Pages

Ads 468x60px

Friday, January 29, 2016

NYUMA YA PAZIA...........


Tulifika kihivi yaani???  kwa kweli ilikuwa surprise..... nature ya biashara yetu kweli inategemea upepo umekajee ... six days before ndo tukawa na uhakika wa safari hivyo hatukuweza kumshirikisha mtu mpaka nilivyokata ticket.....Ticket zenyewe ndo high season mkinga mie nilikuwa nahesabu mifuko ya cement tuu  ha!ha!ha!........ila nilikuwa sina jinsi ha!ha!ha! so 5day before kufika Tanzania ndo tukaanza kuwambia wazazi watoke mikoani kuja kutupokea na wengine kuwasafarisha tukakutane kijijini  zaidiiii ha!ha!ha!

ntakwambia kwa nini kijijini endelea kunichungulia...........nyie haya unafikiri kwa nini wenzetu wachaga tunasema wanaenda chimba dawa??? kuna baraka zake kuleeee. ila sema nene unafanyaje??? je inampa Mungu utukufu?? Ama ndo kuongeza maagano ???

 kutana na watu wangu basi.......

Mama Rose mnamfahamu na Mama Suleiman je??? jaza nafasi zilizo wazi ha!ha!ha!

(yahaya unaishi wapi??? mbona unafikia mahotelini?? yahaya weee yahaya ha!ha!ha!ha!)
ngoja nijitetee jamani kibandani hatukuona hekima kusumbua watu wanaishi jamani kha!!!kwa mda wenyewe wa siku kadhaa............

na shangazi yao mwenyewe mimi namuita Mama mwenye nyumba . jamani huyo ndo Dada ake Mama wawili yaani toka yeye mimi nafuata........... ila kanidunda huyo utotoni kha!!! 

 Mutu na sheji yake tunamwita  The Boss .......yee ndo bwana mipango yote ya mjini anatutoaje ushamba ha!ha!ha! Dogo tumekaa nae akiwa shule yaani ilikuwa kila kitu Dada Rose,Dada rose duu!! sa hizi nimerudi eti  namwita boss wangu ha!ha!ha! (haya huyu ndo nilimuachia ziwa kwa Mama yangu...... kuoa Bado lakini ....wapendwa maono vepe??? ha!ha!ha!)


Boss hivi ile kesi ya makontena vepe imeisha ama?? Ha!ha!ha!

Bwana wee hivi mnajua Mama Rose mapenzi kwangu hamna kabisa habari yote iko hapa yaani.......
akisikia sauti tuu mbona atachinja ng'ombe!! ha!ha!ha! ila kwa Rose akijitahidi sana Kuku tena mgonjwa ha!ha!ha! joke jamani ila kuna kaukweli kidogooo


Eneo langu lakujidai mimi lipo hapa....... asikwambie mtu Bwana, sikilizeni hakuna eneo muhimu kama hili,  Hili eneo linabaraka zake aisee,Tatizo lenu mnaingia fake mnataka kumaliza na  uhalisia. Maeneo km haya ingia kiuhalisia, misingi yako isiyobadilika iweke sawa, ijulikane km black black, white white Kikubwa unyesha upendo wa kweli huku ukisimamia kweli...............Mwanzo inasumbua naweza kusema tena sana.........(ni kawaida hata paka anajihami akiona sura ngeni)....... ila ukikaa sawa sawa mbona system itakaa sawa........ yaani utadeka  nakwambia..... mi mwenzenu hapa basi km ni mtoto  mi mziwanda ha!ha!ha! kaka yenu  atafuata badae.eee.....ha!ha!ha! Ila km uliingia Fake  halafu unataka kuleta uhalisia wako mbeleni best hilo unalo endelea  kuvumilia tuu ha!ha!ha! ndio maana ake si ulivumilia ili ndoa ikamilike basi tena, ndoa haishi mpaka kifo yaani tena ukicheza sana kuna baraka utajifungia....... otherwise omba Rehema ya ufunguzi kwao na utubu kwa nafasi yako.(wakubwa tuu ndo wanaelewa hapa na nyie watarajiwa kamata hii)

Kwa herini

Thursday, January 28, 2016

HODI HODIIIIIII............

Haya turudi jamani Mapumziko yameisha............... kiukweli nilikuwa na Muda mzuri sana Nyumbani..... aisee nyumbani ni nyumbani  kha!!! Amaaa mnajinoma chaa!! 

Ninachoweza kusema heshimu mahali ulipo kwa wakati huu.... unaweza kuwa na ndoto labda za kuwa sehemu nyingine............ wakati unachuchumalia hiyo taji ya kutimia ndoto zako, bado endelea kuheshimu nafasi na mahali ulipo. Kuna kusudi Mungu kukufanya uwe hapo ulipo......... hakuna kitu Bahati Bwana nani kakwambia??? (ila tuna neema ya Mungu ambayo pia inategemea nafasi yako umeichezaje?)haya mapicha picha yamitandaoni yanatuharibu sana akili, nakusahau kusudi mnajua??? mbaya zaidi asilimia kubwa ni fake fake tuu yaani tunawadanganyaaa...........(tufanyaje sasa na nyie mnapenda kudanganywa??? ha!ha!ha!)   Ninachotaka kusema ni hivi,Acha kulaani ardhi aliyokupa Mungu kwa wakati huu, wajibika sawa sawa kwa nafasi yako., Huku ukimkumbusha Mungu haja za moyo wako..........EE Bwana Mungu wetu ni mwaminifu asikwambie mtuu.....

Ni vizuri pia kumruhusu Mungu kuichunguza hiyo ndoto yako nakukupa amani maana, sio ndoto zote zinatoka kwa Mungu. Ni hivi wapendwa ndoto za kweli huwa hazi shut down yaani ...... zinaflow japo kuna kuwa  na ups and down lakini lazima kuna upenyo ambao unakuelekeza kuingia hatua baada ya hatua, yaani huwa inamuendelezo fulani ............Na wakati huo huo hauna uvivu wakufanya mambo mengine yaani kama ni uwajibikaji mahali ulipo unaendelea tuu......

 Ukiona una ndoto halafu imefikia hatua yaani haikufanyi kuendelea umebaki kulaumu tuu nakutamani tamani sijui fulani kawa hivi unaanza kuanza kujaribu nawewe kuwa yeye umesahau ndoto yako....... Mpendwa anza upya tuu hiyo ni dalili ya muovu kutaka kukumaliza.Ikiwezekana na utubu kwa kutoroka ndoto zako kutaka kuparamia ndoto za wenzio ha!ha!ha!

Namshukuru Mungu kwa ajili ya Tanzania yangu na watu wangu..... Eee Bwana watu wanakomaaa Bwana duu!! pamoja na kuwa mafisadi walitaka kujibebea nchi ...............Mungu anaangalia watu wake Bwana......... Mungu anamahesabu yake aiseee...  kweli nimeona mabadiliko makubwaaa........Yaani nahisi hasira za mabox zimeongezeka  ha!ha!ha! Unajua nini wengi hamyaoni labda kwa sababu tunaangalia mabaya tuu  mazuri hatuyaoni(tabia za kichoyo hizo ha!ha!ha!)  au labda mmezoea tuu yaani mnaona kawaida( mshindwa!!! hivi hamjipagi hata dakika kutafakari ukuu wa Mungu ndani ya maisha yenu???) au wengine ndo hivyo  tena kote wapo , ni lawama tuu kinachofanywa na wao ndo bora  kuliko cha wengine ha!ha!ha!( maisha ya kujikweza, umesahau Mungu anamuinua yeyote ampendae) 

Nimesema Hodi haya mnikaribisheee ha!ha!ha! 

  haya mapicha vepe.......
Mama mapicha nikiselfie

hebu angalia hapo utakubali mi muosha magari?? ha!ha!ha! labda unichunguze kucha zilivyo zakikazi ndo utashtuka ha!ha!ha!


Muke ya Slay


 hizi picha zilipigwa siku ya pili tulivyokuwa mjini tukienda kitaa wenyewe

Haya ntawarushia yaliyojili kama kuna yale niliyojifunza au km kuna kitu nataka kukizungumzia ama vepe???

 Nawapenda

Monday, January 11, 2016

NIPOGO

Hata mimi nimewamiss sana wadau laptop yangu sijui imekorofishaje sijui siwezi upload hata simu siwezi sijui ushamba 😀😀 otherwise tuvumiliane Mjage Instagram ndo kidogo naweza rusha mawili matatu.

Nawapenda