Pages

Ads 468x60px

Monday, April 30, 2012

DREAM 2

Wanasema "Cheka na wanao cheka , lia na wanao lia" hivi ndivyo utu  unapoanzia..... Ukiona  mwenzio analia tafuta hekima yakumfuta machozi  mpe story nzuri, mtie moyo  kwa namna yoyote ili asonge mbele  Kwani , JARIBU NI KAWAIDA YA MWANADAMU ............... Na mwenzio anapocheka, cheka nae japo moyoni unamajeraha ambayo huoni tumaini kabisa, Jitie moyo jisemee mwenyewe kama mwenzangu kaweza hata mimi siku yangu ipo..........

NAYAWEZA YOTE KATIKA YEYE ANITIAE NGUVU.



USHUHUDA HUMJENGA YEYE ALIE NA HEKIMA NA UFAHAM, BALI  HUMBOMOA YEYE ALIYE MPUMBAVU.................

Hivi ndivyo mama wawili alivyoamua kushuhudia wiki hii kwa habari ya ndoto zake ambazo ni kwa neema tu zimefanikiwa si kwa nguvu wala uweza bali ni..................  ni mengi wapendwa siwezi hata kuyahesabu na haya unayoyaona ni 2012 tu

JINA LA BWANA LIBARIKIWE

haya wadau km mnakumbuka nilikuwa na likizo ya week sita. ambayo mimi na familia yangu tulitumia 2weeks kwa ajiri ya msiba kijijini na 4weeks tulirudi Dar.yaaani nilikuwa busy sikuweza kupost wala kuwaona baadhi ya watu.............. ambao wengine  mlisema najificha coz maisha yamenipiga, n.k
Ok this is what i was busy for.............
Ahsante Mungu kwa kuniwezesha kwa wengine ni kawaida lakini kwangu  bado  ni muujiza.











kazi ilikuwa haijaisha lakini, muda na nguvu ndio iliishia hapo sikusita kuwaita watumishi  weeeeee

TUKAHARIBU, TUKANG'OA  TUKAMILIKI NA NAKUPANDA MBEGU NJEMA HAKIKA  BWANA AKAJITWALIA UTUKUFU.
AHSANTE MCHUNGAJI SEBA NA MTUMISHI DEO BWANA NA IANGALIE HAJA YA MIOYO YENU

IN GOD WE TRUST

Sunday, April 29, 2012

MY DREAM

Wakina fulani wanasema " i got my new bby" Mama wawili nasema hivi...... "Ama kwa hakika tumeuona mkono wa Bwana" kwa kweli inatia moyo unapoomba Mungu na kufanya juhudi zote ili kukamilisha ndoto yako hasa kina sie wabeba mabox,tuliopewa majina yote mabaya yasiokuwa na idadi, na tena walitunyooshe na vidole wakasema na tuone ataishia wapi, lakini tulisonga na kumuangalia yeye aliyekuleta dunia kwa maana twajua yakua yeye ndo ajue mwisho wetu.............
kina sie ndani ya 2012 model tena march production!!!!!!!
JINA LA BWANA LIBARIKIWE!!!!!!










Haya mdau week hii itakuwa ni juu ya nini Mungu amekutendea na huoni sababu yakutulia lazima useme kwani kwa wengine yaweza kuwa kawaida lakini kwako ni muujiza kwa kweli hasa ukiangalia ulikotoka mmmh!!!!!! unaishia kusema  Ni kwa neema tuuuu!!!!!! . Usione aibu nirushie uwatie moyo wawili watatu watambue kuomba kwao na juhudi zao watarajie faraja mbeleni kwa Mungu yupo.

IN GOD WE TRUST


Thursday, April 26, 2012

MTAZAMO

 Wadau kama mnakumbuka miezi michache iliyopita suala la yatima lilizungumziwa sana hasa katika blogs mbalimbali, kiukweli mpaka wakati huo nilikuwa sikuwahi kupata mzigo juu ya ibada hiyo ya yatima, yaani nilikuwa najua kuna yatima lakini sikuwahi kuumia sana kwa habari ya kufanya kitu juu yao zaidi ya wale walionizunguka mfano ndugu, nao sio kihivyo zaidi yakuchukulia km ndugu wasiokuwa na uwezo, Sikuwahi kujiuliza hawa watu km yatima wanatakiwa kuhudumiwa vipi, maumivu wanayoyapa, wanatofauti gani katika jamii na mambo km hayo, na cha ajabu zaidi hata katika kusoma kwangu maandiko nilifungwa kabisa ufahamu juu ya hili, nilikuwa nasoma tuuuu km gazeti lkn utendaji sikuwaHI kuupata.......

Nashukuru Mungu kupitia muda huo ambapo nahisi ndio ulikuwa wakati wa ufahamu wangu kufunguka  kupitia blogS hizo. Ndipo nilijigundua mimi ni nani? na tofauti iliyopo kati yangu na yatima, na ninatakiwa kufanya nini juu yao japo kwa sehem fulani. Kwa kweli nilijikuta nina mzigo mkubwa sana kuna kipindi nilikuwa nasoma mpaka ninalia mwenyewe, nashukuru MUNGU niliweza kushiriki kwa namna moja ama nyingine.Cha ajabu haikuishia hapo nilijikuta nikiwaza sana juu ya hili, kuna wakati hata nilikuwa nawaangalia wanangu wakinirukia ,kunichezea na kunifanyia lolote ambalo litafanya tufurahi km familia, kitu kilinikumbusha kuna mtoto yupo mahali fulani hajawahi kuona hata jino moja la mzazi tena hajui furaha ni nini ktk maisha yake. Kwa kweli inaumiza wapenzi.............

Jamani nikitaka kuzungumzia how i feel!!!!!! kwa kweli ukurasa hautaishia.Mwezi uliopita nashukuru Mungu nilifanikiwa kuja bongo japo nilikuja kwa majozi yakumpoteza baba mkwe wangu( REST IN PEACE MY FATHER)   Lakini nilijifunza kitu jamani,!!!!!!!!! nikiwa bado akiri yangu haijatulia juu ya yatima nilikuwa tayari kuna kitu ambayo tulikuwa tunasave km familia, Tulianza kufanya research ni wapi ambapo panastahili sisi  tufanye kitu na hatukutaka kwenda vituo ambavyo viko popular coz tulijua hivyo huwa mara kwa mara vinapata kitu japo bado niwahitaji.ndugu zangu kunastory huko uuuuwiiiiiii!!!!!!!

 Mmmh hivi km kweli hakuna dhambi kubwa wala ndogo jamani......HII NI LAANAAAA  kweli unafungua kituo misaada unayopata haifikii walengwa!!!?????? pesa unatumia kwa mahitaji yako unaacha viumbe na njaa!!!????  vyakula vinaletwa walezi mnapeleka majumbani mwenu na viumbe vinateseka na njaa!!! ???????yaani we binadamu wa dizaini hii uuuuwwiiiiii!!!!!!! ndugu yangu kweli kweli umeamua kuwafanyia biashara viumbe hawa?????? kweli najua kuhukumu na kulaani si kwangu ila naomba utambue hukumu ipo na laana ipo na lazima ioneka kwa macho, malipo ni hapa hapa ndugu yangu, Kweli hakuna mkamilifu chini ya jua lakini.................we haya.

MTAZAMO
 Kwa ndugu wote ambao mnaguswa na yatima  na mnaguswa  kufanya jambo kwa ajiri yao msikurupuke tuuu kwa sababu nikituo kwani unaweza kujikuta hujafikisha lengo, japo kuwa kule kuwaza tu, kwaajiri ya  yatima nakufanya kitu  halafu watu wenye mikono mirefu wakakwamisha lengo MUNGU akubariki sana.PIA tukumbuke"WATU WANGU WANAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA"  Haisaidii km unatoa huku unajua kuna utapeli utafanyika,Yaani chunguza sana kwa kweli ikiwezekana omba Mungu akuonyeshe ni wapi unatakiwa kwenda ukiingia kichwa kichwa wanahadithi ndefu sana hao,NAWAOGOPA SANA KWA KWELI SIJUI UJASIRI WANAPATA WAPI???????? hata km maisha magumu mmmmhhhhh!!!! hii kwa wale ambao wanajikongoja km kinasie uwezo wakuwakusanya au kuchukua hata mmoja kukaa nao wenyewe kwa sasa hatuna  ILA, kwa wewe mwenzetu uliojariwa hata kumchuka mmoja au zaidi na unauhakika utaweza kwa kweli mchukue........ Hawa watu niwahitaji kwa kweli na pia jikaguo usije baada ukaingia tamaa na kufanya km hao tunaowazungumzia maana naamini wengine walianza kwa kupondeka hivi hivi lkn roho za tamaa badae zikawaingia.

ANGALIZO
1. Sijasema vituo vyote ni vya kitapeli, Kuna watu kweli Mungu awabariki sana kwa kazi mnayofanya kwa mda mfupi nimeona magumu mnayopitia lakini mmeweza kuthubutu, kweli ni roho yakipekee sana  na Mungu anatambua hicho mnachokifanya msikate tamaa.

2.Sijapigia debe kituo chochote wala sijasema nilipoenda mimi ndio perfect or not. na popote nilipofika au kuulizia lakini sikufanya chochote sijasema ndo nyie wenye midomo mirefu hapana,km nilivyosema mwanzo kuhukumu si kwangu lkn ukidanganywa km uko makini utastuka tuuu.

3.KWA HILI SITAFUTI SIFA ILA KUNA WAKATI INABIDI TUAMBIZANE KUTUMIA MIFANO HALISI ILI TWENDE SAWA.( NATAMBUA UNAPOTOA SADAKA USITAKE MKONO WA PILI UTAMBUE UMETOA NINI)  NA PIA JIULIZE, BILA MTU MMOJA KUSIMAMA NA KULIZUNGUMZIA HILI SUALA MIMI MAMA WAWILI UFAHAMU WANGU UNGEBAKI PALE PALE HATA LEO HUU MTAZAMO NISINGEANDIKA.

                                                IN GOD WE TRUST

Wednesday, April 25, 2012

TULIWAKUMBUKA KIHIVI




Haya wadau hivi ndivyo mimi na familia yangu tulivyoamua kusherekea birthday ya mtoto wangu Cristabell baada ya kuona tuonanne kwenye topic ya mtazamo juu ya hili ujue kwa nini niliamua hili na nimejifunza nini juu ya hili....................................Picha na maandishi nimecopy na kupast kutoka kwenye blog ya mlezi wa kituo Miriam kuona zaidi ingia gurdianangel blog.

THANKS A LOT!

Tunashukuru sana familia ya Mr & Mrs Mbeyela kwa upendo wa hali ya juu mliouonyesha kwa watoto wetu wa kituo cha Guardian Angels kwa kutuletea zawadi mbalimbali kama magodoro, Simtank, Mkaa, majiko, mchele, unga, sukari , dawa za meno, mafuta, mafuta ya kupaka, majani ya chai, neti mboga, maharage na vitu vingi vingine kama vinavyoonekana kwenye picha.

Zaidi ya yote kwa kuja kusheherekea Birthday ya binti yenu Isabela pampja na watoto wetu kwa kweli tumefurahi sana na ni upendo wa hali ya juu mliotuonyesha, kwani mngeweza kufanya sherehe nyumbani kwenu na kufurahia huko lakini mkaona ni vyema kula na watoto hawa ambao wengine walibaki wanashangaa tuuu maana hawayajui mambho hayooo! Na kesi mmetuachia kila mtoto anataka kufanyiwa Birthday !

Mungu awabariki sana pale mlipotoa awaongezee mara dufu na karibuni sana kututembelea hata kama hamna cha kutuletea watoto wamewapenda sana!

Thanks Once Again & Be Blessed!
















KWA PAMOJA TUNAMSHUKURU SANA MUNGU KWA NEEMA HII HATA YAKUWAKUMBUKA HAWA WAPENDWA WETU KWA KWELI BINAFSI NILISIKIA AMANI YA ROHO MARA BAADA YA HILI TENDO KUISHA JINA LA BWANA LIBARIKIWE 

Monday, April 23, 2012

NILIWAMISS JAMANI!!!!! NINAWAMISIJE??????


KANISA LA BWANA  NAWAPENDA KWAKWELI NIMEFURAHI SANAAAA KUIKANYAGA MADHABAHU YA BWANA TENA MUBARIKIWE (MAMA WAWILI AKISALIMIA WAPENDWA)

MY MAMA AKIKASIRIKA NA KUPIGA MAOMBI KWA NINI SINENEPI AKINIAMBUKIZA UNENE...... KWIKWI KWIKWI LAKINI MIMI NIKANDAMIZA MAOMBI KIMOYO MOYO  NIKIOMBA KILE AMBACHO MUNGU AMEWEKA NDANI YA MOYO WA HUYU MAMA HATA NUSU NIKIPATE.....YAANI HOFU YA MUNGU, HEKIMA, HESHIMA, UPIGANAJI, MOYO WA UNYENYEKEVU,UVUMILIVU NA .....................mdau siunaniona nilivyokumbatia huo moyo?????


AKITUKARIBISHA NYUMBANI MWA BWANA TENA NA TENA NA TENA

JINA LA BWANA LIBARIKIWE

Sunday, April 22, 2012

Wednesday, April 4, 2012

HAPPY ANNIVERSARY TO US

MIAKA MINNE ILIYOPITA TAREHE KAMA YA LEO  BABA WAWILI NAMAMA WAWILI HATUKUSITA KUSEMA" MPENZI NAAPA KWA AKIRI NA UTASHI WANGU WOTE KUWA NTAKUPENDA NA KUKUTHAMINI KATIKA SHIDA NA RAHA WEWE NI WANGU MILELE" AAAAAWWWWWW!!!! NIMRUDISHIE NINI HUYU MUNGU KWA NEEMA HII????????????????? MUNGU WANGU NA AJITWALIE UTUKUFU KWA MAANA AMEKUWA NI NURU NA USHINDI KATIKA SAFARI HII.AMEEEN





Tuesday, April 3, 2012

MR&MRS TULIKUWEPO NAKUSHUHUDIA




wadau nimeona maoni yenu yaani kumbe mnanipenda eeh??????????  yaani mama wawili penda sana nyie.................. yaani kupita kiasi mnisamehe sana  nipo busy wapenzi simnajua tena home sweet home????????? mambo mengi muda nilionao huku ni mchache nna km wk moja more na mambo hayakamiliki kabisa nivumilieni sana tuuu............. nina mambo mengi saaaana yakuwapa ila mda unanibana sana sana @ ntakuwa narusha rusha mooja mbili sio mbaya baada ya 2 wks tutaanza mambo au sio