikia kuna ujenzi wa nyumba ya ibada wanachangia 5M kimyakimya.. Wewe ukitoa laki moja basi mpaka mtaa wa saba watakujua! Halafu unashangaa wanazidi kuinuliwa. Mwenye nacho ataongezewa au hujui? Na asiye nacho..... (Malizia)
Wenzako in their 40s wana exposure ya uhakika. Walishafika kuanzia Sauzi, Botswana, Mozambique, Kenya, Ethiopia, Ghana, Naija, mpaka Egypt, The UK, Australia, Hawaii, Mexico, Croatia, The Netherlands, Switzerland, US, Panama mpaka Puerto Rico, Brazil na jirani zake, Hong Kong, Australia, Japan, China, (Incredible) India, Thailand, Singapore, New Zealand, Comorros, you name it..!! Wewe hata Kampala hujawahi fika. Kila siku Tegeta Posta ndo ruti yako miaka 15 mfululizo eti unatafutia watoto maisha! Unaishi au unaisha?
Acha mawazo mgando. Hiyo ajira ifanye serious sana tu lakini kwa muda tu. Jiandae kusimama mwenyewe. Kwani hujiamini? Na Mungu naye humwamini? Changamoto ni sehemu tu ya kufika kileleni. Don't be afraid. Don't dwell in that comfort zone!! Unasubiri kiinua mgongo? Utaenda kukiinvest wapi na kwa nguvu ipi. Na utaenjoy retirement kweli kama at 60 yrs ndo unafungua duka la vifaa vya ujenzi eti vinalipa. Kwa nini hukufungua ukiwa 30 ili uone vinalipa au la. At 60? With due respect.
Suffer the pain of discipline now. Or else you will suffer the pain of REGRET. Halafu ukianza kuregret ndo pressure zinakuja, stress, nk mwisho unawacha hata hao watoto in a far worse situation than your own lifetime.
Life Begins at 40 my friend.. How Old Are You?

Monday, November 3, 2014

NIPOGO.........

Niaje wapendwa wangu???Bila shaka utukufu wa Bwana umewafunika na mnaendelea kupambana kwa namna tofauti......Kikubwa be yourself yaani katika kila kitu..... Usisononeke,usijikunyate, usijutie ila jifunze kupitia,Bado hujachelewa, Wakati ndio huu,Pondeka mbele za Bwana,Nasema hivi mkabidhi Bwana.............................

Basi sawa tuendeleee
Huyu hapa eti Mama wa nani????
Duu kumbe huwa naweza kutabasamu eti eeh???

Anatafakari nini???

Haya Nawapenda mnooo.....

Mbarikiwe