Pages

Ads 468x60px

Friday, October 18, 2013

NAFUNGUKA .........



Wandugu kwakweli mwenzenu nimeuona mkono wa Bwana............. ametenda haswaaaa amebadili jina la mbeba mabox kuwa the Boss of her own............. si kwa akili zetu wala uweza wetu bali ni kwa neema yake....... ametuinua na kutufanya kuwa juu katika nchi ya ugenini???? sisi ni nani?????Jina la Bwana libarikiwe................

kiukweli nashindwa hata kujielezea Mungu ni mwaminifu jamani msikate tamaa Mungu hajafunga masikio  ameandaa mkate mezani pako zaidi ya unavyofikiria .............. yeye ni zaidi ya mipango ya mwanadamu!!!!!  
 Mungu katubariki kampuni nyingine inayoitwa.................., nakushughulika na ................... ambayo iko chini ya Mama wawili akiwa ana idadi kadhaa ya wafanyakazi wadhungu  ndani ya nchi iliyojaa urangi (hili siteti hata wao wenyewe huwa wanasema wamevunja record kwa kuangalia urangi) najaribu kukutia moyo wewe uliye nje ya nchi uone ni jinsi gani Bwana anaweza kutenda pasipo kuwa na njia.....................leo hii mama wawili sibebi bali nawabebesha!!!!!!!JINA LA BWANA LIBARIKIWE 
inaweza kuwa kawaida sana kwako ila kwangu mie ni muujiza!!!!!na bila huyu Mungu hili lisingekuwa ............nina kila sababu yakushuhudia matendo yake........

Nnachokumbuka siku moja nilimwambia Baba wawili wangu sasa we mwenzangu your the boss of your own hebu niombee na mwenzako basi na mimi itokee maana haya mabox ya watu ni noumaa!!! tulijichekea tuu kwa akili yakibinadamu nahisi tulihisi ni ngumu hasa ukiangalia mazingira na hivyo kila kitu ndani ya maisha yetu ni neema !!!!!! ila huwa tunajipenda tunapoamua kukomaa kwa ajili ya jambo fulaniki, mpaka nahisi Mungu huwa anakaa halafu anachekaaa na kunihurumia nakuamua kuachilia............. leo najiuliza hivi kumbe yale mazungumzo tulipanda mbegu  na leo tunavuna????!!!!! bado namshangaa sana Mungu.........


ninamengi yakujengana katika hili wandugu ila nipo busy mnoo wiki mbili hizi nataka kuuzoea  uboss kwanza maana hawa wenzetu wafanyakazi nao wakubembeleza  ukitaka wakuingizie hela inabidi uwe mpole maana hawachelewi kukwambia siji kazini na wewe unakazi kibao za watu unatakiwa kuzikabidhi, wamenipata lakini ntajishushaje?????  it doesnt kill me aisee  hata umeneja mmoja wao atapata aiseee hasa ningizikatia mimi jioni ndio nahesabu manoti........



Wateja wangu wa nguo za watoto mnisamehe wandugu website ipo tayari nilikuwa natakiwa leo kuingia darasani ili kujifunza jinsi yakuitumia kama nilivyowaambia nimekuwa bize mbaya zaidi siku za weekend hawafanyi kazi so by next week mtaweza kununua online wandugu. hakuna kulala hiyo  umachinga utapigwa kama kawa...............last weekend nimedrive miles kadhaa nimehesabu $$$$ kadhaa  aisee.......  namshukuru Mungu kwa kweli nimeshaanza kupata support pia kwa ajili ya hili hapo bado  mauzo ya website............ please just support mama Wawili hata kwakumnunulia mtoto wa rafiki yako kwi! kwi! kwi! yaani nayasubiri mauzo yawadau mnoo maana hizo inbox zenu mnanifanya niwe excited  kwa hili pia..................Mbarikiwe mnooo


ZAWADI
atakayepatia ni kampuni gani anapewa zawadi.

2 comments:

  1. Arudishiwe sifa huyu Yesu wetu aliye kufa kwa ajili ya matatizo yetu' ni watu wachache sana wanaorudisha shukran kwa mungu;amin dada Rose kwa hili la kushukuru bwana atakufungulia njia sana.

    ReplyDelete
  2. Ubarikiwe sana,na mungu azidi kuwa na wewe kwakila ufanyacho..

    ReplyDelete