Pages

Ads 468x60px

Friday, January 30, 2015

LA FAMILY..................................

Wapenzi wetu tuko mafichoni ya siku kadhaa ndio maana hamtuoni humu, tumalizia malizia  mikiki ya shule siinaanza tena wiki ijayo ...........


 ignore mapozi ya toto dogo yetu ha!ha!ha!ha!

sisi hapa


 ukiona mapozi ya malapa ujui ni maeneo ya maji na mchanga mwanzo mwisho.......

Haya tunawapenda

Wednesday, January 28, 2015

THE LOOK.....................


Huyu hapa nani eti????

kwenye maua hapakosekani nyuki ha!ha!ha! eebwana mwenzenu hii top ni suti nilivyoinunua niliipendaje sasa siku nimeaanda huo mtoko duu  nikabadili mawazo ha!ha!ha!ha! ngoja kwanza nijipange upya labda haikuwa sahihi kwa tukio sahihi ha!ha!ha! 





Mama wawili



Nawapenda

Tuesday, January 27, 2015

TEAM FITNESS..................


Haya mwenzenu nimerudi tena huku ki!ki!ki!ki! Ee bwana, hii kitu ukianza unabidi uwe unaendelea hata km mdogo mdogo ukizima kabisa ukirudi mwili unaumaaaa............... yaani mpaka siku ya pili hata kijiko kizito nakwambia ........Sijui ni mimi tuu au wote duuu!!

 mmeona nilivyomshamba wakujiselfie hi!hi!hi!

nimefunika sura picha zooote...........@ ushamba mzigo

Duu ila ukiingia humo ndani watu wanavyojituma mpaka raha yaani......

utajikuta tuu na wewe  uko busy km mnashindana ha1ha!ha!


yaani huu mwaka nimesema sikubali @list once a week lazima nijifit........potezea ile mikakati sijui nini na nini Imegoma aiseee!! yataka moyo na muda sasa  duu!!!mimi mkinga nawaza mabox mda wote kwa kweli imekuwa ngumu mnooo...... mdogo mdogo kiafya ndo mpango

Nawapenda

Thursday, January 22, 2015

THE LOOK.........

Aisee sijawahi kuwaza kama ni mpenzi wa pink, leo nimeanza kuangalia nguo aisee pink imetawala mnoo..... hivi unaweza ukawa mpenzi wa kitu bila wewe kujijua???Ha!ha!ha!ha! i think am official pink lady ki!ki!ki!ki! 



Duu jamani maombi yenu wandugu, dizaini nimeanza kuwaza kuvaa hivi monday to friday............ nikimaanisha no jezi za kuosha magari,mtoto kucha hazibanduki ni full kiyoyozi, nafanya kuita tuu ha!ha!ha!.............kwani siimeandikwa NITAKUINUA KIWANGO KIMOJA KWENDA KINGINE???  vipi sasa kwa nini tunaridhika??? kwa mfano, hivi haiwezekani nikawa na maproject kadhaa yaani mi kazi yangu kupitia tuu nakuchukua mahela????Tuache akili mgando ndugu zangu inawezekana??? narudia tena  Vitu kama hivi havisubiri muujiza vinahitaji utayari wa mtu............... tunajiwekea mipaka sana  ndugu zanguni....


Kumbuka una mamlaka na ndoto unayoota labda kuileta kwenye uhalisia au kuipoteza kabisa kwenye ulimwengu wako.


 UNA NDOTO GANI??



YANGU NI KUMILIKI,YANGU NIKUONGOZEKA,YANGU KUKATAA HISTORIA MAANA NIMEFANYIKA KUWA KIUMBE KIPYA, YANGU NIKUTIMIZA KUSUDI LILOWEKWA MBELE YANGU, MAANA HAKUNA SILAHA ITAKAYOINUKA KINYUME NA NENO LA MUNGU,..............................,......................,.....................,


INAWEZEKANA NA NITASHINDA HAIJALISHI SHETANI AMEJIPANGAJE MAANA NILIYENAYE AMEUSHINDA ULIMWENGU.

Nawapenda

Tuesday, January 20, 2015

HABARI YA MUJINI.................

Kwa mtonyo huu, lile swali la Mama wawili kiatu,sijui ni nani , haya sasa tumemaliza kihivyo yaani.................MIMA HUB ndo kijiwe chetu chakujidai .......... Utakutana na kina ALDO,NINE WEST,ZARA,STEVE MADDEN,CHARLES & KEITH,MICHAEL ANTONIO na wengineo .............. Nimefanya kukuonjesha tuu............fanya kukatiza basi  mitaa ya MIKOCHENI OPPOSITE NA MAZNAT BRIDAL SALON.  halafu unajua nini ???usishangae ukakutana na sura ya Mama wawili  moja ya siku Ha!ha!ha!ha!   


























TUNAKUPENDA MTEJA  WETU KARIBU...........

Friday, January 16, 2015

TAFAKARI..........................

Jamani leo niko kiupako zaidi ha!ha!ha! sijui kwa nini, hili neno nimekutana nalo kama wiki iliyopita kwenye muda wangu wakujisomea Biblia, lakini nimejikuta  mpaka sasa halinitoki nalitafakari , nalichambua,..........,....... duuu!!! mpaka nimeona labda yanipasa kukushirikisha na wewe......

Linapatika kwenye kitabu cha Luka 7


Baada ya Yesu kumaliza kusema haya
yote watu wakiwa wanamsikiliza, akaingia
Kapernaumu. 2Mtumishi wa jemadari mmoja wa
Kirumi, ambaye bwana wake alimthamini sana,
alikuwa mgonjwa sana karibu ya kufa.

 Nilitafakari kwa habari ya, 

Mahusiano kati ya hawa wawili nikajipa moyo inawezekana hata kama kwangu mwenyewe haijatokea basi nimeona kwa macho haya mahusiano  yaani nikimaanisha sio tu tunamabosi wazuri wa dizaini hii pia nimeshuhudia hata mahusiano haya kwa aliyekuwa nacho na asiyekuwa nacho.  Nafasi za watu hazikwezi kiasi kwamba zikapoteza ubinadamu. (Japo  bado tunahitaji wengi wa hivi)

nikaendelea mbele

3Jemadari huyo aliposikia habari za Yesu,
aliwatuma wazee wa Kiyahudi Kwake,
wakamwomba aje kumponya mtumishi wa huyo
jemadari. 4Wale wazee walipofika kwa Yesu,
wakamsihi sana amsaidie yule jemadari
wakisema, “Mtu huyu anastahili Wewe umfanyie
jambo hili, 5kwa sababu analipenda taifa letu
tena ametujengea sinagogi.” 6Hivyo Yesu
akaongozana nao,

 Nikajiuliza  kwanini amewatuma wazee???
Nikajipa majibu mwenyewe kwa tafsiri yangu  mara nyingi kwa mzee tunapata busara, hekima, na zaidi chumvi nyingi ha!ha!ha!
Hapo ndipo nilipoanza tafakari nyingine, je ????nimezunguka  na watu wa type gani?heshima yangu na thamani yangu imebebwa na watu gani? Je wamesimama na mimi? wanatambua mchango wangu ???japo mimi ni binadamu namapungufu yangu  je??? nikipi wanachokiona zaidi je nimapungufu au  kile kizuri???

Haya mdau wangu na wewe tafakari hii.......

 Duu!!! nikaendelea kidogo hapa ndipo paliponipa mawazo mnooo!!1 

 lakini alipokuwa hayuko mbali na nyumbani,
yule jemadari akatuma rafiki zake kumwambia
Yesu, “Bwana, usijisumbue kwani mimi sistahili
Wewe kuingia chini ya dari yangu. 7Ndiyo
maana sikujiona ninastahili hata kuja kwako.
Lakini sema neno tu, naye mtumishi wangu
atapona. 8Kwa kuwa mimi mwenyewe ni mtu
niliyewekwa chini ya mamlaka, nikiwa na askari
chini yangu. Nikimwambia huyu, ‘Nenda,’ yeye
huenda na huyu, ‘Njoo,’ yeye huja.
Nikimwambia mtumishi wangu, ‘Fanya hili,’ yeye
hufanya.”
Ngoja niwambie aisee.... humu ndani mwangu nina kajisebure huwa sikatumii sana,ni theater room kwa wale mtakaonielewa huwa nakatreat kidizaini fulani hivi special ha!ha!ha! hao wanenu wenyewe wakiingia wanakaa kwa adabu wanajua no messy otherwise mumy will be mad!! Sasa kwa sababu kichwani mwangu huwa naimagine kumualika mtumishi fulani mkubwa huko ha!ha!ha! yaani huwa napata picha na yeye amekaa  humo na mimi,ki!ki1ki!  Shemeji yangu naye mmoja aliwahi nitembelea akaniambia yaani shem!! duu unafikiri ukimualika Mh.K humu ndani atakubali kwenda kulala hotelini yaani atakaa hapa(in his voice)huku ananionyesha pozi atalokaa Ha!ha!ha!ha! ( mcheshi fulani halafu mwanasiasi basi wee)

Haya hizo porojo nataka nikulete huku niliendelea kutafakari kama ningekuwa mimi aiseee!!! zile ndoto sijui za mtumishi sijui Raisi hapo ndo ningejipindaje Yesu anakuja!!!! weee ningeita wapishi, wafanya usafi nahisi ningewalipa 24hrs,yaani ni full kujitanua na kile nilicho nauwezo nacho,  hiyo yote kumfanya Yesu afurahi.....Mpumbavu mimi bila kujua he is more than that, na mara nyingine hiyo nafasi inaweza kunikosesha, Vipi kama nisingejaliwa hivyo vyote?? Je nisingemkaribisha??? na kwa kusema hivi sijasema unapofikia kwenye suala la ufalme wa Mungu basi tusitumie mali zetu na vitu kama hivyo .......... Nenda kamsome mwanamke aliyempaka Yesu mafuta yathamani alipokuwa anakaribia kwenda kuteswa, watu walimshangaa?? Yesu aliwajibu nini???

Ninachotaka kusema ni kwamba inapofikia kwenye ufalme wa mbingu kuna vitu vinaambatana navyo,  kuna haja yakuomba neema ya Mungu ujue unakabiliana vipi, na hii pia ipo kwenye maombi, Kuna haja yakujua nafasi yako kama muuombaji iwaje???  Sikumbuki nikitabu gani ila kuna yule aliyesogea mbele za Bwana nakujinadi, oooh! mimi nimekufanyia hivi na vile, sijui nimetoa sadaka, nini na nini . na mwingine alichoweza nikujipigapiga nakukiri yeye ni mdhambi....(Wasomaji mnanielewa) hivi unafikiri huyu aliyekiri kuwa yeye ni mdhambi hakuwa na hata moja zuri ambalo angeweza kumwambia Mungu hata mimi nilikufanyia hili????

Tafakari!!!!


9Yesu aliposikia maneno haya alimshangaa
sana, akaugeukia ule umati wa watu uliokuwa
unamfuata, akawaambia, “Sijaona imani kubwa
namna hii hata katika Israeli.” 10Nao wale watu
waliokuwa wametumwa kwa Yesu waliporudi
nyumbani walimkuta yule mtumishi amepona.

Halafu unajua nini hayo yote alituma hakutaka kujitia kimbelele aonekane, mara sijui nini duuuu!!!! na muujiza wake akapata.

 kwa kweli nimeguswa na kila kitu hapa kuanzia ilivyoanza mpaka uponyaji ulipotendeka aisee!! nilijikuta mpaka chozi limenitoka na kikubwa nimejifunza kitu.......

 Haya mwenzangu uko wapi? nafasi yako iko wapi?


POLENI KWA GAZETI KAMA VIPI NISIPOST NEXT WEEK YOTE ILI MPATE MUDA WAKULISOMA ha!ha!ha!

Thursday, January 15, 2015

NIPOGO................

Hata mimi nawamiss mnoo......... ............

haya kamuonekano hako



Nawapenda


Wednesday, January 7, 2015

YOU GOTTA BE HUNGRY....................

Duu sema tu kiinglish kimehusika na Mama wawili kutafsiri ni shida, Jamani huyu mtu huwa ananibariki mnooo.............. Moja ya watu ambao nikiwasikiliza napata moto mnooo wakuendelea kufanya kile nnachofanya........ nimeona  niwashirikishe  na nyie duuu!!!

Tuesday, January 6, 2015

LA FAMILY................

Haya ndugu zangu habar mpya ni kwamba siku hizi naweza weza kucheza kwenye maji japo kuwa vikombe bado navimeza mnooo..........  Sasa kale kavazi kamtatindio wapendwa  nikiingia tuu kwenye maji mara kamenifunga miguu, mara kamepanda juu namwaga radhi  kwa ujumla hakafai kuingia nako kwenye maji ....... .......... (mwe nnavyojitea sasa kha!!! ha!ha!ha!)   Anyway dizaini hii ndo utanikuta nayo kama nimeamua kuingia kwenye maji....................

 Sasa basi Hawa penda maji wangu  wanapenda sana kubadilisha  viwanja vyakuogelea  swimming pool yao home naona imeota miiba, mara ooh!! twende kule ndo kuna vitu vingi, mara ooh!! nyumbani kunatuboa ha!ha!ha! haya basi ndo hivyo wakanibeba na mtu mzima Maskini naushamba wangu hata sijui sheria  zipoje??????

 legoooooo...... Kikazi zaidi 

Jamani wanangu huwa wanaenjoy wakimuona na Mama anaingia kwenye maji duuu!!! 

 Haya sasa  ndo tushatoka humo ndani kuogelea , kwanza marufuku kuonekana unachukua matukio hilo huwa nalijua.................  haya niulizeni mbona mimi mkavu wenzangu sura zao zinatetemeka na baridi????? EE Bwana sinimeambiwa siruhusiwi  kuogelewa na hiyo top sio yakuogelea........... hiyo ndo sheria yao ha!ha!ha! material yake hayaruhusiwi basi sasa ikabidi niwe msindikizaji..............




 Namapicha tukapiga

Tunawapendeni mnooooo..........

Sunday, January 4, 2015

THE LOOK...........


Nyie bwana sikilizeni, Mwenzenu sinikajifanya kubadilisha nywele hizo rangi!!!!! duuu niling'aje sasa???? nikaanza kujiona kama dancer wa Pepe kale(wazee wenzangu mtanielewa watoto wa K  sio rahisi kunielewa hapa Ha!Ha!ha!) anyway!!! ushamba mzigo duu!!  yakanishinda bwana, duu!!nikaanza kurushia rangi nyeusi  kufunika makali kidogo............ na hapa ndo nikaridhika ngoja kwanza nizoee hizo rangi mbili  then kuna siku ntajilipua ha!ha!ha!ha!

Eti Nke ya nani huyu????

 Baba wawili alizipitisha lakini duu sometimes kujiongeza mwenyewe kwenye kioo khaaa!!!

 habari njema ni hii am now 49.8kg........ ....  0.2 more kutoka kwenye danger zone.
Mama wawili



Spotted!!!



Unahisi nilikuwa na dance nini kwa mfano??? NDILIMGATI MWA YESU NDIKWINOMA, NDIKWINOMA..... NA YUVEVE WINGILE WINOME WINOME ( only in Iringa ha!ha!ha!ha!)

haya nawewe sijakutenga ni  maana yake......

NIPO NDANI YA YESU NINA RAHA NINA RAHA ....... NA WEWE MWENZANGU UJEGE BASI UFAIDI HII RAHA ha!ha!ha!ha!

 Love you wadau

Thursday, January 1, 2015

JIKONI NA MAMA WAWILI.............

Ahsante Mungu tumeuona wandugu........Sio kwamba tu bora kuliko waliotangulia bali ni kwa neema tuuu................Kaa mkao wa matarajio maana UTUKUFU WA PILI NI MKUU KULIKO ULE WA KWANZA...... Tegemea kuongezeka katika  kila eneo la maisha yako.Mwaka 2014 tulikuwa na mengi tuliyoyapitia,Tulianguka na kujikwaa, tulishindwa na kukata tamaa, Tulishindwa kuleta ndoto zetu kwenye uhalisia na mpaka sasa hatuna matumaini.Ninachotaka kukwambia TUMAINI LIPO.......Bwana hajakuacha wala kukupungukia, aliruhusu maana ndivyo ilivyotakiwa iwe katika kukuleta  pale alipo kukusudia. Kumbuka Mungu wetu anatuwazia yaliyo mema. kwa macho ya kibinadamu unaweza usilielewe ruhusu Roho mtakatifu akusaidie kuelewa..........Naongea kwa ushahidi wapenzi 2014 kuna jaribu moja nilipitia, kiukweli ndani ya wiki niliteseka sana, maana nilishindwa kumuelewa Mungu, Nakumbuka kujisemea kwa namna hii ntawezaje kumtia mtu moyo??? Duuu!!! Pale nilipotulia na kuruhusu utendaji wa kiroho aisee!!! nakumbuka nilikuwa naoga bafuni nilipewa jibu ambalo mpaka sasa huwa nalikumbuka nakuogopa jinsi Mungu anavyo Shughulika na maisha yetu .......... 

Bwana alivyotutoa kwenye lile eneo Wapendwa leo hii tunamshukuru Mungu mnooo kwa ajili ua lile jaribu!! Sijui niwaambiaje mnielewe wapenzi wangu kwa mfano!!!!!!! zaidi ninatubu kwa ajili ya ile wiki tuliojipa mawazo, nakujipa maumivu ambayo bwana tayari alikuwa kazini...................Ninachotaka kusema ni hivi, Unamamlaka yakufufua mifupa mikavu, Haijalishi umezungukwa na nini, na nani? acha kusumbukia kwa habari ya kibali maana hapo ndipo wengi tunashikwa na adui........ Tambua uliyenaye wewe ni mkuu kuliko wakuu woooote wa dunia.Wewe ni mshindi,Tena ni kichwa wala sio mkia,wanasema,........ MAJARIBU NI MTAJI....................HAPPY NEW YEAR


out of topic: Hahaaa! jamani hatuja panda mbegu mwaka huu  because tuna madeni mengi khaaa!!! ile mbegu iliyopita bado hatujamaliza deni ngoja tumalize kwanza ha!ha!ha!ha!

haya mwenzenu ndo sikuu yangu jikoni duuu!!! siku kama hizi unakumbuka majiko ya chini yakukaa halafu mabinti wamekuzunguka unaita tuu fulani niletee, fulani osha.... fulani njoo nisogezeee ha!ha!ha1ha!
 nimesimama leo mwanamke masaa karibu sita!!!!kiuno hakina kazi aiseee!!!

 ndo nimeanza hapo... ee bwana hilo dude linavalia kwa vile tuu nimeamua kuwa kikazi mara chache sana kuniona nalo ha!ha!ha!ha!

 hii nimewaletea tuu haina uhusiano na mapishi muone mmalizio wa mti na taa wanangu walivyoupamba.

hapo zimetoka Sambusa,Vitumbua,Egg chop na Sparkling fruit punch
Kuku lazima sikukuu eti???

Egg Chop  zimegoma kidogo muonekano lakini zimelikaje??

Chezea mother house weyeeeeee.......
 nilihisi left over zitabaki wiki nzima tunaangaika nazo mmmmh!!! leo siku ya pili naona sahani nyeupeeeee ha!ha!ha!


midomo inajieleza ha!ha!ha!

Mama tomboa a.k.a vitumbua ndo anavyoviita mwenyewe..........

mapozi ya ya kushiba hayo.......

my life........Thank God!
Furaha yao furaha yangu. Ahsante LAMOUR kwa kuwapendezesha wanangu go follow her @akailatailors.

Nawapendeni na nyinyi wooooote wadau wangu.

Mbarikiwe