Pages

Ads 468x60px

Friday, August 30, 2013

A V/S B




KIKUBWA NI KUJITAMBUA, KUJIKUBALI, KUJIAMINI, NA KUWA NA AMANI    KIUKWELI B NIMEMPENDA MNOO angekuwa mtu mwingine angeogopa kulivaa hilo gauni ila kwa sababu yakujikubali utakubaliana na mimi amependeza mnooooo.......mpango sio mwili ni jinsi gani huo mwili unautendea haki..........



A



B
B  nimempenda bureeeeeeee!!!!

Thursday, August 29, 2013

TUZUNGUMZE


Wandugu mnalazimika kumsamehe Mama wawili yaani hii miezi miwili yuko busy mno ...........anahitaji maombi yenu pia, chochote atakacho post au akipitisha siku bila kupost tafadhali mnielewe................. sijafulia lakini (ha! ha! ha!) niko jikoni napika chakula kizuri ambacho sitaki kuwanukisha harufu bali nikiweke mezani tule wote natushukuru kwa pamoja na kumwinua Mungu wetu zaidi na zaidi na zaiiiiidi...............( angalizo linaweza kawaida kwako lakini kwangu ni ushuda!!!)na hata hivyo BADO YEYE NI EBENEZA ALIYEKUWEPO,ALIYEPO NA HATATOKEA MWINGINE ZAIDI YAKE.


Turudi kwenye topic yetu

Mwanadamu anakosea na hakuna aliyemkamilifu bali ni neema ya Mungu inayotuwezesha na kutufanya tuwe watu wa toba kila siku.... na kwa sababu hiyo wengi wetu tumeshindwa kujitambua  nakutupelekea kufanya ndivyo sivyo..................

kuna upepo ambao unapita kwa kipindi fulani ambao unaweza kupewa majina meeengi mabaya mfano,(mchonganishi,muongo,mchawi,malaya, na mambo km hayo) na  ukijichunguza mwenyewe unajijua kweli iliyopo ndani yako......... nazungumza na wale sasa ambao wakijichunguza kwao ni kinyume na lile jina walilopewa na mara nyingine unachogundua kwamba hili jina nimepewa kwa sababu ya kitu fulani ambacho wahusika walilipokea vibaya , au ulishindwa kulifikisha vizuri kwa wahusika au wahusika wenyewe wameamua kuliweka hivyo lilivyo kwani  ni njama halisi iliyopangwa na wanajua wanachokifanya.............mbaya zaidi neno lolote la uongo huwa linavuma mnooo, ndani ya saa moja Tanzania nzima imeshajua. niliwahi kumsoma kaka yangu mmoja facebook alisema hivi ( mara nyingi uongo unavuma km upepo ila ukweli unapanda ngazi taratibu ipo siku utafika kileleni)

ninachotaka kusema ni hichi tumekuwa tunapoteza sana mda ili kuufanya ukweli ueleweke, tumeumiza akili zetu na mara nyingine hata kuwa watumwa wa jambo fulani ili tuu yule aliyekuelewa tofauti ajue kweli, ni kweli katika kila livumalo kuna nafasi yako unayotakiwa utumike, labda kwa kusema kitu kitakachofanya watu waelewe au kuomba msamaha,lakini uwe nakiasi usilazimishe sana  mara nyingine hivyo ndivyo ilivyotakiwa iwe kwa muda fulani kwa ajili ya ushuhuda fulani, kumbuka kuna watu wako kazini na hawako tayari kupoteza ajira zao kwa kuruhusu kweli yako........

nijuavyo mimi nikikukosea nikakuomba msamaha kwa kumaanisha baada ya muda tena lile kosa bado linaendelea kutumika km silaha yakukujeruhi ,nikimaanisha aliyetakiwa kukusamehe alikusamehe kwa sababu alitaka kuonesha watu amekusamehe au kwa sababu ya mazingira fulani iliyompasa kukubali lakini ndani ya nafsi yake bado lipo nalinazidi kuota mizizi......... wanasema chapa lapa au funga vilago vyako na usonge mbele ukajitafutie amani ya roho na kufanya yako...............huo sio muda wako wakuitwa majina mazuri ........ by they way hayo ni majina tuu hayawezi kuondoa ule uhalisi wako kama ukijitambua na kusonga mbele...................LAKINI kama hujajitambua mbona unaweza kuitwa chizi unavyojiongelesha peke yako!!!!!!!!!!

BEYOU!!!!

Tuesday, August 27, 2013

THE LOOK


mama wawili

muke wa Slay
nacheza na camera....

ujumbe wetu wa leo mpango sio una sh. ngapi??? mpango unakitumiaje kile kidogo ulichonacho???????

Friday, August 23, 2013

THE LOOK

Wandugu mwenzenu weekend ndo isha anza............... nina kila sababu zakupumzika kha!!! maana hiyo wiki ilivyokuwa ni Mungu tuu............

muonekano
mama wawili
muke ya Slay
myself

weekend njema wadau wangu........ KIKUBWA NI KUJIKUBALI NA KUAMINI INAWEZEKANA.................

Thursday, August 22, 2013

KITAA



pata muonekano
Muke yake Slay
mama wawili

pray for mama wawili wadau na project yake anayoianza  soooon!!! 

Wednesday, August 21, 2013

SIKU HAZIGANDI


Kweli siku hazigandi my Cristabell kesho anatakiwa kwenda kwenye interview ya kuanza pre school mweeee??? basi leo tangu nilivyokambia sijui hata kanaelewaje haishi kuniuliza maswali na kumtambia Dada yake (Careen am gonna be a big sister like youuuu, cause my mumy is taking me to your school in her voice......ha! ha! ha! kama umsikie vile. wakati huo huo mama wawili najisikaje raha sasa duu wanangu wanatafautiana darasa moja tuu!!! ningejua ningemaliza kabisa nibaki kulea mwee!!!!sasa kwa mpango huu unaweza kuhairisha ukabaki kuwa Mama wawili ha! ha! ha!
vinywele vimefuka lakini naringaje siku hizi kamkono kangu kamenyooka kidogo hapewi mtu hela za kusuka wanangu siku hizi nakomaa mwenyewe

mwaka jana careen alitujia na hii( i wanna come to school because am not kojoa on my Bed.......) baada yakuuliza swali mnaikumbuka?????? tusubiri Cristabell atatujia na ipi.......
AHSANTE MUNGU WANGU KWA KUNIWEZESHA.......

Tuesday, August 20, 2013

NIGHT OUT

pata muonekano
mama wawili (camera imegoma kunitendea haki.............
muke ya Slay
myself.....

Monday, August 19, 2013

CHUKUA AU NIACHIE MWENYEWE


Jiwe linatupwa gizani  hata mimi linawezakunipata kiaina fulani lakini ndo hivyo tunajitambua taratibu na kile tulichokitambua tunajitahidi kushirikisha na ndugu zetu........... Nimegundua sisi wanawake tatizo sio lonya zetu tatizo hatujui  tuzivalie wapi na wakati gani????? tunajikuta nguo ambayo tulitakiwa tuvae Kanisani tunaivaa kitaa,tuliyotakiwa tuvae usiku tunavaa play ground tena na michuchumio mara nyingine  unaweza ukakutana na mtu kituko alichovaa mchana halafu ukakutana naye usiku tena unajiuliza sasa hii si bora angevaa mchana halafu hii usiku.zote ni nzuri lakini wapi na mahali gani zivaliwe ndio majangaz......

Nilichozidi kugundua kutokujua nini kivaliwe wapi na kwa mda gani kumetufanya tubadilishe kabisa zile nafasi tulizonazo  kama zakuitwa Mama, Mke, Dada na zinginezo ........jamii inaweza isituambie na muda mwingine kutusifia kutujaza ujinga lakini kiukweli tunajishushia nafasi tulizo nazo...............

kuna kina sie ambao tumeonja na tamaduni za hawa wenzetu mwee tunafujo balaa yaani tunaiga na visivyoigwa mpaka wenyewe wanatushangaa tulivyowehuka..... hawa wenzetu wanavaa  vikaptula hata kanisa hasa wale wenye umri kati ya miaka 18 kushuka chini, utakuta na sisi na rangi zetu na maumbo yetu hao tumevaa makanisani tena wengine ni wake za watu mwee...... haya basi  tumeamua kuvaa ovyo  kweli ukavae kigauni kifupi kinaangaza na jua hilo play ground????? yawezekana baada ya hapo unatakiwa kwenda sehemu nyingine panapokupelekea uvae hiyo nguo lakini kuna namna fulani tunayoweza kujistyle na bado kote tukaonekana na hatujachafua mazingira...........kila kitu kina umri,mahali na muda wa kuvaa haijalishi kina thamani gani.............

msisistizo nilikuwa na safari tatu bila kurudi nyumbani lakini naamini bado nilirock kila mahala sio saaaaana lakini, bado ilinitunzia kajinaafasi kangu nilikokuwanako bila mimi mwenyewe kujistukia........ hivi unajua kuna nguo tunaweza kuvaa wewe mwenyewe huna amani na mara nyingine utajikuta umeganda kwenye kiti hata mkojo ukubane hunyanyuki unaona aibu kupita kwa watu????? ishawahi kunikuta hii wandugu ni noooumaaa???? sasa sijui ulimvalia mtu, au ulitaka tuu uonekane na wewe umo?? au ndo ulishamuona fulani amevaa basi unataka kumuonesha km na wewe unayo bila kujali nafasi yako, umri, na umbo lako..........
mnisamehe km nimejeruhi hisia za mtu ningenyamaza nisingeitendea haki nafsi yangu.......


 nimepiga picha nyumbani kabla ya safari baada ya picha visivyotakiwa kuvaliwa kwa mda muafaka vilibaki ndani ya gari.........

hapa nikiwa kwenye safari zangu zilizoniruhu kuvaa hivi

na hapa nikwa tayari kuelekea play ground kukutana familia yangu 

na hii kuelekea kupata chochote na familia yangu baada ya siku kuwa ndefu Mama wawili hajaingia jikoni kabisa na huku nikizingatia hali ya hewa ( kajikoti) kamening"arisha kidogo .

Angalizo

kuvaa uchi sio kupendeza wala ujanja wakati mwingine kunaonyesha ulimbukeni nakujishushia hadhi yako.
hili nimelitambua mwenzenu na nimeanza kujistukia hata Baba wawili anisifie nimependeza na jua hii ni love blind tuu mwanamke kuchanganya akili yako na yakupewa..........

mbarikwe wadau

Thursday, August 15, 2013

TUZUNGUMZE

Nilichogundua ni kwamba wanadamu tumeumbiwa nafasi mbili. moja nikujitendea/kujihudumia mwenyewe na ya pili ni kujitendea/kuhudumia mtu mwingine.............cha ajabu ni kwamba wengi wetu tumejikita sana kwenye nafasi ya kwanza ambayo imetupelekea kuwa wabinafsi,na zaidi imetupelekea kutokujua nafasi ya wakati muafaka na jinsi yakukabiliana nayo, na tena imetufanya tuwe wanyonge,watu wakunung'unika,laumiana sisi kwa sisi  na vitu km hivyo.tumetekwa na hii nafasi kiasi kwamba 24/7 tunataka kuwa sisi na kujihurumia kuliko pita kiasi............ 

Tumesahau kwamba kuna nafasi ya pili ambayo inatupasa kuipitia ili fulani apone,ili fulani ainuliwe,ili kusudi ukiokee kinyonge na kukipa furaha,ili kusudi  kupitia wewe jamii ipate tumaini na ndio maana tumekuwa tukiwakumbuka wengi nakuwaita mashujaa.... tukimaanisha walipata neema yakujitoa kwa namna fulani kwa ajili ya wengine kwa maana nyingine hawa watu waliitambua hii nafasi ya pili nakujua nafasi yao nakuitumia kwa ujasiri........ nikisoma maaandiko matakatifu na muangalia Musa , nanukuu kutoka3:11("MIMI NI NANI HATA NIENDE KWA FARAO NIKAWATOE WANA WAISRAELI WATOKE MISRI?)

kwa jicho la Mama wawili, nahisi Musa hakutambua nafasi yake,yawezekana aliangalia ukubwa wa jambo lilivyo,au yawezekana alijihurumia hasa akimwangalia Farao na mamlaka yake,au hakujiamini kabisa  ("TAZAMA HAWATANIAMINI WALA HAWATANISIKIA SAUTI YANGU") mpaka pale alipokubali na kuonyeshwa baadhi ya uweza uliopo ndani yake.
Hivi ndivyo tulivyo wanadamu waleo tumekuwa ni watu wakujihurumia kupita kiasi, tumeshindwa kutatua matatizo ( face challenges) kwa sababu ya ubinafsi cha ajabu tunajikuta kila siku tunaangukia kwenye hilo tatizo na halipati utatuzi  kuna msemo unasema TATIZO HALIKIMBIWA ILA LINATAFUTIWA SULUHISHO. kama mimi mama wawili kuna kipindi niliangaika mno juu ya hili nilidhani njia pekee ni kuwa mbali na jamii au vitu hivyo vilivyonisababishia tatizo,na kukimbia kabisa cha ajabu Mungu alinipa mapumziko ya mda tuu na kunirudisha kwa kasi na kujikuta  nimerudi nakufungiwa na mageti ikimaanisha hakuna kutoka mpaka KIELEWEKE ha! ha! ha! ila kikubwa baada yakujitambua amenipa amani ya hali ya juu kiasi kwamba ninaweza kuwajibika bila wogo, kujistukia, ujasiri wa ajabu yale maumivu niliyokuwa nayaona yamegeuka kuwa kicheko na mda mwingine yamenigeuza kuona huruma kwa muhusika hasa anapoona anafanya kwakunidhuru  au kunikomesha au kwa namna yoyote inayofanania.........NYIE ACHENI MUNGU AITWE MUNGU BWANA............wasomaji  wa Biblia mtanielewa na hasa tukimwangalia Yona alivyogoma bora afe kuliko kuendelea na wito aliyoitiwa.

Namwangalia Daudi pia alivyotambua muda na nafsi aliyonayo hasa pale mtoto wake alipomgeukia kutafuta roho yake akiwa katika harakati zakumkimbia mwanawe alitokea mtu wa kabila la Sauli aliyeitwa Shimei, kasome samweli wa pili 16:5......... nilichojifunza Daudi aliujua wakati alionao , angeweza kumfanyia chochote ila aliruhusu kulaaniwa, kutukanwa, na kuaibishwa. 

Kikubwa  hapa ninachotaka kusema matatizo yapo ( challenges) na yapo kwa sababu fulani  kikubwa ni kutambua nakujua nafasi yako juu ya hili. 


Namalizia kwa kumwangalia YESU mwenyewe aliposoma chuo cha nabii Isaya LUKA 4:18  .tukumbuke alikuja kama mwanadamu alipata maumivu km mimi na wewe alijua vita atakayoikabili,upinzani juu ya hayo aliyoyasema lakini kikubwa alijitambua na mamlaka iliyopo ndani yake.

HILI NI JICHO LA MAMA WAWILI

Wednesday, August 14, 2013

I AM HUMBLED!!!! (SIKUSTAHILI)

Hivi karibuni nimekuwa  hivi, kila kitu kinachotokea ndani ya maisha yangu lazima nikipe mda wa kutafakari na kujiuliza kwa nini kimetokea,nakujitathimini mwenyewe ni njia ipi inipasayo kukikabili??? na mshangaa Mungu mnooo!!!! moja ya vitu hivyo ni hili.......

last weekend kama jumuiya ya watanzania tuliopo eneo hili tulikutana kwa ajili yakuchagua viongozi, mkutano huo ulifanyika nyumbani kwa Mama na Baba wawili. kama muonavyo hapo chini niko kimama zaidi...... bila mategemeo wala kuhisi  jina langu likatajwa kati ya list ya kugombea umwenyekiti bila kupoteza mda nilijitetea kwa kutokujiamini,km hiyo nafasi hainistahili naamini kabisa yawezekana mda wa kura ungefika bila kujitetea nisinge shinda simnajua kura za makaratasi huwa haziongopi????ha! ha!ha! cha ajabu nafasi yakatibu likatajwa tena nakusisitizwa ni marufuku mtu kukataa, nilijitia moyo kwani majina yaliyokuwa kwenye list niliamini kabisa sio rahisi mimi kushinda lakini nilimshangaa Mungu kushinda nafasi hiyo.................Baada ya hapo nikaanza kutafakari,nakutathimini zaidi kumuuliza Mungu imekuwaje....................TUTAZUNGUMZA NI NINI NILICHOJIFUNZA KUPITIA HILI...............

WAJUMBE
MAMA WAWILI AKIWA HAJIAMINI ANAVYOKABIDHIWA MAJUKUMU

Tuesday, August 13, 2013

WAWILI'S TIME

Safari yetu ndio hiyo imeanza leo tumeamua kujipigisha picha nje ya  nyumba  na wanangu sasa ukiwatoa nje wanavyokuwa  na fujo  na sifa za Mama yao mbona Camera iliwapata........
my wawili.......sina lakuongea ila JINA LA BWANA LIBARIKIWE!!!!


SI KWA UWEZA WALA AKILI ZANGU
SIKUSTAHILI LAKINI ULINIPENDA, UKANIKUMBATIA NA KUNITETEA......
aiseeeee!!!! ACHENI MUNGU AITWE MUNGU.......

dada utamjua tuu
na mdogo mtu kudekaje sasa????
wanaitwa Careen na mdogo wake Cristabell a.k.a Wawili
tunakoenda tunakujua wenyewe... leo hatuna car seat aisee na mawazo police wakinikamata nitawajibika haswa bila kumlaumu mtu maana nimeamua kuvunja sheria kwa hiari.......
wenyewe wamefurahi leo no car seat....... kweli mtoto ni mtoto mwee....


Friday, August 9, 2013

USINIGUSE

Mpango mzima wa leo ni dont touch na mwendo wakunyata nyata ha! ha! ha! na hivyo wadhungu wanavyojua hug zakipendwa pendwa bila shaka sitarudi na madoa  uzuri wao hawajuagi kujibwiliga make up kama kina siye ha! ha! ha! hilo nalo nimelizingatia............... nimekaa mkao wakupokea wapendwa naelelekea kwenye mkutano wa wanawake nikazidi kujazwa na kujifunza wanawake wa imani walifanyaje,wanafanyaje.....
mama wawili
muke ya Slay
dare to be yourself wandugu.......
msijari ntawaletea desa kwenye topic zetu za tuzungumze........

Thursday, August 8, 2013

KITAA


Mafuta yakupikia kweli ya dumu japo kuwa unaweza nukia fish & chips all the time mmmh!!!! hivi????huu unywele wangu au nimeaazimwa maana nauchezea tuu..... leo nibane hivi mara kesho kaua mara.............
toto la kibena,kinga & hehe  mrembojeee??? japo kuwa sura yakikazi zaidi kwi! kwi! kwi!
kujikubali, kujiamini kuthubutu mpaka kieleweke ndo spirit!!!!!

Mama wawili

muke ya Slay
BWANA NDIE MCHUNGAJI WANGU NI MWOGOPE NANI???????

Wednesday, August 7, 2013

IT IS POSSIBLE

 nikutie Moyo....... angalia kwa Makini halafu mtukuze Mungu kwa vile ulivyo. AMINI NA SIMAMA KWA UJASIRI..... UBARIKIWE

Tuesday, August 6, 2013

WAWILI.....


baada ya siku yangu kuwa ndefu mnooo........ kutana na wawili na swaga zao
wanapenda camera km Mama yao
malaika wangu
am blessed
hii ndio sababu yakuitwa Mama wawili