Pages

Ads 468x60px

Wednesday, September 11, 2013

TAHADHARIiiiiiiiiiiiiiii...............

haswa kwa wenzangu na mie tulio nje ya nje.............

 Wandugu Deni ni lazima ulipe natusipende sana vya bure .... ukiona kitu kimekuja kimteremko fanya utafiti ujue kimekujaje kujaje kabla hujakitumia........ kila siku huwa napinga watu wanaopenda mteremko sijui na mimi nimeingiaje katika hili nimejikuta tuu............... yaani hili ni pepo lenye idara zake inabidi kuwa makini mno maana linakuja kwa njia nyingi ili likupate..............



 Mama wawili nimepatikanaje???? yamenikuta km ungeniona jana ungenihurumia aisee.....

ni hivi nilikuwa natamani mno hizi hela za serikali huku kuna watu wanapewa bure  bure mi huwa zilikuwa zinanitia wivu kwa kweli.............yaani mtu kakaa nyumbani hana kazi analipwa mi mama wawili natesekaje hata sitiwi moyo....... hii ni kama unauraia...... mama wawili kila nikijisogeza naambiwa sina vigezo ( vigezo vinaangaliwa kipato cha familia kama kipo juu ya viwango vyao we endelea kukomaa na kulipa tax wenzio wapewe vya bure.........) 

sasa nikapata upenyo fulani wa kwenda kuwambia wandugu kipato cha familia yangu kimepungua kwa sasa na mimi naomba vya bure kwi! kwi! kwi! huku najua hiyo ishu ya miezi miwili mpaka mitatu na haikuwa kiivyo insurance ilikuwa bado inatulipa ila kwa sababu ya vya bure sikupoteza muda aisee....... hiyo ilikuwa 2011.............nnachokumbuka  waliniambia hivi , mara baada ya kipato kurudi kwenye hali yake rudi haraka kutupa taarifa au tupigie simu. 

kwanza mpaka leo bado huwa nawashangaa kipato changu kilivyorudi kwenye mstari tuu mwezi wa kwanza nikatumiwa barua kunikumbusha km kipato kimepanda niwape taarifa..........Mama wawili kimoyoni najisemea mnanitega eeeh!!haji mtu huu ndo wakati wangu wa bure na mie mweeeee!!! wakaendelea kunilipia asilimia fulani day care na kwenye account yangu vi $ 40 kila baada ya wiki mbili nilikuwa sikosi....(nilijua nawakomesha) mara hee mwisho wa mwaka naletewa deni hilooooooo natakiwa niilipe serikali mbaya zaidi no more $ 40 wala kulipiwa day care na barua ikijieleza kipato chetu cha familia halali  hapo chacha...............

sikuwa na grounds zozote zakujitetea  kilichobaki nikujieleza wandugu siwezi lipa hili deni mara moja naomba nilipe kidogo kidogo......nikaambiwa hilo deni sharti lilipwe ndani ya mwaka yakapigwa mahesabu ya mwezi duu mama wawili nikairudisha hiyo hela ki tshs ninachoona ,mbele yangu ni ule mshahara niliyokuwa nalipwa kama afisa masoko bongo kwa miezi km miwili mpaka mitatu....... yaani bila maelezo.
nikaanza kulipa mwezi mwingine silipi yote au naruka mwezi nawapigia simu mwezi huu sijakaa sawa ntalipa mwezi ujao  wenyewe wananiitikia tu sawa, kumbe lile sharti lazima ilipwe ndani ya mwaka............
sasa jana sijui ndo mwaka hata sijataka kujua mahesabu yao nimepigiwa simu nikiambiwa hivi,

 mpiga simu: wewe ni Rose.............,unaishi..............
mama wawili:   ndiyo
mpiga simu: tunaomba utupe  jina la ukoo,tarehe /mwezi/mwaka wa kuzaliwa ilitukwambie kwa nini tumekupigia

mama wawili :( kwa jeuri) siwezi kukupa hizo details sijui wewe ni nani ???

mpiga simu: ok tumepewa taarifa zako kutoka sehemu fulani unatakiwa kulipa kiasi fulani kweli???
Mama wawili: ndio, ni mimi jina langu la ukoo..... tarehe........ nilitaja vyooooteee nahisi  ha! ha! ha! ( hapana chezea hii serikali aisee)

mpiga simu: tunakupa option 2 zakufanya ndani ya dakika hii 1.tupe namba za kadi tutoe hiyo hela sasa hivi au tuingie kwenye account ya Mumeo tutatoa na riba yake ama vipi tukufungulie file...............

wandugu ndani ya sekunde chache  nililiona pepo la rushwa likinijia( niliona picha moja ya kibongo sijui km ipo bado ile kuchenji vibuku mbili kwa ajili ya traffic njiani aisee,mbaya zaidi huyo mpigaji simu yuko kikazi no njaa mweee...........nilishia kumwambia ngoja nichukue kadi ile natafuta wallet machozi yananitoka ninachoona mbele yangu nikajumba kaheshima kavyumba vitatu pale kijijini kwetu............jinsi nilivyokuwa naithaminisha hiyo hela.........duuuuuuu!!!!

DENI LIMEISHA ILA MAUMIVU NDIO BADO NINAYO .........KISA KUPENDA VYA BURE

najiuliza matokeo yake km hilo deni limekukuta umefulia...... ndio yale yale mambo ya mnada mnakuja kuuziwa hata vile mlivyovitolea jasho la haki vinapotea na usiombe ufunguliwe file nchi za watu aisee bora nirudi Bongo................

yaani siruhusu pesa yoyote ingie mkononi mwangu bila kujua imetoka wapi..............

HAKUNA MTEREMKO DUNIANI WANDUGU TUKOMAE NA HAKI YETU NA BWANA ATATUKUMBUKA NA WALA 
HATA TUAACHA.................

poleni kwa gazeti

6 comments:

  1. This comment has been removed by a blog administrator.

    ReplyDelete
    Replies
    1. This comment has been removed by the author.

      Delete
    2. Wandugu nimetoa hizo comment nimeona hazijengi kwenu wadau iko kimimi na mwandikaji zaidi...... Anaumwa mawazo ngoja tumuache aendelee kutuletea chicken wings recipes maana hana analojua.....

      Delete
  2. Hehee mama wawili mwenza umenifanya nicheke huku nakuonea huruma, pole Mama ila kweli veta Bure uponza naviogopa balaa, nawaona watu wanavyozienjoy ila nawaacha tu nakula hubby anachonipa japo kweli ukiingiwa pepo la tamaa waweza fika hata mbali Na hapo. Kheri umeweza kulipa Mungu atukuzwe Na maisha yanaenndelea huku tukijifunza Jambo. Kheri limepita salama

    ReplyDelete
  3. Hahahah..nimecheka..basi niliwahi kuwekea hela kwenye account ya bank.kimakosa..wee acha nifurahie mbona nilikuja kuzilipa..

    ReplyDelete