Pages

Ads 468x60px

Tuesday, March 31, 2015

MAMA WAWILI........

Ha!ha!ha! nyie Bwana mi mzimaa kabisa yaani hata siumwi....... Lile Gauni hata mimi nilikuwa najicheka kitambaa cha ndani  kilikuwa unahitaji kukitengeneza kila pozi sasa kungine nilikuwa nasahau  ha!ha!ha!
 Kesi sitaki mjue......... ila vinyama vimeongezeka mpaka nimejishangaa......ila nilichogundua kwa wale mnaotaka vinyama nyama aisee do not pay attention to your body we vuruga tuu ha!ha!ha! nimesema sijipimi ng'o mpaka nione sasa inatosha ndo nijue nimevunja record kwa kiwango gani................ otherwise nikianza kujipima pima ntarudi kule kule kwenye kupay attention ndo ntavuruga kabisaaa.........




 Umeamini eeh!! hamna kitu humo....................maana wengine umeanza kunitumia mibaraka  mweee isije ikawa lisemalo linakuja uuwiiii!!!  jamani km liko njiani basi tusubiri mpaka haka kabinti hapa chini kawe kwenye umri fulani wakumbeba mtarajiwa............ kwa sasa ndugu zangu mmmh!!! 

Jamani nyie acheni kaendelee kuwa katoto kanyumba  ha!ha!ha!

Nawapenda

Monday, March 30, 2015

TUZUNGUMZE..........

Ndugu zangu, mwenzenu niliachia tuu hii  nilisoma juu juu nilijua itakutana na makamanda huku najipa muda na mimi wakuikalia........ mbarikiwe mnooo wapenzi najuvunia aisee nina  makamanda huu ndani hatariiiii!!!!pia najifunza kitu na mimi kutoka kwenu Mbarikiwe mnoooo............ Naomba na mimi niongezee kidogo mawili matatu 

nimeicopy ili kwa wale ambao hawakuisoma wajue tunazungumzia nini....

Habari rose. Natumaini uko salama na familia yako. Mimi ni mmojawapo wa watu wanaovutiwa sana na blog hii. Kwa kweli nimejifunza vingi. Naomba ikiwezekana hii comment yangu iweke kama topic kabisa ili nipate msaada. 1.Nimekua nikiandamwa na roho ya kudharauliwa na kukataliwa kwa muda mrefu. Mwanzoni nilikua sitilii maanani lakini baadae nikaona kuna tatizo. Mimi ni mama wa watoto wawili nipo tanzania. Nilipomaliza chuo nilipata kazi nzuri kwenye kampuni moja kubwa. Toka nifike pale supervisor wangu akawa anafanya mpango nipelekwe section nyingine lakini ikawa inashindikana. Akawa ananifanya nionekane siwezi kazi, ananipangia kazi ambazo si zangu, hanielekezi kazi, kila mara ananipa kazi za kuniweka kwenye mtego. Baadae niliondoka kwenye hiyo kampuni baada ya kutokea fraud and my name came up, but I swear I didnt have anything to do with it na hiyo ilikua plan ya yule supervisor. Wakwe zangu na wifi ni mojawapo ya watu niliyowajali kipindi nina kazi lakini ni wasengenyaji sijapata kuona. Yaani nikisaidia mimi wanajua ni pesa ya ndugu yao. Nikija na plan nzuri ya biashara wanajua ni ndugu yao, yaani naumia mno. Hata nikichangia mchango wa mawazo ambao ni bora hakuna atakaeutilia maanani ni mpaka madhara yaje yatokee baadae. Yaani hata nikiongea kuchangia kitu hua naonekana kama najisaidia.wakija kwangu ni kukosoa kila kilichopo kwangu, hua siwezi kuongea chochote kwakua mimi hua ni mkimya labda na muoga. Yaani hakuna anayetaka kua karibu na mimi, najiangalia sioni labda nina tatizo, lakini hua nasalimia watu, mtu akiwa na shida nitajaribu kutatatua shida yake. Lakini kwa mara, ara ya kwanza katika maisha yangu nilishangaa inakuwaje uwe unamuwazia mtu mema alafu ghafla unakuja kujua nature yake halisi. Jamani wadau nisaidieni, maana naona kama naanza kubadilika na kua tofauti. Labda ni vile sina kazi now ila roho ya hasira na chuki naona inaninyemelea, hua saanyingine nalia sana. Nimekua na uchungu mwingi sana moyoni. Nisaidieni kwa maombi najua hapa kuna wanawake majemedari wa maombi, rose najua nawe ni muombaji niwekeni kwenye maombi, msinisahau kwenye vikundi vyenu vya maombi. I promise nitakuja kutoa ushuhuda hapa.



  Wadau nafikiri wametumika sawa sawa kikubwa ni maombi hiyo ndio silaha yetu. Tukiwa kwenye maombi pia kuna vitu tunahitaji hekima kuvitambua, au kujua nafasi yako katika hilo huku likiwa ndani ya maombi.

Nimeelewa hasa kwenye mazingira ya kazi ofisini mara nyingi huwa kuna mipaka. Kuna vitu vingi huwa vinachangia kwenye mazingira ya kazi hivyo mara nyingi huwa ni hekima kuingia kiroho zaidi.........na Wakati mwingine panahitaji watu km wakina Esta na Modekae Esta 2:19-23) ili kutatua tatizo.........Vinginevyo nikukazana maombi kabla hujaingia ofisini.......... ikiwezekana muweke muhusika mbele za Mungu kabla hata hujakutana naye...(Mnajua vyenyewe tunafanyaga wapendwa wangu, ila ujue nini usilaani) 

Mtume Paulo anasema,

2wakorinto 10:2 Nawaomba nitakapokuja kwenu nisiwe na ujasiri dhidi ya watu fulani kama ninavyotazamia kwa wale wanaodhani kwamba tunaishi kwa kufuata namna ya ulimwengu huu. 3Ingawa tunaishi duniani lakini hatupigani vita kama ulimwengu ufanyavyo. 4Silaha za vita vyetu si za mwili, Bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome. 

Sasa basi naingalia hii roho tena naona kama inanizoea sana ujue??? maana imekuja mpaka nyumbani kwangu wapenzi unavyosema nyumbani kwangu shetani anatakiwa atambue uko kwenye himaya yako yaani mi nipange kochi langu kulia for no reason we uje unipangie kushoto eti kwa sababu wewe sijui nani yake nani aiseeee!!......... kama zilivyo taratibu zakule kazini  ambazo tumeona kabisa km sio Esta na Modekae ambao ni watu  sahihi wamewekwa ili watumike,  basi ndivyo ilivyo kwenye himaya yangu.........

Hapa wapendwa wengi huwa tunachanganya na shetani anatumia sana sana sana sanaaaaaaaa............. kuna vitu vingi huwa vinazaliwa hapa aisee usipokuwa makini. Ninachosikitika pia km ndo hiyo roho imetumika kwa mda mrefu bila kukemewa huwa inaleta shida sana kuibadilisha........................Wengi wetu tunalia sana kwenye ndoa zetu na mara nyingine tunaona km Mungu hatusikii kumbe ni namna tuu ambayo unaiandaa akili yako jinsi yakukabiliana na jambo. na mara nyingine haipo hivyo unavyofikiri inakuhitaji wewe ufanye kitu.....................

 Ngoja nikupe mfano  ambao nahisi Pia nilikuwa naandaliwa kuja kuuleta hapa (labda ni mawazo yangu tuuu)

 Juzi niliota niko na Dada mmoja hivi namjua ambaye ni mjane. tulikuwa tuna have fun nakusaidia sana, sikumbuki tulisaidiana nini ila kuna kitu nilikuwanamfanyia kwa moyo wote, Sasa tukiwa tunaendelea kuna kitu alikifanya gafla ambacho mimi ndotoni nilihisi hakina upako, sikumpotezea aisee, hapo hapo nilimpa ukweli wake, kiasi kwamba ikaonekana yale yote mazuri sasa tuliyofanyiana yamekuwa zero............ kitu ambacho kikanipelekea hata mimi kuumia moyoni, nakujiuliza kwa nini ameshindwa kunielewa??? yale yote niliyomfanyia yalikuwa kwa moyo wote isipokuwa pale kwenye uovu ilinibidi niseme......... Gafla nikastua usingizini mara nyingi nikiona hivi huwa nakimbilia kwenye biblia  fasta ha!ha!ha!ha! Guess what??? nilikutana na hili neno

Warumi12: 9 Upendo lazima usiwe wa unafiki. Chukieni lililo ovu, shikamaneni na lililo jema.
Aisee nilipata nguvu hapo kwa maana nyingine nilitambua alienifanya niumie rohoni usingizini ni shetani, kutaka kunifanya nijione yote niliyoyafanya ni zero kumbe nilifanya kwa sababu ya upendo au ndivyo nilivyotakiwa kutumika  bila kucompromise.  kwa maana nyingine tusifunike ovu kwa sababu labda ni mjane, masikini, wifi ,mkwe................................ kwanza dhambi ujue???Ha!ha!ha! sikwambii ulete  timbwili humo ndani No!no!no! hiyo si hekima na wala sikwambii Mimi nafanyaje , mpendwa nyumba zinatofautiana  kikubwa ujue himaya ni yako kwa namna yoyote ile iliyo nzuri, himaya yake inatakiwa ikupe amani ili uweze kuitumikia vizuri......................... Kama wanakusengenye wakiwa huko shida ni nini eti mpendwa wangu??? Binadamu hana jema....... neno la Mungu linasema kila ufanyalo fanya kama unafanya kwa Mungu, usipoteze muda kusubiri shukrani za wanadamu japo kiukweli kuna Muda tunahitaji kutiwa moyo, lakini hilo lisitupelekee tukajikuta tunavaa mabomu ndani ya mioyo yetu kama ujisemeavyo mwenyewe hasira,chuki inakunyemelea....... Nikwambie kitu sometimes huhitaji wewe direct kutoa huo msaada km unajikuta una huo mzigo, unatamani kusaidia  mpe huyo  ambaye wanaona anafanya, sasa yeye ndio atajua anavyopeleka atawaambiaje,kikubwa  ukweli  atabaki nao yeye halafu unajua nini huyo ndo ze big boss........  na hata kesho na kesho kutwa chochote kikitokea, huhitaji kwenda mbele za Mungu kulia lia ukweli ujulikane maana Ze boss ana ukweli  badala yake unaingia mbele za Mungu kwa moyo wa shukrani jinsi anavyokutetea mbele ya watesi wako..........

Hizo Hasira ,chuki, naona shetani alikuwa anakuandaa mpenzi na anataka kukuwin ushindwe kufocus, mbaya zaidi kipindi ambacho unahitaji akili itulie ili uweze kufocus na mambo yako ya kazi ndo yamekuwa yamekutinga............. Nikwambie kitu pia acha kuhusianisha kila unachokikabili mbele yako kina uhusiano na hiyo roho yakukataliwa hizo ni mbinu za muovu.... ni dhahili anataka akuvishe hilo vazi na wewe uridhike nalo . kila ukiamka asubuhi Mwambie wewe ni mwana wa Mungu kila uwekapo nyao zako patabarikiwa, Tangaza roho ya ushindi, ni kweli patakuwa na ushindani na mvutano......... unajua nini????? mwisho wasiku We ni Mwana wa mfalme!!!!!
Malizia hiyo mistari hapo chini na Mungu akusaidie hekima jinsi yakuitumia kwenye uhalisia

Angalizo huo mstari wa 16 kumbuka alikuwa anasema na watu wajamii moja yaani wanaoongea lugha moja kwa namna nyingine anasema na wapendwa sasa tusije tukachanga ukataka kutafuta amani na pepo halafu sometimes yanakujaga na sura ya kipendwa usipokuwa kiroho imekula kwako ha!ha!ha!ha! (from experience you know)



 10Pendaneni ninyi kwa ninyi kwa upendo wa kidugu. Waheshimuni na kuwatanguliza wengine. 11Msiwe wavivu, bali mwe na bidii katika roho mkimtumikia Bwana.12Iweni na furaha katika tumaini, katika dhiki iweni na saburi, dumuni katika maombi. 13Changieni katika mahitaji ya watakatifu, wakaribisheni wageni. 14Wabarikini wale wanaowatesa, barikini wala msilaani. 15Furahini pamoja na wenye kufurahi, lieni pamoja na wale waliao. 16Kaeni kwa amani ninyi kwa ninyi. Msijivune, bali mwe tayari kushirikiana na wanyonge. Wala msiwe watu wenye kujivuna kwamba mnajua kila kitu. 17Msimlipe mtu ye yote ovu kwa ovu. Jitahidini ili mtende yaliyo mema machoni pa watu wote. 

Nawapenda


Friday, March 27, 2015

THE LOOK.........................


Huyu nani eti????


ha!ha!ha! kuna kitu nimejicheka hapa guess what?? nikupe zawadi ki!ki!ki!

Kajiuso thatha ee bwana ukiona unashinda juani kila siku kwenye mabox na bado ukirudi makeup inafunika funika  ujue hiyo makeups ni???????

Kibokoooooooo.............Nyie bwana hii makeup mkombozi bwana sifa acha tuzitoe




The face she makes  akiwa bado anatafakari nakusubiri hekima imuongoze.........

love you

Wednesday, March 25, 2015

SEMA TUPONE..........................

Sema neno wandugu mwenzetu apone...

Habari rose. Natumaini uko salama na familia yako. Mimi ni mmojawapo wa watu wanaovutiwa sana na blog hii. Kwa kweli nimejifunza vingi. Naomba ikiwezekana hii comment yangu iweke kama topic kabisa ili nipate msaada. Nimekua nikiandamwa na roho ya kudharauliwa na kukataliwa kwa muda mrefu. Mwanzoni nilikua sitilii maanani lakini baadae nikaona kuna tatizo. Mimi ni mama wa watoto wawili nipo tanzania. Nilipomaliza chuo nilipata kazi nzuri kwenye kampuni moja kubwa. Toka nifike pale supervisor wangu akawa anafanya mpango nipelekwe section nyingine lakini ikawa inashindikana. Akawa ananifanya nionekane siwezi kazi, ananipangia kazi ambazo si zangu, hanielekezi kazi, kila mara ananipa kazi za kuniweka kwenye mtego. Baadae niliondoka kwenye hiyo kampuni baada ya kutokea fraud and my name came up, but I swear I didnt have anything to do with it na hiyo ilikua plan ya yule supervisor. Wakwe zangu na wifi ni mojawapo ya watu niliyowajali kipindi nina kazi lakini ni wasengenyaji sijapata kuona. Yaani nikisaidia mimi wanajua ni pesa ya ndugu yao. Nikija na plan nzuri ya biashara wanajua ni ndugu yao, yaani naumia mno. Hata nikichangia mchango wa mawazo ambao ni bora hakuna atakaeutilia maanani ni mpaka madhara yaje yatokee baadae. Yaani hata nikiongea kuchangia kitu hua naonekana kama najisaidia.wakija kwangu ni kukosoa kila kilichopo kwangu, hua siwezi kuongea chochote kwakua mimi hua ni mkimya labda na muoga. Yaani hakuna anayetaka kua karibu na mimi, najiangalia sioni labda nina tatizo, lakini hua nasalimia watu, mtu akiwa na shida nitajaribu kutatatua shida yake. Lakini kwa mara, ara ya kwanza katika maisha yangu nilishangaa inakuwaje uwe unamuwazia mtu mema alafu ghafla unakuja kujua nature yake halisi. Jamani wadau nisaidieni, maana naona kama naanza kubadilika na kua tofauti. Labda ni vile sina kazi now ila roho ya hasira na chuki naona inaninyemelea, hua saanyingine nalia sana. Nimekua na uchungu mwingi sana moyoni. Nisaidieni kwa maombi najua hapa kuna wanawake majemedari wa maombi, rose najua nawe ni muombaji niwekeni kwenye maombi, msinisahau kwenye vikundi vyenu vya maombi. I promise nitakuja kutoa ushuhuda hapa.

Monday, March 23, 2015

LATE POST............BABY SHOWER

Haya wandugu  ukizungumzia one of my girls, yaani huyu humkosi kwenye list yangu, nampenda mnoooo na huu ujio wa huyu kiumbe  sasa dah! Mungu mwenyewe ndo anajua ni jinsi gani ninafuraha!!!!

Haya mamii yangu nakupenda mnooo unalijua hilo eti eh??? Mungu aliye Hai aendelee kukupigania yaani ha!ha!ha!ha! Mambo mengine natamani kuendelea kufunguka ila naogopa utanichapa ki!ki!ki!ki!



halafu we mrembo ujue??? hapo tuu Mama kitumbo dah!!!



ha!ha!ha!ha! mi sijasema kitu ujue......... Sema nini  Shemeji yangu ana shiiida



Deco by ?????


Mjengoni palinoga aiseee???

uko na nani hawa???

Atakae kuchukia wewe ana shida!!!  you are so sweet babe.....

The woman behind the Camera nimeona nisipitwe bila kuweka baraka zangu.....

oh dear !!! mwingine huyu yaani.......... nimejikuta nimemtoa kwenye list yamarafiki amekuwa my Dada aisee tunajuana wenyewe...........EE bwana kila mtu anamjanja wake a.k.a mtu anayetumika kwenye maisha yake aisee huyu Dada alitumika mara baada yakufika kwenye hii nchi ya wenyewe!! Aisee nimekumbuka mpaka nimetokwa na machozi.............................. Sorry Ney i shouldn't do this hapa  aisee nimeshindwa kujizuia..................i will always respect that Sarah!!!!!


mutu na maboss zake chezea kupendwa wewe vyeo pembeni ha!ha!ha!ha!

Bibi yetu  ha!ha!ha! nimemiss story zake.......


Shemeji ya mimi alikuja  kutuchungulia  akapewa adhabu hiyo yakuonja hivyo vyakula vya watoto aseme vina radha ya nini.......... alinimaliza kuniambia kimoja kina radha ya ukwaju ha!ha!ha!ha!

Friday, March 20, 2015

NISEME NISISEMEEE???

Ha!h!ha!ha!ntasema next time............... halafu  nyie si mnajua kwenye masuala ya selfie ni sheeder!!!  Ila nimejitahidi khaaa!!!Haya hiyo ndo my new makeup...................... ntakuja  nikirudi ntawambia imekuwaje sasa mbeba mabox na mimi nimeanza kuingia kwenye mambo yakujiremba ha!ha!ha!  Yamenikuta mwenzenu ntarudi kwi!kwi!kwi!

UPDATE
He nyie acheni kutaja taja majina ya watu basi, khaaa!! na hivyo vichambo mnavyonipa sasa loooh!!! hivi mmeshindwa kuvumilia kujua nataka kusema nini au??? Kweli Mungu atuhurumie aisee.............Halafu ujue nini  nilitupia hizi picha for fun yaani nilitegemea watu mcheeeekeeee...... maana mimi mwenyewe nilijicheka baada yakujimwagia maana nilikuwa sijielewi nafanya nini full kujaribu kila kitu sikujua nini kitatokea nikajikuta kichekesho lakini hapo hapo nikapata kitu cha utangulizi ya kile ninachotarajia kukisema.......... mbona imekuwa tofauti sana na mlivyolipokea eti???? kha!!  Sasa copy & paste ipi kwa mfano, hivyo nilivyojimwagia au???duuu!!kwa akili yako unafikiri nimeshindwa kuziedit??? au kutumia camera yenye quality????duu!!! km ndo  hivyo sasa nani ntamuuzia???wewe au??? basi ukikubali basi na wewe utakuwa mwenzangu na mie............(Products km products kweli mkombozi ila hizo picha hazikunia mauzo nielewe weweeeee) na talent ipi mnayozungumzia??? kipi kipya hapa kupaka wanja au??? halafu wanja wenyewe hapo nahisi nilisahau kupaka ha!ha!ha! heeee!! nyie hata kama  am full time kuosha magari,kusafisha vyoo jamani nina visiku vyangu na mimi za kujinaniliu yaani........nilianza kuiba wanja wa Mama Rose toka niko shule ya msingi nilichapwa  mnooo,nimejichora hadi na mkaa mjue??? baadae angel face ha!ha!ha! sema tuu sio yule mtu wa 24/7 ukiniona nafanya yamenikuta tuuu.... ndo utulie sasa ujue kwa nini yamenikuta...........

 Anyway nimejikuta tuu nimekasirika sio kwa sababu mmenichamba ki!ki!ki! moja ni kwa sababu yaani mmeenda mbali mpaka duuuu!!! yaani tungekuwa faster hivyo hata kuzitafuta aisee umasikini ungeisha.............. na kubwa lililonikasirisha nimejikuta nimewaza tuu, haya maroho ya hivi, yanayowakamata watu mnoo.......... mwisho wa siku mtu anafeel km hana thamani tena, haiwezekani,yaani anakata tamaa kwa sababu ya maroho yanayotumika namna hiiii.........Kwa mtu ambaye labda aliwaza afanye  ili apate namna kujitoa,au labda ndivyo alivyotakiwa kufanya, akikutana  na macomment ya hivi aisee, hivi unajua ni jinsi gani utakuwa umemkwamisha huyu mtu??? Ushindwe na mapepo yako ulipo....Humu ndani watu tumechoka tunataka kutiana moyo na michongo namna gani inawezekana............ wewe km kazi yako kupita pita nakuvuruga aisee wee kaa mbali ujue unacheza na wapendwa humu????ha!ha!ha! usiombe wakakulipua kwa maombi kwi!kwi!kwi!  Jamani hebu tuache hayo mambo yaani........ Hebu tutiane moyo.... Ntakwambia kitu kimoja kuna vitu ni lazima mtu aanzishe, au atumike kuamsha ndoto za mtu hii ipo mnooo............

Ntakupa mfano, leo nilipata invite kwa mtu fulani mzoefu mnoo kwenye  mambo ya biashara, Sasa tulikuwa tunaongea naye kwamba tunaona kunauhitaji sana wa kitu fulani kwenye hili eneo, kitu ambacho sisi tunajua wapi kwa kupata lakini hizi taratibu za nchi tunahisi zinaweza kutukwamisha........ Alitupa idea ambayo nafikiri Mungu alipanga ilitukapate majibu yetu kwa maana nyingine ametumika mnooo..... na wakati huo huo hicho ni kitu ambacho yeye hakukiwaza lakini anaona kabisa its a big deal ............. Nakwambiaje???? naamini kabisa anauwezo wakukifanya lakini atakavyokifanya yeye na tutakavyokifanya sisi am sure kitakuwa tofauti........ kikubwa  tusiweke chuki ndani yetu like kwa nini amechukua idea zetu na wala yeye asifanye kama anataka kutuibia idea, nakuhakikishia kila mtu atabarikiwa.............

 Mfano mwingine 
Wakati tunanunua hii biashara kuna mtu ambaye alikuwa interested kuinunua ila sema mambo yake hayakukaa sawa na muuzaji hakuwa tayari kumsubiri...... Sasa siku ya makabidhiano jamaa kaja amefuka moshi anataka biashara, mambo yamekaa sawa hataki kuamini km  Wana wa mfalme wameshajinyakulia muujiza wao ha!ha!ha! DUUU!!! jamaa alileta fujo fulani sie hao tukaondoka eneo la tukio..... ujue nini tulirudi tukapiga goti kumshukuru Mungu maana  kwetu sisi lile tukio zima lilitudhihirishia kwamba ni KWA NEEMA  kulikuwa kuna vingi vinaendelea nyuma ya pazia lakini Mungu alitupitisha...... few weeks later jamaa akafungua same business  mbele kidogo ya tulipo na kwenda around kwa wateja wa kampuni wakubwa, dizaini kama kuwachukua kitu ambacho kwa akili za kibinadamu naamini alikuwa na nafasi kubwa yakuwachukua, kwa sababu wanamjua  alikuwa rafiki wa aliyetuuzia, na wakati huo huo tuliamini yawezekana aliyetuuzia pia alishiriki ili kulinda ushoga  na jamaa maana ilibidi amsaidie kufungua (kuna vitu vilitufanya tuunganishe dots )na tulikuwa na kila sababu yakumshtaki maana mkataba haumruhusu kujiingiza kwenye biashara yoyote inayofanania kwenye eneo tulilopo......... In short Hakuna hata mteja  aliyefanikiwa kumchukua............. Na sisi mzigo ulikuwa ni bandika bandua hata kuwaza kuna mshindani mbele yetu saa ngapi????  kwa Muda fulani nafikiri Mungu alikuwa anamuandaa maana alitegemea vitu vingi negative kutoka kwetu ambavyo hakuvipata mpaka pale alipotulia......  Sasa hivi ndo tunamuona anafanya yake na sisi tunafanya yetu.  Mwisho wa siku nafikiri wote tumejikuta we were meant kufanya same biashara lakini kila mmoja kwa namna yake.........


 Ninachotaka kusema ni hivi Tatizo sio kufanya,Tatizo ni namna kinavyofanyika................

 Haya Sasa ndo msubiri mjue nataka kusema nini........ Itanibidi sasa nisema soon as i can maana nahisi kuna watu mna hamu uvumilivu unawashinda.... 

Otherwise napendaje sasa????

 Halafu nyie bwana nimenoga duuu!! ila tatizo pua khaaa!!! mnafanyaje sasa mbona kama ndo imevimbishwa ha!ha!ha! au ndo ya hivi hivi najifanya siijui??? ha!ha!ha!

Thursday, March 19, 2015

MAMA WAWILI..............


 Haya ndugu zangu, march  mpango ni yellow...... ili tuwe pamoja na wenzetu  wenye tatizo la endometriosis tuungane nao wapenzi, zimebaki siku chache bado unaweza ukafanya kitu sauti yako inaongeza idadi bado hujachelewa..........tuonyeshe tunawajali nakuwathamini eti eeeh!! Haya  mi ndo nimewanominate nyie wadau wangu wooote, mkafanye kunominate na marafiki zenu watano ili sauti isikike huko kwenye masocial media.............. 
Na km kuna mdau wangu humu na wewe hii kitu unayo pole sana wangu aisee nimewahi kubahatika kuishi na mwanamke wa hivi nyie acheni........ mbaya zaidi siku zile hutakiwi kusema yaaani labda km ni rafiki yako otherwise unaugulia mumo kwa mumo duuu!!! Mungu awatetee ufumbuzi upatikane. Sauti yangu na yako kwa Pamoja tunaweza........

msisahau ku #GOYellow4Endo#ManyfacesofEndo.




Monday, March 16, 2015

MAMA WAWILI ....................


mbili tatu basi zakuchangamsha genge eti eeh????
 suala la mnuno niachieni mwenyewe ha!ha!ha!ha! nahisi mlinisifia nikinuna napenda au ndo  sheria za Camera ha!ha!ha!ha!

haya nawapenda






Friday, March 13, 2015

TOTOZ DAY............................

Wamegoma kunipiga picha leo wamesema its their time............  haya Mama mtu nimegeuka kuwa mpiga picha leo
 
she is turning 5yrs next month jamani nyieeeeeeee!!!!


 haya mapozi yakupindisha mguu hata mimi siyaelewi  ha!ha!ha!

the face, when she is shy



Haya twende huku nako mmmh!!

 i know the talent please people dont remind me ki!ki!ki!ki!



 I promise....... Mumy will  support you babe..... ngoja kwanza tuweke msingi wa academic kwanza ha!ha!ha!


 soon my shoe closet will be stolen ki!ki!ki!ki! blame Dad for this.........

Sema nini??? siku hizi nawabania kidogo hawachelewi hawa, wakikua kuanza kudai haki zao, Mumy ilikuwaje  kuniweka weka kwenye mablog bila sababu ???? chezea watoto wa Obama wewe??? Naogopa mwenzenu!!!! Ha!ha!ha!ha!
nyie mwenzenu  hapo kwenye ukoka wangu nimeona uyoga km mitatu minne imeota........... nikakumbuka ule uyoga sumu watu walikula wakafa mnakumbuka??? Sasa Careen na yeye kauona wacha aanze kuukimbilia wee nilipigaje kelele stop Careen Sumu!!!! ha!ha!ha! Akajibu Sumu???!!!! what is Sumu????  maelezo yaliyoendelea siri yetu.........

 Tunawapendaaaaaa

Thursday, March 12, 2015

NIMEKUTANA NAZO........

 Ha!ha!ha!ha! leo bwana nimekumbuka maficho yangu imebidi niingie kwenye kumbukumbu zangu eee bwana sinimekutana hizi............... 

 Aisee zimenikumbusha mbaliiiiii nyie mwenzenu nilikuwa sijawahi kulala 5* maisha yangu yote mpaka siku ya honey moon (kempist) baada ya hapo ndo nikajimuvuzisha  huku na hii ndo ilikuwa my  first 5* kulala kwenye nchi za watu aiseee??? nyie ushamba mzigo nyie acheni tuu ki!ki!ki!
Mweee!!! acheni nicheke maana nikiwasimulia hapa Baba wawili atanichapa ha!ha!ha!ha!

  haya   chungulia my TBT......
 Mwanangu alikuwa na miezi 8 hapo.... duuu kweli siku hazigandi  ukimuona leo kweli ni NEEMA

 nyie bwana nahisi nahitaji wigi siku moja moja mbona kama nimekuwa mtamu kuliko mcharo??? Ha!ha!ha! au ndo kunyonyesha kulinipenda tupige namba tatu nini???

 Mwe jamani mwenzenu nilikuwa km nalea mapachaHa!Ha!Ha! Hapa Careen alikuwa km ana miaka miwili na miezi michache sema alikuwa  mrefu kuliko umri wake....

Mapozi sijaanza leo ujue???

Ujue nini sasa Basi wanetu walikuwa wakilala nasisi tunajivalia kiouting  humo humo hotelini tunafanya yetu ha!ha!ha!

Duuu halafu nyie my husband is handsome khaaaa!!! Acha niwe na wivu ki!ki!ki!

 Bye

Wednesday, March 11, 2015

HAKUNA JIPYA CHINI YA JUA............................

Imeandikwa mtu hataishi kwa mkate bali kwa neno la Mungu.......... We mwenzangu unalielewaje hili neno??  Umejaribu kila unaposoma neno na kulileta kwenye uhalisia??? Je ukitafakari hupati picha halisi ya yale yanayotendeka leo??? Nimejikuta na waza sana aisee?? 

Basi mwenzio leo nilikuwa namtafakari mtu mmoja tuu kwenye biblia  nikajikuta nimemleta kwenye uhalisia wa sasa.  Ngoja nikushirikishe........

YOHANA 12

Basi, Maria alichukua chupa ya marashi ya nardo safi ya thamani kubwa, akampaka Yesu miguu na kuipangusa kwa nywele zake. Nyumba yote ikajaa harufu ya marashi. 4 Basi, Yuda Iskarioti, mmoja wa wale kumi na wawili ambaye ndiye atakayemsaliti Yesu, akasema, 5 Kwa nini marashi hayo hayakuuzwa kwa fedha dinari mia tatu, wakapewa maskini? 6 Alisema hivyo, si kwa kuwa alijali chochote juu ya maskini, bali kwa sababu alikuwa mweka hazina, na kwa kuwa alikuwa mwizi, mara kwa mara aliiba kutoka katika hiyo hazina. 7 Lakini Yesu akasema, "Msimsumbue huyu mama! Mwacheni ayaweke kwa ajili ya siku ya mazishi yangu. 8 Maskini mtakuwa nao siku zote, lakini hamtakuwa nami siku zote."

 Namzungumzia Yuda Iskarioti na Maria.... Hawa watu wawili kuna mmoja amesimama kwenye nafasi yake na mwingine mdogo mdogo ameanza kuchomoka kwenye nafasi yake  ( Kumbuka ni mmoja wa wanafunzi waliotembea na Yesu, waliokula na Yesu,  kwa maana nyingi ni mmoja wa watu wakaribu mnoo wa Yesu si eti eeh???)......... 

 Ukisoma kuanzia mwanzo wa hiyo sura tunaambiwa Maria alikuwa akihudumia tuu, Nilivyotafakari mimi nahisi alihudumu kikamilifu, mpaka kuamsha kale karoho kachafu kalikojificha ndani ya Yuda kalikosa uvumili  Ha!ha!ha! halafu unajua nini, Shetani anavyotumika mahali mara nyingi huwa anakujaga na kadizaini fulani hivi , usipo kuwa makini unaweza shawishika, nakuona ni busara   kumbe kuna uovu ndani yake.......... HAKUNA JIPYA..........

5 Kwa nini marashi hayo hayakuuzwa kwa fedha dinari mia tatu, wakapewa maskini? 

Wow! busara si ndio hii  au we unaonaje????  Ha!ha!ha!

tuendelee

6 Alisema hivyo, si kwa kuwa alijali chochote juu ya maskini, bali kwa sababu alikuwa mweka hazina, na kwa kuwa alikuwa mwizi, mara kwa mara aliiba kutoka katika hiyo hazina.

 Hapo chacha........HAKUNA JIPYA...........

Kuna mambo mengi yakujifunza kutoka kwakwe, Kuna muda alikuwa anajistukia nakuuliza maswali ambayo ana majibu maana yeye ndo muhusika mkuu, ila alitaka ajue km amestukiwa, na mwisho wa siku  tamaa ilimzidi kabisa  nafasi ya uwanafunzi hakuithamini tena, utunza hazina hakuumtosha tena nahisi mbinu za wizi zilimwisha  (mi nami kwakuongeza chumvi duuu!!!ha!ha!ha!ha!)  jamaa akaona ajitose mzima mzima  Amuuze kabisaaaa Yesu  Ametisha eti eh!!!   HAKUNA JIPYA...............

Kuna kitu kingine nimetoka nacho hapa wakati Yuda hajielewi, Yesu alikuwa anajua anadeal na mtu gani.......... Alideal naye kihekima maana andiko lilikuwa lazima litimie......Kuna wakati alifadhaika (27 Sasa roho yangu imefadhaika, na niseme nini? Je, niseme: Baba, usiruhusu saa hii inifikie? Lakini ndiyo maana nimekuja--ili nipite katika saa hii)  

Sikia nikwambie mpendwa  NDOTO yako ni nini???  Je wajua unauwezo wa kuizika au kuifufua?? Wa Kina Yuda hawajaanza kwako, walikuwepo na wataendelea kuwepo. Wamewekwa kwa Makusudi  na makusudi hayo ili ndoto yako ikamilike..............

Ntakuwa mchoyo kama sitasema na Yuda wa sasa ........ Tumeambiwa mwisho wa siku Yuda hakuona thamani ya chochote pesa alirudisha nakuamua kujipoteza kabisa. HAKUNA JIPYA  huwa wanaishia kuwa maloser

Habari njema ni kwamba hii nafasi ya Yuda nayo  sio ya lazima uibebe mpenzi, Huwa inakuja kidogo kidogo ila mmmh!! ukishakuwa level ya juu aisee kukutoa kazi .......  Chezea shetani akishakuwa amejipigia chata yake??? Ha!ha!ha! Jamani Imeandikwa walio wangu na wajua........ 

 Kajiushauri 

kabla hujalala we jipe nafasi hata ya Dakika mbili ujue siku yako iliendaje yaani lazima utakumbuka na utajitambua tuu km ulivyofanya  ulitumika au sio hapa pia panahitaji na uelewa na jinsi yakuchanganua mambo.... Ha!ha!ha!  mi  natabia yakupiga story na Baba watoto bwana kiukweli mi mwenzenu siri ndo sina ukitaka iwe siri basi Baba watoto awe anaijua ha!ha!ha! yaani km kuna kitu niliwahi lkumficha  mmmh!!!  kama ni dhambi basi  nahitaji maombi yenu ki!ki!ki!ki! sasa sometimes huwa nampa story, ili kunogesha najikuta naongeza na chumvi ha!ha!ha! sasa  nikishaanza kujitathimini mwisho wa siku naanza kusumbuka yaani utanisikia best ujue pale mwenzio niliongeza na chumvi ilikuwa hivi ila mi niliielewa hivi ha!ha!ha! ntajitetea hapo bora mradi nibaki na amani ki!ki!ki!

 So ni hivyo ndugu ukijitengenezea kamda kakujithamini sio rahisi ukafikia hatua mbaya yakukutoa kabisa na kukusahaulisha kusudi lako.

Halafu unajua nini ndugu zangu Mungu wetu ni Mungu wa rehema yaani anasamehe!!! anachotaka ni wewe tuu kujitambua baasiiii.......


Nawapenda mnoo

Monday, March 9, 2015

AFRICAN ATTIRE.............................


Jamani ninavyojisikia yaaani!!!!!!!!! Aisee nyumbani ni nyumbani hata ubishe..... kutabaki kuwa nyumbani ............Kajisemea na Mama yangu mwanangu huko ulaya kumetosha  mrudi nyumbani sasa kha!!! Ha!ha!ha! 
 Nani huyu etiii???

 Mjanja wangu yule yule @akailatailors........ fanya kumfollow basi

Duuuu!!!! 


Haya zinawatosha eti eeeh???

 Nawapenda

Wednesday, March 4, 2015

SEMA TUPONE.............


Haya Wadau  nimeona nianzishe hichi kipengele cha SEMA TUPONE........
  Je una kitu unatamani Dunia ijifunze, Una shuhuda ambayo huwezi kutulia kila upatapo nafasi unatamani umuaibishe Shetani?? Ulikuwa nakifungo ambacho ulivyotoka hujielewi zaidi ya kurudisha utukufu kwa Mungu kwa ajili ya neema aliyoiachilia juu ya kifungo hicho??? Kwenye ulimwengu wetu huu wa social Media labda unaona kuna udanganyifu ambao shetani anatumia kupitia ungependa kusema kitu ili yule aliyekusudiwa aupate ujumbe????

 Wakati wako  ndo huu ifanye Blog hii iwe yako kwa hilo Maana nimejikuta nimekuwa mchoyo kila siku ni juu ya mimi tuu......... Kumbe kuna wakati na mimi nahitaji kujifunza kutoka kwenu.

Naomba Shuhuda iwe ya kweli wadau, ujue hapa dizaini km Madhabahu ha!ha!ha! ningependa kuwe kuna ukweli ndani yake ili mioyo ya watu ipone. Dunia ya sasa tumezukwa namaigizo mengi hebu sisi tuwe tofauti eti eeh!!

 TUNAMSHINDA SHETANI KWA USHUHUDA...... SHUHUDA ZA KWELI UJENGA NA KUINUA....

 Ila usije ukaniambia, shuhuda yangu nilipanda dala dala konda hakuniona nikashuka nakukimbia,  we ushindwa huo wizi usinishirikishe mwenzio.......

 Ngoja niwachekeshe nilikuwa na mpendwa mmoja kiukweli alikuwa wakuonewa huruma kutokana na historia ya maisha yake sasa alivyoanza kuja kanisani watu wakawa wanamuhurumia  wanampa hifadhi hee Mpendwa asianze maombi ya mwenye nyumba asahau nyumba yake na shuhuda anatoa Mungu kampa nyumba, Mwenye nyumba baadae nahisi akahisi kitu akatafuta namna yakumtoa weee, mpendwa aligoma nakufunga juu hiyo ni nyumba yake hatoki ha!ha!ha!ha! Mwisho wa siku alitoka wee Mungu wetu sio wadhuruma, ni Mungu wa haki   hafanyagi vitu kihivyo yaani dizaini hiyo utaipata labda kwa waganga wakienyeji ha!ha!ha!

 Haya nitumie e mail slayros@yahoo.com

Angalizo: nitakapo  publish  huo ushuhuda  usitegemee sana  comments  kikubwa ujumbe umesomwa eti eeh!!
 Blog yangu inasumbua comment nimelalamikiwa sana...........Sema nini???sina hela yakutengeneza website nyingine Ha!Ha!ha! jamani joke, bado sijaona umuhimu labda huko mbeleni tutabadilisha...... tatizo nilishawaona watalaamu ili nibadilishe  waliniambia  hilo jina (BE YOU) lazima libadilike  au kuongezwa ongezwa mavitu Duu!! Mama wawili nalipendaje sasa???

Mbarikiwe

Tuesday, March 3, 2015

MAMA WAWILI....................................

Muke ya Slay.......

 Mambo mengine majanga yaani...... hivi umewahi kutana na yule mtu ambaye stage fulani ya maisha hakupitia  anaanza kuleta fujo uzeeni??? Ahsante Yesu maana aliniacha nichafue chafue huko kwa muda wake akanitoa kabla sijamezwa kabisa mweee!!! ..............kweli ni kwa Neema!! 

Ila, kuna haka kajieneo nahisi sikuingia ndio maana nawaletea shida bloguni ha!ha!ha!  Mambo ya ulimbwende........... hivi nyie hamnistukii??? mi nishajistukia ukifika muda wa kamera....... duu!!! hayo mapozi halafu unaona yakulazimisha kabisa Ki!ki!ki!ki! we niangalie hapo juu huo mnuno na mishipa ilivyonitoka utajua tuu i wish  lakini haikuwa..........Nani alaumiwe eti???

Kwa maneno mengine nasema hivi,

Kuna haja   yakujua kwenye hii mitandao nani kapost,  kwa nini unataka uwe wewe? je kuna haja?? unahisi unachokiona na kukitamani  ndicho kilivyo kwenye uhalisia?? Je unatamani na wewe uonekane? au unataka uonekane kwasababu  ni kweli hicho kipo ndani yako(ndoto)??? 

ntakupa kajimfano 

Kabla ya kutolewa shimoni kuna kitu nilikuwa nafanya kwa sababu walionizunguka wanafanya........ Aisee kilevi mwee!!!!!!  kwanza ulikuwa ukiniuliza natumia kilevi gani?, sijui, Ila nilikuwa na hakikisha kundi ntalokutana nalo linakunywa konyagi na mimi nimo , sijui Serengeti nimo Ha!ha!ha! na mwisho wa siku lazima niwaonyeshe Mimi mlevi zaidi yao yaani... Halafu nikwambie unafikiri ule uchungu nilikuwa siusikii?? Maumivu nilikuwa nayapata pale pale, tatizo watanionaje kama mi mjanja sasa?? 

 Aisee sikumbuki kama kuna siku nilikunywa bila kutapika..... halafu nikigundua washikaji wameniona natapika, Nilikuwa nawambia ujue leo nimeanza kilaji kabla ya kula ha!ha!ha! uongo mtupuuuuu!!! chezea umaarufu wewe???

  Sometime huwa najisemea Labda roho wa Mungu alikuwa ananifanyisha vile, maana alijua sio wa pande ile........   na mara nyine najisemea labda ndo maana haikunichukua muda kuacha, maana hakukuwa na uhusiano mzuri na mwili wangu zaidi yakutaka mahusiano na wale wanaonizunguka............, Lakini pia namshukuru Mungu mnoo kuniruhusu niingie kwa muda sahihi nakunitoa kwa muda sahihi.......kunileta kwenye nafasi yakujitambua na hata leo nina nafasi yakushuhudia kwa mfano halisi................................


 Bora hapa nimelegea kidogo mwee............ ntazoea tuu we ngoja ha!ha!ha!ha!

 Nawapenda