Pages

Ads 468x60px

Wednesday, October 31, 2012

NDOTO NDOTO


Nina kila sababu yakumshukuru Mungu ambaye anazidi kukuza kiwango changu cha imani siku hadi siku, kuamini hakuna kinachoshindikana kwakwe, haijalishi we ninani, una rangi gani, watu wametamka nini juu yako,uko kwenye ardhi ya nani, una umri gani haijalishi, umezungukwa na nani wala na nini haijalishi, kikubwa ni kwamba unaamini nini? na unawekaje ndoto ya maisha yako na kile unachoamini............

Kama mnakumbuka tarehe 26/08/12 nilitoa post ya Safari inaanza, ilikuwa ni tendo la imani ambalo ilikuwa kati yangu na Mungu.....ni siku niliyomwambia Mungu sasa yatosha! yatosha! yatosha! nimeona matendo yako mengi makubwa hili kwangu si dhani km utashindwa na km utashindwa basi itanipa woga mbeleni kwa kuamini  KWAKO HAKUNA KINACHOSHINDIKANA......nilimwambia Mungu huu mwaka usinipite nataka nikuoneeeee

Ndoto iliyonisumbua kwa zaidi ya miaka minne,miaka miwili ya kwanza nilijitia moyo siku ipo, nilifanya juhudi zangu zakibinadam nilijikuta nagonga mwamba, bahati mbaya sana nikajichanganya na jamii ambayo ilinifanya nione haupo uwezekano kabisa,na wengine walinijeruhi nakunicheka kwani walijua ndoto yangu,NIKAJIHAKIKISHIA MWENYEWE kwakuangalia ngozi yangu, hasa katika nchi ya ugeni, na pia niliangalia history za wanadam kwani, niasilimia chache sana ya watu walionje ya nchi kufanikisha ndoto yao ndani ya nchi ya ugeni.......miaka miwili mingine kabla ya tarehe 26/08/12 nilijikuta nimezima kabisa ndoto yangu yaani niliitandikia shuka nzuriiiii nakuilalia hahahahaaaaaaaa............Mtu pekee ambaye hakuchoka, kunitia moyo, hakuacha kuizungumzia ndoto yangu ni Mume wangu mpenzi, Baba wa watoto wangu,Mume aliyetoka kwa Mungu,ambaye aliamini pale nilipo si pangu, kuna wakati aliniona nimeridhika, kila nilipompa wazo la kubadili ndoto hakuniruhusu hata kidogo.....kila alipoingia na kupata nafasi yakuuliza ufumbuzi wa ndoto yangu hakusita na aliporudi nyumbani aliniambia,HONEY (in Slay's Voice) nimeongea na mtu fulani amesema tufanye 1,2,3....... hahahaaaa kuna wakati nilimuhurumia, niliona anahangaika bureeee haitawezekanaaaa.........AHSANTE MUNGU KWA KUNIPA HUYU MUME....
Siku moja kabla ya tarehe hapo juu nilijikuta nipo na positive people ambao waliniuliza maswali meeeengi ni kwa nini nimeizima ndoto yangu??? walinipa mifano mingi sana ikiwa pamoja na mifano yao jinsi walivyoweza fanikisha ndoto zao kwa kweli hawa watu walitumika kikamilifu kusema na mimi,Mungu awabariki sana sana na km mnanisoma wapenzi jueni kwamba yale masaa machache mliozungumza na mimi,Mungu anayakumbuka,mliokoa roho yangu bila nyinyi wenyewe kujijua........niliondoka na ujasiri mkubwa sana....
Tarehe 26/08/12 ni tarehe ambayo nilifanya maamuzi upya nakujichunguza mwenyewe nilifanya yote lakini sikujikubali kwamba pamoja na hatua zote nilizofanya nilisahau ukuu wa Bwana..............
Tarehe 31/10/2012 dakika 10 zilibadilisha kila kitu na kuona ukuu wa Bwana......ndoto yangu ilijibiwaaaaa, ukiniuliza ilikuwaje mi sijui jamani ni kwa neema tuuuuu.... kila kitu ni muujiza kwangu mpaka naandika leo bado nautafakari ukuu wa Bwana..........mwacheni aitwe Bwana na hakunaga km yeye na hatatokea


NILICHOJIFUNZA

1.TAMBUA NDOTO YAKO

2. USIIRUHUSU NDOTO YAKO IKAPOTEA

3.USIRUHUSU NEGATIVE PEOPLE WAKAINGILIA NDOTO YAKO

4.AMINI SIKU IPO YAKUKAMILISHA NDOTO YAKO

ANDIKO LAKUKUTIA NGUVU

Nayaweza yote katika yeye anitiae nguvu, hakuna linaloshindikana kwa Bwana, km bwana akisimama hakuna alie juu yetu,vita tulivyonavyo ni vya Bwana,tutaketishwa nawakuu,hatutakuwa mkia bali vichwa,tutainuliwa kutoka kiwango kimoja kwenda kingine

hahahaaaaa unatamani kujua ndoto yangu???????

4 comments:

  1. Ushuhuda mzuri sana hakuna linaloshindikana kwa Mungu ,umenitia nduvu sana na ushuhuda wako Reylevy

    ReplyDelete
  2. DAAAAAAA HATA MIE UMINIPA NGUVU MPYA MPENDWA....MWANA MKE UMBEA BABU TUAMBIE BC NI NINI?

    ReplyDelete
  3. Amen. mie ndoto naijua. Mungu ni mwema mama wawili. over the moon for you wangu. yaani imebidi nijifunze kucomment leo.

    ReplyDelete
  4. jamani umenitia nguvu sana maana ninavyojipaga moyo halafu sifanikiwi huwa nakata tamaa,sasa umenipa nguvu mpya,tuambie basi kiduchuuuu

    ReplyDelete