Pages

Ads 468x60px

Monday, October 13, 2014

NA MENGINEYO.............


 Humu ndani tulijionea jinsi movie inavyotengenezwa

 na sisi hao tunatengeneza kamovie ketu ha!ha!ha!

spotted 
Mama wawili in action chezea mimi nyie??? na vazi langu sasa!!
humu ndo ilikuwa hatari ............kujieleza nashindwa bwana!!! nyie angalieni picha tuuu kwi!kwi!kwi!


mweeeeee!!!


sinikajua moto kweli na ushamba wangu weee!!! nilipiga kelele nahisi wote walijua mpori pori kavamia jiji.........

Story ya huyu Scooby nini sijui..........sina hamu
Bwana sinikajua ride ya kawaida kumbe inakonipeleka ni roller coaster iko ndani kwa ndani..... humo ndani giza kujitoa huwezi yaani ni lazima  safari uimalize weee niliita majina yote humo ndani ungemsikia mwanangu anavyonihurumia mwee........ mumy we r going to finish soon, mumy dont cry, Mumy .......,Mumy ......... mtu mzima nalia mwanangu mbona hukuniambia km ndo hivyo,Slay weweeee....... Slay mwenyewe hayupo anatusubiri nje na Cristabell. Cristabell haruhusiwi so tukafanya zamu zamu huku Careen akitusindikiza....... Sirudii tenaaaaa!!!!

mbaya zaidi hayo madudu sasa yalikuwa yanakuja usoni kabisa kunitisha duu!!!!
mimi eti ukanibingilishe humo juu khaaa!!!


mwenzangu huyu Bwana ikifika kwenye hayo madude napewa la uso ,Mama we kama hutaki kaa pembeni  tutaonana nikimaliza.........kwi!kwi!kwi!

 Hapa mwenzenu nilizidi kujifunza hawa watoto wa dot com nikukazana kuwafunika kwa damu ya Yesu basi .................
 Unajua nini??Wanangu hawaangalii haya mavitu nyumbani kwangu nawanalijua hilo. kuna zile ambazo nimezipitisha na nyingine nimarufuku, sasa tulivyoingia humu ndani madude yote wanayojua wao nimarufuku kuangalia yalikuwepo ......... mmoja akanipiga swali la kizushi Mama mbona leo umetuleta tuangalie wakati nyumbani ni No??? nikawajibu leo mnaangalia kwa sababu sio video ni live na mko na Mumy & Dad. wee Baada ya hapo watoto walianza kutaja majina ya hayo madude kama wanashindana nani anajua zaidi...........Mie na Baba mtu tukatoleana macho na kuulizana haya mambo wamejulia wapi?saa ngapi?na lini?    Mwisho wa siku utaumiza kichwa ........fanya uwezalo kama mzazi then mkabidhi Mungu akusaidie yagizani usioweza kuyaona aiseeee...........mbaya zaidi ya gizani huwa wanayafanyia bidii kuyajua kuliko................



Kwa pamoja tunawapenda.........

1 comments:

  1. Tunakupenda pia pamoja na familia yako....yaani umenichekesha sana kuhusiana na hiyo rollercoaster ya kutisha.....mpaka machozi. Ubarikiwe sana.

    ReplyDelete