Pages

Ads 468x60px

Wednesday, February 5, 2014

SEMA NENO TUPONE WAPENDWA.......



Hello dada Rose,
 Jin ala bwana libarikiwe.Mara ya pili hii nakuja kwako.Mara ya kwanza niliomba ushauri juu ya mahusiano ya ndoa.Nakushukuru sana. Leo naomba niate maoni yako na wasomaji wako kuhusu yafuatayo

1.Nimepata hela kama milioni nane hivi nnawaza je nijenge nyumba ambayo itaishia msingi kwa sasa afu ntakuwa na dunduliza  tu laki laki mbaka nyumba iishe God knows when? au je niifanyie biashara? je biashara gani kwa huku Tanzania itanifaa wadau wako watanisasaidia.Nasikia woga sana kuanza biashara nnaweza kusali vipi ili Mungu anisaidie kama ni biashara iwe ya mafanikio?mimi ni mfanyakazi wa kuajiriwa.Lakini ndoto yangu ni nikifiaka 40 niwe independent na ajira.currently nna miaka 28

2.Napenda wanangu wasome na wapate elimu bor.kuna shule nilienda kuuliza nikakuta dola 2000(agakhan kindergarten) kwa mwaka.mm na mume wangu tunaueweo wa kawaida sana lakini tukijiminya twaweza mlipia japo huyo mmoja.wengine(wawili) watosoma shule average au labda MwenyezI Mungu atatufungulia milango huko mbeleni nao tuwapeleke huko.Swali langu jeis it worth it kumpleleka mototo kwenye hiyo shule? na je ni vibaya kumpelelka huko wakati wengine wanaenda shule za average?

Naomba nipostie my dear nasubiri busara za kimungu kutoka kwako/wasomaji wako ili nifanye maamuzi

Yours mama watatu

Dada nimefurahi kuona una ndoto tayari na mikakati umeshaianza yakutumiza ndoto yako, Ubarikiwe na Mungu akutangulie.
 labda na mimi niseme kidogo  kama ningekuwa nipo kwenye nafasi yako,  nafikiri ningeanza na hifadhi (nyumba)kwanza maadamu uhakika wa mshahara kila mwezi mimi na mume upo, nafikiri  kwa jinsi ulivyojieleza bado kuna nafasi fulani ya nyinyi kujinyima mkapata saving ya $ 2000 kwa mwaka, Basi nyie  mpo kwenye nafasi nzuri yakumalizia nyumba japo wewe huamini kama itawezekana.... Binafsi nimejifunza ujenzi wa Tanzania unatakiwa  nia tuu... otherwise huwezi kujenga na utakuwa unaogopa kila siku.  Nina mifano mingi mnoo kwa watu walioamua wakiwa hata uhakika wa million hawana lakini waliweza. mmojawapo akiwa ni Mama yangu ananyumba tatu mpaka sasa hata sijui amewezaje zaidi yakumtumia hela ya kula.

Kama ningekushauri Biashara Dada ntakudanganya nipo kwenye hiyo industry na nimeanzia Tanzania  hivyo ninakaulewa kidogo. Biashara inahitaji plan, ujue unataka kufanya nini, nakufanyia research ya hali ya juu kabla hujatupa pesa kwenye hiyo Biashara. na pia nijuavyo mimi hiyo pesa kama utataka kufanya Biashara  ili kuilinda itakulazimu uache kazi ili uitete hiyo pesa vizuri kitu ambacho sikushauri bado sana kwa wewe kuacha kazi kwa sasa  ili uweze kutimiza hiyo ndoto yako. na kama utafanya kazi na biashara kunauwezekano ukaipoteza hiyo pesa. ni uelewa wangu tuu.....

Kwa habari ya mtoto mmoja kwenda private na mwingine kayumba  binafsi ningewaacha wote shule ya sasa, huku ukiwa makini kama mzazi kuwasaidia kwa namna Mungu atakavyokuongoza ili wawe na uelewa na kukua vema. Hii nazungumza nikifikiri hao watoto ni wadogo wako kwenye level za primary lakini wangekuwa labda kwenye level ambayo naona Mungu atasaidia huyo mkubwa atamaliza level fulani ndani ya miaka miwili mitatu na akapata kazi akanisaidia kuwalipia wadogo zake ningefanya hivyo, lakini kwa sasa nahisi safari ni ndefu mno.  Naelewa ni jinsi gani ungependa  labda mwanao hata mmoja awe kwenye hizo  Shule, usijari sana Mama tumetokea huko huko kwenye kayumba na wazazi walitamani hata sisi twende huko  hatujutii kwakweli maana leo tuna ushuhuda  tumeuona mkono wa Mungu.( hii kama huna uwezo lakini kama una uwezo mpe mwanao the best you can)

 Nikiwa nimejaribu kugusa kila eneo nililotakiwa kusema  naomba nimalizie kwa kusema  nimepiga mahesabu  fulani hapa naona kabisa kwa jinsi ulivyo na ndoto na ukaamua ndani ya miaka mitano hadi saba wewe uko kwenye nyumba yako ya kawaida tuu, ambayo itakufanya usave  hela uliyokuwa unalipa kodi ya nyuma  plus $2000 uliyokuwa unaweza kusave tayari ndani ya miaka mitatu wewe  unakuwa na nafasi nzuri yakuanzia Biashara ambayo umeplan na kufanyia research wakati unasave ndani ya hiyo miaka mitatu. Mpaka hapo  utakuwa na miaka 36 -38 unamiaka Kadhaa yakusimamisha hiyo Biashara na Muda huo huo umeshatengeneza mazingira mazuri yakuwapa watoto the best education watakayoitaka maana tayari watakuwa na umri mzuri wakukueleza nini wanataka na wewe ukawasaidia.( kama umeweza kupata million 8 mara moja hebu mwamini Mungu kwa zaidi mpendwa.........Inawezekana)

HAYA YOTE YANAAMBATANA NA MAOMBI,KUJIAMINI NA KUJITAMBUA.
 Itapendeza zaidi kama hayo maombi yatakuwa yamapatano na Mumeo , mkubaliane kwa habari ya ndoto. umbeeni uzima , afya na ulinzi hasa kwa watoto. MUNGU AKAANGALIE HAJA ZENU NAKUPATA KUZITIMIZA.


8 comments:

  1. KWAKO, MDAU,

    8MILLION can go beyond msingi ila inategemea ni nyumba ya aina gani.... Mimi ni Mdau nitamtupia inbox facebook Rose so that we can chat na muhusika direct ni mweleze how can 8 Million do wonders, USIPENDE KUSIKILIZA STORY ZA WATU MSINGI MILLION 10 ETC HOW CAN MSINGI KUWA 8 MILLION WHILE,

    SAND 18TON NI 120,000 FANYA 2 ITS 240,000
    KOKOTO 18TON NI 180,000 FANYA 2 ITS 360,000
    TOFALI 1000 EACH AT 1500 WHICH IS THE MOST EXPENSIVE TENA JKT 1.5 MILLION
    CEMENT I BAG 15600 FANYA UNANUNUA 50 ITS 780,000
    NONDO NI 14500 FANYA UNANUNU 30 ITS 435,00

    TOTAL HAPA NI 3,315,000

    NA HAPA MIMI NIMEPIGA CALCULATION ZA FIVE BEDROOM HOUSE
    BILA LABOUR CHARGE WHICH CAN BE KAMA LAKI NANE AU TISA.

    PLEASE LET NOT PEOPLE WAKURUDISHE NYUMA KWAKUWA HAWATAKI MAENDELEO YAKO, ANYONE CAN BUILD ITS JUST PLAN AND TO STICK WITH THE STRATEGY YOU HAVE

    QR.

    ReplyDelete
  2. Mdau nisamehe kama nitakukwaaza ila hakuna kitu kizuri kama kujivunia nafasi ambayo Mungu amekuweka katika wakati huo kwani wako wanaosoma hizo shule na ni bure kabisa mwombe Mungu amfanye mwano kichwa na sio mkia kama alivyoandika katika biblia yale maandiko ni kwajili yetu tumepewa tuyatamke tukiamni na kuyakubali pindi uombapo na kuwakbidhi mikonomi mwake kila kitu kinawezekana katika yeye, kama wewe ni msomaji wa biblia unafahmu hili lakini ukipata muda usome habari ya mtumishi wa Mungu Ayubu ni kama hadithi lakini utaona yakuwa haya yote ya dunia usikimbizane nayo sana kwani wanaweza kusoma kokote kule na Mungu akachuku vyote ulivyonavyo ndani ya dakika moja, Mtangulize Mungu kwakuwa toka siku ya uumbaji wa dunia hii alikuwa anaujua mwisho wako na yote utakayo yapitia sikiliza suti yake na yote utakayomwomba atakutimizia ila kumbuka ni katika wakati wake, WAKATI WA MUNGU.

    QR

    ReplyDelete
  3. asante QR bakuelewa vizuri wala hunikwazi,asante pia mama wawili..Naendelea kuwasikiliza wapenzi.
    mama watatu

    ReplyDelete
  4. KMA NITAKUWA NAKOSEA MNISAMEHE WAUNGWANA NI HVI NAOMBA MAMA WAWILI HILI SWALA UMPELEKE MANGE KWA BLOG YKE NAAMINI WATU WENGI WAMEZOEA KULE KUTOA MAONI SJASEMA HUMU HKN WATU HPN KUNA WATU BT NHC WANAPITA TU C KMA KWA MANGE AU KM WANACOMENT BASI MAMA WAWLI UTAKUWA WABANA COMENTI ZAO NI KWA NIA ZURI TU ATAPATA WAP PAKUANZIA NAWATU WATATOA EXPERIENC ZAO HADI HPO WALIPO WAMEFNYJ BIZNESS LBDA HKU WANAPIGA KAZI JE WALIFANIKIWA AU MAUZA UZA WALIAMBULIA AU ILIKUAJE N KWA NIA NJEMA N KWA UPENDO WA MUNGU NIMEONA HIVYO SMHN SANA KM NITAKUWA NIMEKUKWAZA MAMA WAWILI N MWENYE KUOMBA KUSAIDIWA KULIKO KUKURUPUKA N VZR KUPATA MAONI YA WATU ZAIDI KWA MANGE WENGINE WATAKUTUKANA LKN KM WEWE N MTU MZMA UMEPITIA MENGI SO MATUSI N MAMBO Y KAWAIDA KWA BINADAMU WENGINE UNAWACHUKULIA HIVYO HVYO N STRESS ZAO MANA HKN KITU KIBAYA KMA STRESS ZA HELA SO UNAKUTA MTU HAWEZI VUMILIA SO ANATUKANA OVYO HUMU OR KWA BLOG NYINGNE IKO HVYO KWA BINADAMU TUNATOFAUTIANA KUKUBALIANA NA MATATIZO..

    ReplyDelete
  5. SAMAHN LKN KM NITAKUWA NIMEMKWAZA MUOMBA USHAURI OR MAMA WAWILI N WADAU KWA UJUMLA HYO N MAWAZO YNGU JMN POLEN PIA KWA MAHERUFI MAKUBWA WAPENDWA .

    ReplyDelete
  6. haujaniudh mdau.asante kwa ushauri blog ya mange naifahamu lakini nilionelea niombe ushauri hapa,nilikuwa na maana yangu dear.Ushauri ukiwa mwingi kupita kiasi unaweza kuharibu na unaweza kukupa wakti mgumu kuamua.Acha ikae hapa naamini inasababu yake kwanini haijacommentiwa sana.Unajua ukiwa na imani sana kwa Mungu watu wengine wanaweza kukuona chizi.Lakini hivi ilivo ndivo naamini Mungu ameongoza iwe ivo.Naimekuwa hivi kwasababu.
    Asante mdau, I hope utanielewa .
    mama watatu

    ReplyDelete
  7. nimekuelewa mamii usijali n uko sahihi.

    ReplyDelete
  8. una mawazo mazuri sana anza kujenga nyumba..hyo hela ya kodi uliyokuwa unalipa utaiutumbukiza kwenye biashara baadaye....barikiwa sana na Mungu akutangulie..

    ReplyDelete