Pages

Ads 468x60px

Sunday, May 31, 2015

BADO NI MBINU ZA MUOVU..................

 Unajua nini?? iko hivi, kila kitu huwa kina sababu, ni vizuri kukipa nafasi japo hata kwa sekunde kukitafakari.......... Waamini tunaamini Mungu anaweza kutumia kitu au mtu kusema na wewe...... 
Mara nyingi huwa na tofauti ya mapokeo labda kwa sababu aliyetumika ameshindwa kufikisha ujumbe au mpokeaji ameshindwa kuupokea km ulivyokusudiwa................. 
Kushindwa/kuweza kwa hawa wawili kupokea au kutoa ujumbe huwa kunatokana na mazingira au mahusiano yao.........
Ninaposema mazingira ninamaana hii, labda ujumbe ulivyokuja umekuja katika muda ambao kiakili za kibinadamu unaona kabisa sio sahihi yaani hutaki kuamini kama huo ujumbe umekusudiwa kwako.... unachotaka kuamini kwamba ni haters tuu ............. 

Sikia ni kwambie adui huwa anatumika vizuri sana kukupa ujumbe, kwa kauzoefu kangu haka kadogo niliko nako,nimegundua hana huruma yaani ,hajali maumivu ya muhusika,mara nyingi huwa anajua uhalisia uliopo ila huwa anatafuta namna yakuitosheleza akili yake ijue kile cha uhalisia sio cha ukweli maana hakifurahi kukiona, akiwa kwenye harakati za kuvuruga na kutafuta mbinu za kuvuruga hapo ndipo pia anapoanza kutumika ha!ha!ha! Mungu atamtumia kukupa ujumbe how bad adui anawish kukuvuruga...... ni namna tuu yakukumbusha endelea kuishika hiyo neema uliyonayo...............wakati huo huo adui hawezi jua km anatumika for a good reason yeye ataamini amekupata sasa ha!ha!ha!ha! si tayari amejipatia kaushahidi kakuiridhisha akili yake!!!!atahakikisha anavyokufikishia ujumbe hilo jambo limejeruhi hisia,akili,............... maana hizo ndio ndoto zake bila kujijua anatumika............  ki!ki!ki! kwani???? hujasikia, Mwizi huja ili kuharibu,kubomoa na kuiba????? unategemea nini hapo sasa???? Mpendwa SILAHA ZA KIROHO.

 ninachotaka kukutia moyo hizo bado ni mbinu na pia ni ujumbe unaokwambia usijisahau sana, pamoja na yote endelea kujivika silaha....... kuna mambo yanayoendelea nyuma ya pazia ambayo Mungu hajataka kukufunulia, Adui halali huko aliko anatafuta kila mbinu kuyavuruga hayo mazingira uliyo nayo sasa..... Mungu ameruhusu tuu usikie labda km uvumi ili usijisahau...........
1Petro 5:8 (Mwe na kiasi na kukesha,kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi,kama simba angurumaye,huzunguka zunguka akitafuta mtu ammeze)

mapicha time eti eeeh???? haya twende sasa
nani hawa eti???

wamejificha eti...........
  Mungu ndie ajuaye........... Sitasahau fadhili zake maana amekuwa mwaminifu.... wala si kwamba sisi tu hodari, au tumetenda zaidi ni Neema tuu. 

duu!! ndo utaelewa why i love high heels ha!ha!ha!



NAWAPENDA MNOOOOO

Wednesday, May 27, 2015

MBINU ZA MUOVU..........

Hivi imewakukuta siku unachokiona mbele yako ni nguvu ya shetani inayokwambia huwezi????  umeshindwa??? you are not the best??? ukichunguza sana jambo hilo na wewe unajiona umefanya sana kwa nafasi yako unashindwa kuelewa imekuwaje???? Ngoja nikukumbushe km unaona kabisa kimwili umewajibika  bado hiyo nguvu unaona mbele yako juu ya jambo fulani,  best tambua hiyo ni roho, na roho inaondoka kiroho yaani......... Fanya kuingia kiroho pigana kiroho kumbuka unapoingia kiroho ingia kiujasiri maana tayari umejua siri.... Unajua nini??? adui hana jeuri yakuingia mzima mzima ila huwa amejipanga ........... anaanza mdogo mdogo kukutekenya, ukitekenyeka tuu  na kuzaa hofu basi! hilo kosa la kumpandisha kiwango.......  Wana wa Mungu hawana hofu kama hunielewi kasome Isaya 43
nimesema chunguza ujue tatizo limeajer???
 lipo pozi kidogo km la Mama wawili ha!ha!ha!

cheza kiroho  uliyenaye ni Simba wa Yuda ujue???? tatizo ni nani???vumbi lake atalikuta mbele ya safari


Mapozi ya ushindi hatusemi kwa akili zangu bali tunamuinua yeye aliyetuwezesha.........


Nawapenda

Monday, May 25, 2015

NANI HUYU ETI???????

 Nazidi kuwa mcharo mtoto wa mkulima au misifa tuu najifagilia??? ha!ha!ha!



nimenyoooka 

mapozi.........


 haya mawazo naona ha!ha!ha!

 feeling me self.........

 penda nyie........ nyie bwana mkiona kimya mjue mabox yamechanganya chezea bills za ulaya wewe.... Bwana we mshukuru Mungu popote ulipo kubaliana na mazingira , maisha ni popote ambapo Bwana ameruhusu uwepo kwa wakati huo... Hakuna short cut but you have choice ................. unatakaje kuwa, akili yako unailisha nini???? au unailisha mabaya huku ukitegemea matokeo mazuri??? MINDSET ndo chanzo cha hapo ulipo........

 Nawapenda

Wednesday, May 20, 2015

NIPOGO..........

Nyie bwana tatizo mabox  mwenzenu khaaa!! chezea bills za ulaya nyie ha!ha!ha! otherwise nipogo wapenzi wangu.... haya mimi huyo...

Mama yao wawili........
shoe game ...... napenda viatu mwenzenu mweee mpaka najihurumia......

 binti wa Yesu mie ndani yamapozi

hapa sijui ndio nini kha! labda nilikuwa nataka kuwaonyesha nina balance yaani naweza kusimama kwa mguu mmoja ha!ha!ha! chezea mapozi ya uzeeni wewe???

 haya nawapenda

Wednesday, May 13, 2015

MAMA WAWILI...........


Mwenzenu hako kakofia ndo zawadi ya siku ya wa Mama ki!ki!ki!




nikajifanyia naka tea party kamwenyewe mwenyewe chezea wewe  raha jipe mwenyewe ukingoja watu wakufanyie  utasubiri sanaaaa..... watu wanawaza bills mpaka wakakukumbuke ni neema ujue...........ha!ha!ha!

Mama ya nani huyu????
 haya sasa kasimama.......

Sunday, May 10, 2015

HAPPY MOTHERS DAY WADAU.............

MITHALI 31

10Mke mwenye sifa nzuri, ni nani awezaye kumpata? Yeye ni wa thamani sana kuliko marijani. 11Mume wake anamwamini kikamilifu wala hakosi kitu cho chote cha thamani. 12Humtendea mumewe mema, wala si mabaya, siku zote za maisha yake. 13Huchagua sufu na kitani naye hufanya kazi kwa mikono yenye bidii. 14Yeye ni kama meli za biashara akileta chakula chake kutoka mbali. 15Yeye huamka kungali bado giza huwapa jamaa yake chakula na mafungu watumishi wake wa kike. 16Huangalia shamba na kulinunua, kutokana na mapato yake hupanda shamba la mizabibu. 17Hufanya kazi zake kwa nguvu, mikono yake ina nguvu kwa ajili ya kazi zake. 18Huona kwamba biashara yake ina faida, wala taa yake haizimiki usiku. 19Huweka mikono yake kwenye pia, navyo vidole vyake hushikilia kijiti chenye uzi. 20Huwanyoshea maskini mikono yake na kuwakunjulia wahitaji vitanga vyake. 21Theluji ishukapo, hana hofu kwa ajili ya watu wa nyumbani mwake, kwa maana wote wamevikwa nguo za jotob. 22Hutengeneza mazulia ya kufunika kitanda chake, yeye huvaa kitani safi na urujuani. 23Mume wake anaheshimiwa kwenye lango la mji, aketipo miongoni mwa wazee wa nchi. 24Hutengeneza mavazi ya kitani na kuyauza, naye huwauzia wafanya biashara mishipi. 25Amevikwa nguvu na heshima, anaweza kucheka bila kuwa na hofu kwa siku zijazo. 26Huzungumza kwa hekima na mafundisho ya kuaminika yapo ulimini 

Na kwa wale single mothers wooote kumbuka Mungu anawapenda................


Friday, May 8, 2015

MSAADA WA KIROHO.................



Eti wadau sote tunajua kwamba Mungu anamtumia mtu yeyote , Mara nyingine huhitaji kuwa mtakatifu ili utumike yaani Bwana anakutumia vile vile  yaani unatumika haswa na Bwana anajitwalia utukufu................... Tena unajua nini mara nyingi anatutumia kina sie ambao tunajua kweli ila kuna vipengelea  tumejihalalishia,  na tunatumia nafasi hizo tulizonazo labda kuvuruga wale wadogo wanaoanza kukua kiroho waone ni kawaida........ mbaya zaidi km ni uko kwenye mamlaka fulani labda niseme nimchungaji kwa mfano ...... na kwa sababu Mungu anakutumia sana kwenye madhabahu  yaani ni ukitulia madhabahuni moto unaotoka pale ni hatariiiiii basi kupitia hicho alichoweka Mungu ndani yako, tumejikuta waumini tunakuamini sana sasa kumbuka tuliokaribu na wewe ndo tunajua mapungufu yako behind the scene binafsi huwa sioni km ni tatizo maana sisi sote hatujakamilika tatizo linapokuja ni pale sasa unapotaka kuhalalisha/kulazimisha yale mapungufu yako  sisi tuliowakaribu labda tukuunge mkono au tushirikiane na wewe kwa namna fulani........ labda niseme bodi ya kanisa imeona kabisa hilo pungufu halimpi Mungu utukufu na pia sio sheria iliyoweka ili ifuate (maana imeandika tiini mamlaka na sheria zilizowekwa) ni kapepo tuu kamejiingiza huko  na sisi wapendwa tulivyowanyenyekevu sasa na umepewa kanafasi kaushemasi basi lolote utakaloambiwa na huyo mchungaji utafanya tuuu...........

Naomba nieleweke sipo kumnyooshea kidole mtumishi yeyote yule............ nawaheshimu mnoo hasa kwa nafasi wanayoitumikia sio ya kila mtu aisee, binafsi huwa nasema ni nafasi ngumu kuliko zote ila km umepandwa kweli hujaingia kwa akili zako Bwana lazima akutetee........... tatizo langu ni hako kapepo sasa kanavyoambukiza .......

 Mara nyingine niliwahi kuwaza ili ukue kiroho labda uwe muumini wa kawaida tuu ujue kuingia na kutoka .......lakini, ni nani atakaye jenga nyumba ya Bwana??siamini km una utakuwa kiroho hapo. Maana ni bora uyajue hayo mapungufu na ukabiliane nayo ili ujipime kiwango chako na Mungu ujue ni kweli unamuamini Mungu anayemtumia huyo mchungaji au unamuamini mtu???

Kinachonipa tafakari zaidi mara nyingi watu wanaomzunguka mtumishi wa dizaini hiyo huwa ana nafasi zaidi kimwili na kiroho..... ninaposema kimwili nina maana ya kwamba labda kuna kahela fulani kakujikimu kanapatika, au labda kuna namna fulani kwenye safari yako ya maisha alisimama na wewe, na mengineyo na ninavyosema kiroho ni vile anavyotumika madhabahuni basi hii roho nayo inajiingiza kwa siri watu tunasahau kusudi...................mbaya zaidi hizi roho za dizaini hizi zikituingia tunajisahau kabisa.......... unaweza ukajikuta hata madhabahuni tunazileta kwa namna fulani hivi....... ngoja nikupe mfano 

Huku kwenye nchi za wenzetu vitu km boyfriend & girlfriend  vimehalalishwa hadi makanisani yaani watu wamezoana huko wanakuja wanashikana shikana na watu tunawabariki tuu...... hakuna cha  engagement  wala nini jana alikuwa peke yake leo amekuja na binti wanashikana shikana tuu  mbaya zaidi wanaweza wakakukalia mbele yako ili uwaone vizuri ha!ha!ha!  umekaa nyuma unasikiliza mahubiri watu mbele yako wanashikana shikana tuu mbaya zaidi utaambiwa watoto wa wachungaji sijui nini na nini..... kuna hiyo moja niliwahi kuishuhudia  nilikuwa kwenye ibada moja tuliambiwa tufurahi na hao watoto wamefanikisha mwaka mmoja pamoja  aiseekumbuka kuna waumini ambao walishindwa kuvumilia kwani wana watoto wa umri ambao walikuwa wanaona hayo wasingependa watoto wao waige na kwa sababu kanisa lilichukulia kawaidi baadhi ya waumini waliona bora wahame tuu (kondoo wa Bwana walipotea usitake kujua imani yao ilikuwaje baada ya hapo je hawakuona umuhimu tena wakubaki kwenye kusudi au??? Yes sad story after...... ........ lakini pia huhitaji kukurupuka tuu nakusema neno kuna hekima inatakiwa na kutubu kwa ajili ya kanisa........baada ya mda hao watoto wakaachana ha!ha!ha!  guess what nikaitwa kushiriki kuomba heee!!! kwa lipi sasa  jamani bora ungekuwa uchumba ningemuomba Mungu atusaidie macho ya rohoni tujue labda ule uchumba haukuwa kwa kusudi la Mungu sasa niombe uzinzi ???uliobarikiwa badala yakufurahia sasa pepo la uzinzi halitakuwa lina niblock mbele yangu nikiwa kanisani!!!! duu ikatokea sasa wameingia kwenye kumi nane zangu ikabidi niulize kwani nyie wezangu hili swala lote mnalichukuliaje?? tulielezana mengi ila jibu nililopewa mwisho  niliambiwa hivi, kuna wakati unatakiwa kujua km mwanao anapanda mlima  au hapandi ....upo hapo?? nikamjibu sasa kwa sisi waumini muongozo wetu uko wapi? si kwenye biblia? na biblia inasemaje juu ya hili?? .......................

Ninachotaka kusema ni hivi sasa kwa mfano huu utaona kabisa watu tuhalalisha vitu ambavyo sasa mwisho wa siku vinatuhamisha kwenye kusudi........ na kwa kusema hivi jamani nimetoka huko yaani wokovu wangu umenikuta tayari niko huko kwenye dimbwi la takataka thank God mara baada yakujua kweli juu ya hilo nilipanga mikakati mizito yakumshinda Shetani kwenye eneo hilo na nilimuona Mungu akinitetea. Sasa ninapoona mtu tayari anaijua kweli nakuhalalisha bila kuweka mikakati !!!!mbaya zaidi anataka na mimi nishiriki kwa namna moja ama nyingine duuu!! hapo ndo nahitaji kujua nafasi yangu iko wapi??? Ninachojua mimi wokovu wangu umegaramiwa aisee ........ sijiweki kwenye nafasi hii miaka kadhaa ijayo wanangu watakapo fika umri huu lakini ninachojua mimi kweli ndio wanayotakiwa kuijua  macho yangu hayakotayari kushuhudia na wala moyo wangu haupo tayari kubariki wao wamezaliwa kwenye kweli na kweli ndio itakayowaweka huru. haijalishi Mama yao neema ya wokovu ilinikuta wapi wanachotakiwa kujua wao wamezaliwa ndani ya wokovu na Mungu atawasaidia kuyashinda...... nakubariana na wewe kuna wakati inaweza tokea lakini jukumu langu ni nini??? kamsome Heri utanielewa nasema nini.............halafu mbona imeandikwa (Waebrania 10:26 Maana, tukiendelea kutenda dhambi makusudi baada ya kufahamu ukweli, hakuna dhabihu iwezayo kutolewa tena kwa ajili ya kuondoa dhambi.)


Wengi mtaniambia ni hekima kukaa kimya nakuangalia ,ngoja niwambie kajiupeo kangu kadogo kakusoma soma biblia namuona Yesu alipotakiwa kusema alisema, nikweli hakutaka kujiboost boost kujionesha yeye ni nani  ila alihakikisha kila alilolisema halibadilishi maana kama Yeye ni Mwana wa Mungu, namwangalia Daudi alijificha sana mbele ya macho ya Sauli lakini kila walipokutana uso kwa uso Daudi alimpiga la uso Sauli kwakumwambia ukweli.... Huyo huyo  Daudi kwani hujamsikia alimpiga neno mfilisti jitu kubwa??? Kwani Bwana alimuacha?? ha!ha!ha!  utaniambia Yohani kajifanya kampa ukweli mfalme mwisho wa siku kichwa chake kikakatwa Ha!Ha!Ha! unajua haikuwa rahisi kihivyo yaani Muda mrefu ulipita yaani mpaka hilo tendo likatendeka hapo kati Yohani aliendelea kupiga injili km kawa binafsi huwa nasema hivyo ndivyo ilivyoruhusiwa iwe ili mimi na wewe tujifunze kitu ni bora ufe kwa sababu ya kulitetea kusudu au uhame kusudi?? halafu unajua nini Muda wa kufa ni ule ule yaani..................

Tujiulize sasa nafasi zetu ziko wapi?? wewe ndo unajua ile kweli kwa jinsi na namna uliyookolewa je bado uko pale pale au kusudi limebadilishwa kwa siri bila kujijua labda leo Mama wawili nimekukumbusha??

 Kwakusema hivi nikiwa niko kwenye hili tafakari nimeingia mitandaoni nimeona kuna hii freedom of speech ndugu zangu mnataka kunyang'anywa nimeenda kuisoma hiyo bill ama sijui ndo sheria wapendwa kwa maoni yangu yaani hii kitu inatakiwa IREKEBISHWE  yaani imekaa kukukandamiza sana wewe uliyebarikiwa  sauti ila nafasi huna($$$ ze cheo huna,  ha!ha!ha! kumbuka wewe ni nchi na nchi ni wewe .... nimeshangaa sana nimepita kwa wapendwa wengi hatujasema lolote juu ya hili ..............  sijaelewa au ndo tumejifungia kuomba mavyumbani au???binafsi jamani km juzi kati hapo nilijikuta kabisa kuna haja kuwe kuna sheria mitandaoni........ lakini tena nilivyoipitia hivyo vipengele duu aisee marekebisho ni muhimu ama sivyo ibaki tuu kama ilivyokuwa maana huko ndo tunaenda kuharibu kabisaaa nazungumzia kimwili hapa ha!ha!ha!ha!huu ni mda wa kusema nini maoni yako ikishapita mpendwa hauna choice nilazima uifuate........Nyie haya mwenzenu nawasikilizia nikiona vipi fasta nabadili gamba from kijani to........ ha!ha!ha!ha!


Siwangalii usoni leo maana wengi wenu nimewavuruga ha!ha!ha! nawapenda lakini.





Wednesday, May 6, 2015

THE LOOK.......................


Juzi nimeingia mitandaoni hee nikakutana na rangi nyeupe kila kona duu nilivyoamka tuu akili ikawa inawaza nyeupe nyeupe tuuu hahahaaaa basi sasa nikatafutiza  ndo hivyo na mama wawili nikatokelezea ha!ha!ha!



Tunawapenda.............

Monday, May 4, 2015

CHANGAMOTO...........

Nyie bwana mkiona kimya ndugu zangu sa nyingine nagomewa mwenzenu kupigwa picha ha!ha!ha! kama hivi  mgomo ulipita nikaambiwa zamu yangu kuwapiga na ikitokea km ndo kuna mnuno basi mbona wanajua kwakunikomeshea ha!ha!ha! chezea kublogua nyie .................

binti yangu huyu  miezi sita ijayo eti anagonga 7yrs old mweee!!!!! Hizo zawadi sasa ninazoombwa eti simu!!! kweli???? anataka kuwasiliana na nani kwa mfano?? majangazi....... atasubiri mnooo kha!!! huu uzungu mbona balaaaaa.......

 she is cool hey???

my first love...............


Sifa na utukufu ni kwake yeye aliyetenda na anayeendelea kutenda peke yangu mimi ni sifuri............

 mwisho wa siku nilizomewa kihivyo yaani mgomo wao ulikamilika ha!ha!h!ha!

 Nawapenda mno wapendwa tuendelee kuichuchumilia taji kwa pamoja.........