Pages

Ads 468x60px

Thursday, December 6, 2012

MAMA WAWILI HAPA NIMECHEMKA

Wadau kati ya hawa bado sijui nani awe mshindi...... ahsante kwa wote  waliojitahidi kutuma kwa kweli nimepata respond nyingi mpaka nimejishangaa.......shukrani kwa wale mlio nje na Tanzania  wengi wenu mlinijibu majibu yangu vizuri sana kwa kweli nimejifunza mengi sana....... lakini, km nilivyosema naomba mshindi atoke Tz ili pesa yetu ikafanye kitu nyumbani kama mbegu ya BEYOU BLOG ikaote na kukua kwa ajili ya utukufu wa Bwana......
Haya sasa ndugu zangu naomba mnisaidie hili just email namba ya mtu ambaye unaona ni mshindi.......kwangu umekuwa mtihani kwa kweli.... naamini hii mbegu imekusudiwa kwa mtu hivyo neema ya Mungu ituongoze kwa hili..........

Angalizo pls km wewe ni mmoja wa haya majibu na hauko Tz plz naomba ni e mail tofauti na hiyo ya mdau anaetamani apate hiyo hela kwa ajili ya mama yake......

1.Kwako Mama Wawili,

Natumai nyie ni wazima familia haijambo.

NINAVYOVIPENDA:

Kwanza kabisa nikupongeze kwakutupa burudani ila zaidi ya yote kuonyesha ya kuwa kuwa mama ni jambo jema na mke mwenyewe busara ila kubwa kuliko yote ni kumtegemea Mungu, ni jambo linalinifurahisha sana mimi na ni sababu kubwa ambayo unifanya nitizame blog yako kila siku....Ya kujifunza humu ni mengi sana hasa upendo wako kwa watoto na mumeo na zaidi familia inayokuwa katika misingi ya dini...huwa nafurahi sana nikiingia kwa blog na kusoma post zako zikiwa zinamtukuza mungu kwa mambo aliyofnaya na anayoendelea kufanya kwenye maisha yako ya kila siku.

Malezi ya watoto ni jambo jema sana hasa ukiwa unawapa kipaumbele kwa mambo ambayo ni muhimu kuzingatia katika shule na maisha ya kila siku kwa sisi ambao watoto wetu ni wadogo kabisa hujifunza vitu kutoka katika post hizo na hujenga mahusiano yetu na watoto wetu zaidi.

Mimi napenda vitu vingi sana humu sitaweza kusema yote ila jambo lingine linalo nifurahisha ni kwamba hujasahu ulikotoka wewe ni mtanzania na ujivuna hivyo na huwa unaeleza vitu ukikumbushia hali yako halisi huku tanzania....na hata jirani zako wameenza kujifunza ukarimu wa huku nyumbani tanzania kutoka kwako nadhani unamkumbuka yule aliyekuletea maua akiwa aamini kwamba umemsamehe kwa ule mkwaruzo wa kwenye gari....ulinifurahisha sana.

Hili litakuwa la mwisho nikupongeze kwa aina ya uvaaji wako...ila niizidi kusisistiza kuwa MAVAZI hayana mahusiano na imani ya mtu mahusiano yake na mungu ukiwa umeokoka haimaanishi uwe mchafu mwili ni hekalu..Hakuna anayetaka kukaa kwenye hekalu chafu hata siku moja basi naamini hivi uwe nadhifu kadri ya Mungu alivyokuwezesha ili kumtukuza Mungu wako ukiwa na furaha na hali uliyonayo.

KISICHONIFURAHISHA:

Kisichonifurahisha ni pale unapowajibu watu ambao hawa kazi ya kufanya wanapokuwekea comments zisizofaa nawe unawapa nafasi ya kuwajibu...Nikukumbshe ya kuwa shetani hupenda kuwaweka na kuwatumia watu kuwarudisha nyuma wale wamtumainiao Bwana Yesu, sasa basi hiyo pia inabidi ufanye jambo juu yake kwakuwa naamin wewe unajua nazungumza nini juu ya Ibilisi na kazi zake usikubali akutumie kabisa.


NIMEIJUAJE:

My cousin send me this link http://beyou-rose.blogspot.com/search?updated-min=2011-01-01T00:00:00-08:00&updated-max=2012-01-01T00:00:00-08:00&max-results=36   wakati tuanchat kwenye yahoo akiniambai kuwa kumbe leo ni bday ya Mke wa Mkwawa i was like ohooo haya ngoja nicheck akaniambai tena you will like the blog i tell you there's a lot to learn kwakuwa hakuna mashauzi ya mjini nikacheka kwakuweka kikatuni kile cha yahoo then nikaenda kuangalia link tukaendela kuchat nikimwambia we mpekuzi sana ulikuwa unatafuta nini huko alinijibu ahhaa sisy hizi blog za mambo ya mjini zimeshamchosha mambo yale yale tu kila siku wanatuwekea fake life hakuna hata tuanchojifunza zaidi ya kutakutufnya tutamani vitu vikubwa kuliko uwezo wetu wakila siku...then toka siku hiyo ika ni habit nilikuwa majamzito karibu kujifingua sina mengi yakufanya so nilikuwa ni internet kuangalia different blog na pia nikapata blog nyingine kupitia ya kwako inaitwa beauty with love...

Na hama kwa hakika ni be you blog hasa kama jina lenyewe.


Kwa keo niishie hapo.
Salamu kwa Wawili na baba wawili, Mungu awalinde daima


Salaam



2.Naipenda Blog ya Be you kwa sababu inaonyesha Maisha ya Mwanamke wa Kitanzania mwenzangu anayeishi Nje ya Nchi yeye na Familia yake , wakiwa na mafanikio Makubwa maana , si lazima mtu akujue sana bali hata picha zinazungumza zenyewe. Najipa moyo na kuamini kuwa kumbe hata sisi tunaweza kufanya Mambo makubwa kwenye Nchi za wenzetu, Napenda Familia yako hasa Watoto wako ( Wawili) Wanaonekana wanapata Malezi Mazuri sana na wanaakili sana pia..Pia ni Familia yenye Hofu ya Mungu ..Kutokana na Mistari yako ya Kumtukuza Mungu wetu Mara kwa Mara...bila kusahau Nyumba yako inamvuto + safiiii..

Niliifahamu hii Blog Kupitia Blog ya Frola yule Dada wa UK ...nilikuwa nafungua fungua tu listi ya Blog zake za pembeni na kukutana na wewe kuanzia hapo sijaacha kuchungulia Blog yako kila siku ..Yaani ni kati ya Blog ambazo lazima nitupie jicho kila siku ...

Nisichopenda kwenye Blog yako ni ngumu sana kutuma Comment I mean Binafsi nikifungua sehemu ya comment mara igande,mara ipande juu yaani inakuwa complicated sana ...

By the way I wish nishinde maana nimebanana na Joto la Dar lol ! hahahahah

Cheers!
3. Dear Rose -Muke Halali ya Slay,

Ahahaha huwa napenda sana hilo neno nikiona umeliandika.

Kwanza kabisa huwa haipiti siku bila mimi kuchungulia humu bloguni kwa sababu wewe unaniinspire sana hasa nikiona watoto wako wawili wazuri na wenye afya. Napenda sana jinsi unavyoishi na jinsi unavyomjua mungu wako huna mashauzi na its real you mana upo kama wewe.

Katika blogu hii ninajifunza mambo mengi hasa tabia yako ya kutopenda makuu, hupendi kujibizana na watu hasa haters badala yake hata wakikuandikia comments za ajabu wewe huwajibu kwa upendo!! kitu hicho kimenivutia na kunifurahisha sana sana mana ungekuwa unajibu kwa hasira ungesababisha ugomvi na baadhi ya blogers wenye kupenda makuu.
Nimejifunza kumtegemea Mungu katika kila jambo na kuwa na ndoto ambazo ninaziwekea malengo ili zitimie siku moja. Huwezi amini dadangu nilipoona dream zako zinatimia nami uliniinspire sana na mimi nitakuja kushuhudia humu humu bloguni kwako aliyonitendea Mungu wetu! Nakupenda sana dada Rose.

Kitu ambacho sikipendi humu ni wewe kukaa muda bila kupost, napenda ujitahidi ku update blog kila siku mana mimi hupita humu kila siku.
Napenda sana uweke picha zako na za watoto wako mana nina wapenda sana na ninatamani na mimi one day nipate watoto wawili wa kike kama wewe ahahahaa.
Mwisho blogu yako niliifahamu kupitia blog ya Jestina George pale kwenye blog list yake kulikuwa na blog yako kailist ndo niliingia kwako kupitia kule so tangu siku hizo sijaacha kuingia humu.

Ni mimi Mdau wako wa Musoma Tanzania


4. Bwana yesu asifiwe mama wawili, naitwa dada amina kutoka dar es salaam tanzania. Naomba kujibu maswali yako kama ifuatavyo..
1)Kutokana na blog yako najifunza kutokukata tamaa na kujiamini nikiwa na yesu, manake mama wawili marazote umekuwa ni mtu unaejiamini.
2)Napenda jinsi unavyoishi yani unaonyesha maisha yako halisi.
3)Kuhusu maboresho, naona ujitahidi kuweka habari mpya, na kuhusu ambacho sipendi nadhani hakuna, sababu naona kila kitu unafanya jinsi roho wa mungu anavyokuongoza..
4)Nimeijua Be you blog kupitia blog ya Ruma africa...

NAMALIZA KWA KUSEMA MUNGU AKUBARI NA AKUPE MAONO
        ZAIDI JUU YA BLOG YAKO...


5). Hellow mama wawili,here i go...
1. Katika blog yetu ya be you ninachojifunza ni kumtegemea Mungu na
kumwamini katika kila jambo,upo karibu sana na Mungu kila kitu chako
unamtanguliya yeye,nimebadilika siku hizi naenda kanisani kila
jpili,umenifanya nijione mpya coz Mungu ndie kila kitu katika
maisha,kiukweli am a new person ilifikia kipindi nilijiuliza wewe una
kila kitu na bado unamtegemea Mungu je mimi nilie na kidogo?endelea
kutukumbusha na Mungu akutie nguvu na kukubariki.
2. Sio kwamba sipendi sana lakini kwa kiasi kikubwa unapenda sana
kupiga picha ukiwa maeneo ya nyumbani,yani mi nadhani itafikia kipindi
watu wataanza kuskip picha zako coz mazingira yatakuwa ni yale yale ya
kila siku,so kwa kuboresha nadhani uwe unapiga picha maeneo tofauti
tofauti blog yetu izidi kuvutia.
3. Kitu ninachokipenda ni vile unavyoemanage blog,napenda kwa sababu
inaweza kutembelewa na watu wa rika zote,hamna matusi,mashindano
yasiyo na msingi,dharau yan i love that kwa kweli,mtu unakuwa huru
hata kupitia blog na mdogo wako au mumeo,ipo kiustarabu and inanifanya
nifeel nipo ninapotakiwa kuwepo sio blog ya ushenzini kutwa wanawaza
kusutana,kuishi maisha fake,kutoleana siri hadharan khaaa..
4. Nimeijua be you blog kupitia kwa rafiki yangu,siku ya kwanza
ananambia kuhusu blog hii alisema winnie huyu dada ni mstarabu sana
hataki ugomvi wala mashauzi mcheck najua utampenda sana,and here i am
full of love for u gel,kip t up gelfrnd (hope i can call u that)

6  
Hongera kwa BE YOU BLOG SPOT kutimiza mwaka mmoja

1.Niliijua Be You Blog kupitia face book wall yako.Ulipokuwa unashare some post from the blog.

2.Nimejifunza nii

- Nimejifunza sana sana kupitia baadhi ya shuhuda zako ambazo umekuwa ukipost eg ushuhuda wa nyumba,gari etc kweli zimekuwa zikinspire na mimi kuendelea kumngangana Mungu kwa vile ambavyo natamani afanye kwenye maisha yangu.

-Napia kupitia post yako uliyopost very recent(ndoto ndoto) ilikuwa very touching serious imenifundisha kuvumilia na  kumgoja bwana.


-Pia nimejifunza kuvaa,the way unavyotupia mitupia sometime inanifundisha my self kupangilia nguo.Kupitia picha zako tu i learn alot.

-Pia nimepinda kitu kimoja kutoka kwako ambacho nitofauti na watu wengi wanaoishi nje....your humble na unawasaidia wengine kuwa humbe and usibadilisha na maisha ya wazungu .
-Umenifundisha kuwa responsible mother in the family like how you are.

Maboresho

-Unaweza kuongeza kuandika zaidi kuhusu post za mitazamo ni nzuri sana and inspiration stories zaidi.Binafsi hii imenisaidia sana but ni vizuri kuongeza zaidi na angalau kila wiki tukapa some insiring msg naamini your good on that sana please usiache.


-Usihangaike sana kuwajibu watu wakiandika vitu ambavyo hupendi kwa sababu huwezi kupendwa na wote katika dunia hii lakini pia ambao hawakupendi wanakusaidia sana kukufanya ufanikiwe so just love them they are  part of your success.


-Unaweza kuongeza part ya mavazi /fashion or jinsi ya kuvaa najua unaweza kusema kitu kwenye hilo eneo na kuwasaidia wengine ili wajue kuvaa.



Otherwise your doing a good job keep it up usiache tuambie na ndoto ili tujifunze kwi kwi kwi kwi kwi TCHAO!!!!!!!!



7.KWANZA NAKUPONGEZA KUKWAKUFIKISHA MWAKA NA BLOG YETU.


1.BE YOU BLOG NIMEIJUA KUPITIA KWENYE BLOG YA JESTINA GEORGE NATANGIA NIMECHUNGULIA HUKU SIKU YA KWANZA MPAKA LEO HAKUNA SIKU NISIYOINGIA HUMU....

2.NILICHOJIFUNZA HUKU KWENYE BE YOU BLOG NI KUTOKATA TAMAA KTK MAISHA NA KUISHI KWA KUMTEGEMEA MUNGU SANA KWA KILA JAMBO KWANI NDICHO KIKUBWA NILICHOKUPENDEA KWANI HAKUNA SIKU USIYEMTAJA MUNGU NA KUMSHUKURU KWA KILA JAMBO LAKO. KINGINE NILICHOKUPENDEA NI HAUISHI KIFEKI FEKI..WALA KWA TAMAA NA UPO VERY HAPPY NA FAMILY YAKO NA KWA UPENDO WA WAHALI YA JUU NA KWA KUMSHIRIKISHA MUNGU KWA KILA JAMBO.

3.NISICHOKIPENDA NI UNAVYOWASUKAGA WATOTO NYWELE NYINGI KM WATU WAZIMA NA KWANZA UNAWACHOSHA NA KUWAKUOMAZA USO. NAKINGINE NISICHOKIPENDA NI KWENYE MAANDIKO YAKO NAJUA C WATU WOTE WATAKAO KUPENDA ILA SIPENDI UKIWA UNAANDIKA HUKU UNAONYESHA KM KUNA WENGINE HAWAKUPENDI MF USINICHUKIE NO SIPENDI BORA UWAPOTEZEE..

4.CHA KUONGEZA NI KUTUWEKEA POST KILA MARA NA KUWEKA MADA ZITAKAZOWAPA WATU MOYO BILA KUKATA TAMAA..



MI NIPO UK KAMA NINA MIEZI SITA SASA BADO SIJAJAALIWA KUPATA KAZI.. NIMEJIBU NIPATE  ZAWADI YA HELA YA KUMUONGEZEA MY MUM KTK MATIBABU YAKE YA MGUU WAKE ALIYOKATWA KWA AJILI YA KANSA.

8 Hellow dada Rose
Mimi najifunza kuishi na watu vizuri na kwa ushirikiano kama wewe, kuwa na muda na kuijali familia yako na kumtanguliza Mungu katika kila jambo.
Sipendi baadhi ya picha zako huwa hazina quality nzuri,jitahidi ziwe na quality nzuri.
Napenda the way you live your life, yaani hau pretend na unawapa watu ukweli inapobidi bila kujali yatakayosemwa.
Niliijua blog yako kupitia kwa dada yangu (ndiye aliyenihabarisha), nilipoitembelea niliipenda so huwa na visit mara kwa mara

9
Habari mama wawili,
Mimi naitwa Benedictor, kitu kinachonivutia katika blog ni:
* Namna unavyompenda Mungu na Kumtegemea yeye haijalishi una mafanikio kiasi gani  unatambua yeye ni Mungu ndo muweza wa kila kitu

Namna unavyolea watoto wako inanipa funza namna ya kulea watoto, na namna unavyompenda mume wako.
Najifunza unaweza kuwa na mafanikio makubwa still ukatimiza majukumu yako kama mama wa familia.
Najifunza kuwa kama mama ni lazima ujifunze kutabiri vitu vizuri kwa watoto wako, daima watamkie vile unavyotaka wawe na watie moyo kila iitwapo leo kwa kuwasifia kwa kila wanachofanya hiyo inawaonggezea kwa watoto kufanya vizuri zaidi na Mungu anawabariki pia.
mfano namna ulivyompongeza mtoto wako kwa certificate aliyopata hiyo inamfanya awe motivated zaidi na aweze kutaman kufanya vzr zaidi.
Kuwa smart na fashionista hata kama umeolewa ni vzr kwenda na wakati na kuwa smart hiyo inaongeza mafanikio zaidi.
Najifunza kama mama ni lazima uwe responsible na familia yako na kutimiza majukumu yako kama mama.

Kitu kinachonikwaza ni pale ninapofungua blog na kukuta hujaupdate kitu chochote.

2 Niliifahamu hii blog kupitia blog ya http:\\rumaafrica.blogspot.com
nilipoiona niliiadd kwenye favorite yangu.

Nkutakia kila lililojema na Mungu akuwezeshu kufikia malengo yako

mama wawili huyo.....

love you all!

10 comments:

  1. kazi kweli kweli mi naona no. 7 akupe comunication za kutuma kwo huko tz..coz anaonekana ameandika kutoka moyoni na kutamani kumsaidia mama yake japo yupo nje

    ReplyDelete
  2. Duhhh huu mtihani ndugu.......Ngoja tuone wengine,No1 kanigusa lakini nikisoma zaidi nakosa jibu......MUNGU azidi kukubariki na kukuongoza...

    ReplyDelete
  3. Number 3 should be a winner

    ReplyDelete
  4. Ungeweka washindi walau wawili Jamani

    ReplyDelete
  5. Kazi ipo hapa,namba 5 had ameanza kwenda kanisani ningependa apewe zawadi ya ushindi

    ReplyDelete
  6. no. 7..mi nadhani haina haja ya kubagua wakati mtu kajieleza kikamilifu hajadnganya km yupo nje..any whay mwenye uwamuzi wa mwisho ni wewe

    ReplyDelete
  7. Namba 3 kanigusa hata mimi nawapenda sana wanao.
    Namba 3 anafaa

    ReplyDelete
  8. Hahahahaaa..! Copy and Paste umemuiga u-turn.!

    ReplyDelete