Pages

Ads 468x60px

Wednesday, July 31, 2013

NEWLY WEDDING

Jamani hii ndio habari ya mujini Dar es salaam na London....... kwa wale mnaowajua na hamjabahatika kuthibitisha hili huu ndo mpango mzima, imehalalishwa wiki kadhaa zilizopita.

Bi Amina  muke halali ya Mnukwa a.k.a Muke ya rafiki ya Mume wangu  karibu sana mamii hawa watu hutojuta hata kidogo......we  omba Mungu akupatie hekima yakuitumia nafasi yako km mke uone utakavyopetiwa petiwa ha! ha!ha!
Mr &Mrs

gorgeous!!!

Tuesday, July 30, 2013

ONJA


Nasikitika tu viatu vya mama wawili havina mrithi hapa maana hiyo miguu ya wawili duu!!!
yaaaaammmmmm!!!
nimekuza mwenzenu hata siamini.....
yaliyojiri

Monday, July 29, 2013

BABA NA WAWILI


LA MOYONI.... kiukweli moja ya vitu ambavyo Baba wawili huwa anavifanya na kujiona nimebarikiwa  kama Mama/mke ni hichi wapendwa kutenga muda wa kuwa na wanawe  yaani yeye tu na wawili  aisee huwa nafarijika mnoo.....kama Mama au mke utanielewa hapa.....ndani ya wiki lazima iwe siku yao  kwa mda fulani cha ajabu sijawahi mwambia mwee sijui namuonea aibu au ndo vile kuchukulia kawaida kumbe kumoyo unamshukuru Mungu mnoo ha! ha!ha! simnajua mda mwingine akikukodolea macho huwezi kuunganisha maneno????kigugumizi.....Baba watoto ukinisoma kwa kweli unanibariki sana sana sana najivunia kuitwa Mama watoto wako..... hii ndio sababu niliwang'ang'ania  nije na nyie  bila kuvuruga utaratibu wenu ili niwapige picha nimshukuru Mungu kwenye kadamnasi km hivi.


the team
niko nyuma nyuma leo hata sauti za Mama sizisikii niko kikazi zaidi......

nilijisahau hapa nikapiga kelele Ba Careen mtoto anaanguka huyo!!!! 
wanafanya yao
wawili
mmmh!!!
happy them

hapo sasa
nikiripoti kutoka eneo la tukio ni mimi.......

Friday, July 26, 2013

TUZUNGUMZE


Ninacho amini kila mwanadamu aliwahi/anayo/ amesha kuwa na maono juu ya jambo fulani linalomuhusu, nalo hili mara nyingi huwa linabeba uhalisia wa mtu husika .....lakini kwa sababu ya msongamaono wa maisha yaliyotuzunguka na kushindwa kujitambua, wengi wetu tumepoteza uhalisia nakubaki kuwa chombo kisicho namuelekeo..............

ni vigumu sana kutimiza malengo kama tutauzika uhalisia na kuwa vile mwanadam anataka uwe,kuiga au kutamani kusiko na kiasi hadi kupelekea kupoteza muelekeo wa uhalisia wako,mwanadam ni mwanadam lakini tumeletwa kwa uhalisia tofauti. kwa mfano:

  (Mwanzo 37 nakuendelea) nimejifunza mengi. namuangalia Yusufu alikuwa ni kipenzi cha Baba lakini ndugu zake walimchukia kwa kile ninachoamini uhalisia wake nanukuu ("Yusufu akamletea Baba yao habari zao mbaya basi Israeli akampenda Yusufu kuliko wanawe wote") pamoja na kwamba hakupendwa bado Yusufu mazingira hayakumbadilisha alibaki kuwa Yusufu,ukiendelea  tena tunamsoma Yusufu alivyoota ndota Yeye km Yusufu hakujua km alichoota kina uhalisia alivyosimulia ndugu zake walitambua uhalisia uliopo katika ndoto, chuki iliongezeka na kuzidi kujipalia kaa la moto........kwa wale watu wamaono hapa tutaelewana vizuri, kuna wakati unaweza ona kitu usikipe uzito,au ukaona hakiwezekani na kukipuuzia na tena iwe imetukuta hata tumekosa hekima yakulisimlia kwa jamii, mara nyingi  imetupelekea kuwa adui nakuitwa majina fulani fulani.........na mara nyingi unapoona huwa huoni njia mbadala zitakazotumika...... hivi ndivyo nnavyomtazama Yusufu kwa maana nyingine ni hii.........Aliota? ndiyo, akasimlia? ndio, cha msingi kakaa kwenye mstari (uhalisia)

naendelea zaidi kumsoma, ameota ndoto nyingine ambayo hata kipenzi chake Baba yake ilimuumiza masikio nakumkanya..... hii inaniambia uhalisia wa mtu uko ndani ya mtu, na mtu mwenyewe ndio anaweza kujibadilisha....... nnachokuja kuona ni mbinu za kutaka kumuua ambapo pia ilishindikana mmoja wa adui akageuka kuwa daraja lakumpitisha Yusufu katika safari yake(wow! nzuri hiyo) na badala yake mwingine akashauri tena auzwe wakijua wanamkomesha kumbe wanamsindikiza Yusufu kwenda kujitwalia utukufu wake...............kajisomee mwenyewe utanielewa mpendwa

NAJIULIZA??????
 hivi Yusufu asinge simulia ndoto zake kwa hofu ya wanadamu ndoto zake zingetimia (Yes! inawezekana Mungu hakosi njia,lakini ninachokiona  uhalisia wake uligeuka kuwa chuki na chuki ndio iliyotumika kuwa daraja la yeye kupitia) na hili ndilo lililopo katika dunia ya leo mara nyingi chuki inajengeka kwa sababu ya uhalisia wa mtu( kile kituu cha kipekee ulichonacho ambacho waliojenga chuki hawana na km muhusika ukisimama kwenye mstari na hekima chuki ya huwa ndio mlango wako wakutokea  wengi tunaushahidi wa hili.........na habari njema ni kwamba HAKUNA MWANADAMU AWAYE YOYOTE MWENYE UWEZO WAKUKUTOA KWENYE MSTARI zaidi ya fujo fujo tu zakukuchelewesha na kukutengenezea mazingira mazuri zaidi........

na mwisho naiona aibu ya ndugu zake walipoenda kumuinamia km ndoto ilivyosimliwa aiseeeeee!!!!!!

KAA KWENYE MSTARI,TUNZA UHALISIA WAKO,BE YOURSELF)

ANGALIZO

hekima na uhalisia viende pamoja, uhalisia pekee muda mwingine unaweza ukafanya usumbufu mwingi kwenye safari yako ambao unaweza ukajikuta unakata tamaa na mambo yafananayo........

weekend njema

Wednesday, July 24, 2013

HABARI YA MUJINI

NI WALE WALE SILVER BOUTIQUE WAMEKULETEA MZIGO MPYAAA............ PIGA 0713608383 KWA MAWASILIANO ZAIDI














NIMEKUTANA NAYO.....

 Nilitaka kuzungumza kabla sijaanza nikakutana nayo ha! ha! ha! nimechekaje mpaka nimeishiwa nguvu zakuzungumza.............. hawa ndio wanadamu.....


Tuesday, July 23, 2013

THE LOOK


MUKE YA SLAY
haya sasa lile pozi letu la kupishanisha miguu nimelishinda....... khaaa!!!!
kununa sasa ha! ha! ha! i love my self kwa kweli!!!!
myself

Monday, July 22, 2013

Friday, July 19, 2013

LA FAMILY 2


LIHIMIDIWE JINA LIPITAYO MAJINA YOTE, LILILONIFANYA LEO KUWA SHUHUDA WA MATENDO MAKUU ANAYOYAFANYA, AMBAYO HAPO KALE SIKUWAHI KUAMINI YAPO KATIKA HALI YA UHALISIA. NA HATA KAMA NILIJUWA YAPO KWENYE UHALISIA BADO NILIONA KUWA NI NDOTO KWANGU ISIYOWEZA KUTIMILIKA, KWANI SIKUONA MLANGO WALA NYUFA........... NA SASA AMENIFANYA  KUWA SHUHUDA, NIMEONA,NIMEGUSA,NIMETENDA NA BADO NAENDELEA KUZINGOJA FADHILI ZAKE ........................INAWEZEKANA!!!!!!

WAWILI
BABA NA MWANAE




GIRLS
mtu na dada yake
another view
happy us

muke ya Slay
mama wawili
INAWEZEKANA............