Pages

Ads 468x60px

Thursday, August 28, 2014

TOTOZ DAY............

jamani hii kama week imepita  nimezipitia nikazipenda tuu, ukizingatia alhamisi!! yeah!!! TBT  ndo mpango..........

Niko na Dada wa mimi,shoga ake, makubwa, ................ majina yote yake aiseee. Halafu nyie simnajua kuna mahali huwa kuna watu wanatumika kwenye maisha yako? kuna wakati huwa wanajitambua na wakati hawajitambui. na ule uthamani wa lile tendo uliotendewe wewe ndo huwa unalijua kuliko yule aliyekutendea......... mara nyingi ni fumbo wakati linatendeka, huwa linatoa mapungufu yoteya kibinadamu  kiburi, jeuri, sifa ,...............na hapa ndipo huwa tunapata marafiki,ndugu katika bwana,.................. Pamoja na matokeo hayo yote mazuri yakumrudishia Mungu utukufu, Shetani naye huwa anaitumia hii nafasi inaweza kuzaa uadui mkubwa mnoooo..... ambao unatokana na labda yule aliyetumika ameanza kujiinua anataka kutukuzwa kwa lile alilotumika bila kujua haikuwa kwa akili zake,au labda yule aliyesaidiwa ameanza kujistukia nakutaka kujionesha kwamba sasa anaweza( hunibabaishi)............ kitu ambacho si vibaya ila tu ni ile namna anavyokiweka

HUYU DADA KANITOA MATONGOTONGO ULAYA, HUWA NAMSHUKURU MUNGU MNOOO KWA ILE NAFASI ALIYOTUMIKA AISEEEE!!!! 

Samahani mwee simnanijua nikianza kuweka mafeeling nini siwezi kujizuia ???? haya tuendeleee

tulienda zoo kushangaa wanyama

watu wanavyomchukuza huyo mjomba  mmmh!!!

 huyu jamaa nahisi alikuwa anatutamani alivyokuwa anahangaika nilihisi atabomoa kioo



full kushangaa uumbaji wa Mungu
washamba wengi eeeh!!!


Jolamu ndo nini bwana hebu toa upako hapo you never know tunaweza kushawshika kupiga no. 3 kwi! kwi! kwi!


sisi hapa
]
nyie kumbe kuna makobe makubwaa hivi

the team



nimechoka wandugu inatosha eeeh!!!

Tuesday, August 26, 2014

MAMA WAWILI.........

Wahehe tunaita mnyela mumo........ sijui wenzetu mnaitaje??? mbaya ujikute uko kwenye choo cha foleni ukitoka watu watakuwa wamenunaje??? maana kuitoa kama unaingia kuoga vile..... ... ama kweli fashion gharama eti eeh!!!

Nimemkumbuka na Mama yangu angechekaje sasa kuniona na hili vazi na hicho kitambaa chake kilivyo mtepete simpatii picha.....
last weekend kiua mpaka kilitubu simnanijua nikiifumania style???

Mama yao anawapenda munoooo......

Monday, August 25, 2014

MAMA NA MWANA..................

Church look , sikujua kama na mwanangu kidogo tumematch mpaka mwenyewe niko kwenye Gari nasikia anamwambia Dada yake mimi na Mama leo tumevaa sare ndo ile kustuka kajicolour na material ya top yake somehow tumematch Kwi!Kwi!kwi! aisee kila aliyempa dakika kadhaa moja ya maongezi ilikuwa ni hiyo....................
Nyie kila mtoto ana historia yake aisee haka kakwangu kamenifundisha Umama ugenini mweeee!!!!! (wale mlionilelea Careen kama nawaona vile mnavyocheka huko maana hata kumpa chupa mtoto nilikuwa sijui mweee!!!) nasema hivi ngoma ya tatu nahisi mtanipokea tuuuu!!!
Priceless..........
kaone kwanza Sina chakumrudishia Mungu aiseee kwa Wawili wangu mweeee!!! ni kwa NEEMA!!!

Wednesday, August 20, 2014

CONGRATULATIONS MR &MRS R.MUSTAFA..........

Wandugu Camera ya Mama wawili ilivamia tuu, haikualikwa  si mnajua huwa haiwezi kutulia??? Angalia matukio iliyofanikiwa kuyapata..........

 Kwa ujumla Shughuli ilinoga mnooooooo 

Sasa wanaitwa Mr & Mrs R.Mustafa...... Duuuuu!!! nimefurahije sasa?? yaani nahisi nilikuwa nawakera maana, kila nikikutana nao wakinipa dakika kadhaa  za maongezi lazima niwapige swali MNASUBIRI NINI??? Hatimaye yamekuwa........

Wifi yetu sie,Muke ya Barrick........alifunika aisee!!!
Mr & Mrs Mjema
Dad yake nani?? na Shemeji yake nani??
haya nyie full kudekezana....(Mr & Mrs Hassan)

Mr & Mrs H.Chaburuma
napita kimya kimya kuna shemeji pembeni


Hapo chacha !!! Ni Mr&Mrs ..........

Boss wangu unadeka eeeh!!!

waone kwanza (nawapendaaaaa)

ni sheeder!!!!


 The Majige's...........

hawa hapa chacha nawasubirije???Kwi!kwi!kwi!(mnanielewa eti eeh??)

umenoga jamani

friends

Esther &Georgina

Sarah & Ummy

Ummy & Neema

ni spotted au pozi kweli ?? mmependa mnooo!!

Dogo letu sie akiwa na Madada zake (karembo eeeh)
The woman behind the Camera akiwa na Baba watoto

Monday, August 18, 2014

TUPOGO...............

Ukiona hivi ujue tushavamia miji ya wenyewe

nani hawa????

sisi hapa.....

Haya endelea kunichungulia kujua kulikoni.........