Pages

Ads 468x60px

Wednesday, July 30, 2014

MAMA WAWILI

Ishawahi kukukuta umealikwa kwenye ka event, kama bby shower, mwenyewe umejiandaa kipink pink (nimekariri kwa sababu ninao mabinti tu) masaa machache unagundua ni bby boy na closet haina colour ya kibby boy na kama ipo hali ya hewa imegoma kukuruhusu kuvaa hiyo nguo???

 ndo yaliyonikuta mwenzenu, huo mchomekeo wa kibibi bibi ndo ulikuwa only option na hiyo skirt ndo kidogo ilikuwa imepoa katika zoooote ili iendane na kishughuli kwi! kwi! kwi!


bora kuliko ningevamia kipink pink siningefukuzwa???
ready to go......
naringaje sasa????
penda nyie mnoooo

Monday, July 28, 2014

MAMA WAWILI


Mimi hapa......



muke ya Slay

spotted


Nawapenda mnooooooo!!!!

Friday, July 25, 2014

NIMEGUSWA........


Wednesday, July 23, 2014

TUZUNGUMZE.........


  Kwa wale wadau wangu mnaonifuatilia, kama mtakumbuka niliwahi kuzungumzia, jinsi gani nilivyoteseka miaka kadhaa iliyopita kwa habari ya  wanadam fulani fulani, Ambao baadae niliweza kulielezea kwamba wakati niko kwenye mapito hayo nilidhani tatizo ni wanadamu hao kumbe tatizo ni mimi mwenyewe. 
Nikasema ,Binadam tonatofautiana sana kitu ambacho mimi kipindi hicho sikuweza kuiruhusu akili yangu iamini hivyo., Labda kwa ajili ya makuzi niliyokulia, mazingira niliyoishi na vitu kama hivyo.........

 Ngoja nikupe mfano, niliwahi kuamini unaposema huyu ni ndugu nilitegemea mengi, kuliko, isivyo kwa ndugu. Na kumbe!!!!kunauwezekano mkubwa asiye ndugu akakufaa kuliko ndugu. Neno ndugu kwangu lilimaanisha kabila,taifa,ukoo n.k yaani nilipokuwa na deal na taifa mbalimbali nilitegemea zaidi kwa Mtanzania mwenzangu kuliko kwa mtaifa mwingine, nilipodeal na Mtanzania,nilitegemea zaidi kutoka kwa ndugu  wa damu kuliko kwa rafiki au jirani au mtanzania yeyote yule ..................... Nafikiri mnanielewa, na kwa kusema hivi naomba nieleweke  sijasema NI KOSA endelea kunisoma chini utanielewa.

Nasikitika kusema kwamba kwa kipindi fulani matarajio yangu hayakuwa hivyo, Mbaya zaidi nilikuwa mwepesi sana wa kulia (maumivu yake usiombeeee).Nililazimisha sana kumbadilisha mwanadamu, nilitegemea mzigo ninao ubeba mimi juu ya ndugu yangu(rejea maana yangu ya ndugu) nilitegemea na yeye atabeba kwa uzito, na kama ni maumivu na yeye ataumia vile vile .......... 

Wandugu hii ilinitesa sana nakumbuka kama nimaombi nilioooombaaaa ,mpaka, nilianza kuamini kuna maombi mengine Mungu hana uwezo nayo maana kila nilipoomba ili kudumisha yale mahusiano ndo kwanza nilikuwa naharibu, Nilitumia akili zangu sana mpaka nikaanza kuishi maisha yakuigiza ili tu niweke mambo sawa.Ndio kwanza niliharibu. Nilijikuta naishi maisha yakinyonge ndani ya moyo wangu, kwani maisha yangu binafsi yalikuwa hayana tatizo lakini ilipofika kwa jamii haikuwa kivile.

 Siku isiyokuwa na jina akili ilinijia, sijui ilikuwaje (ni Neema) nikajikuta nawaza, tatizo sio jamii tatizo ni mimi. Nategemea zaidi kwa wanadamu kuliko kuwa na kiasi. Nikajikuta  najisemea MAANA YA UNDUGU ninayoijua ni KWELI  ila kuna namna inipasayo kudeal nayo...............Ilinibidi nifanye maamuzi, Haikuwa rahisi  aisee ee!!!!! Nilijikuta nimeanza kuvaa vazi fulani ambalo kwanza sikutaka kunibadilisha uhalisia wangu. Ningeweza kukueleza mengi hapa ila baadhi mnanielewa hasa wadau wa siku nyingi.

Kuna kipindi sasa baada ya kukubali hilo vazi nilianza tena kujitathimini nilihisi kabisa huu sio mpango wa Mungu, maana nilijiona ile nafasi ya unyenyekevu,kupondeka imetoweka, yaani sinayo tena!!! zaidi nilijikuta mtu wa ujasiri mwingi, nilijiona niko proud sanaa LAKINI  kila nilipojitathimini nilisikia  sauti ikiniambia (unyenyekevu,kupondeka haimaanishi hali ya unyonge na kukupa maumivu bali, ni namna fulani ya hekima ambayo mwisho wa siku inakupa amani nakutokujutia. 

 KWA NINI LEO NIMEKUMBUKA HILI

 Juzi kati kama kawaida yangu napitia madeni  nikajikuta kuna $550 nilikasahau  kama miezi miwili hivi, ila kwa sababu mteja mwenyewe ni the big boss, nikajua sio shida hata yeye amesahau ngoja nimkumbushe. Nikanyanyua simu nampigia duu!!!! jamaa naona kichwa hakikuwa sawa, aisee alipa ma f words yakutoshaaa!!!!! yaani nikabaki nashangaa kwenye simu nilichoambulia ni kimoja tuu kwa nini namdai wakati ameshanilipa??? nilimkatia simu, nikaanza kuwaza hivi  amepata ujasiri upi kunifanyia hivi kwenye simu yakiofisi?? kwa nini anitukane hata kama pesa kaweka, kuna mengi yaliendela hapo huwezi amini. Nikajikuta kwanza nimekaa namwambia Mungu sitaki kukumbuka kilichotokea, ila haki yangu naipataje? 

Kilichofuatia ndicho kilichonikumbusha  hayo yote.

Nilijikuta nimelia tena!!!  jinsi nilivyokuwa najiskia enzi zile ile hali ilinirudia tena wapendwa.............Jamani nililia kama mtoto. 

Haikupita nusu saa nikajikuta natoka nje ya ofisi huku nikiwa nawaza yaliyonitokea, Mbele yangu nikamkuta mwanamke ninayemjua ameshika bunch of flowers anakuja. Namjua kama ni mfanyabiashara na pia huwa namuona kanisani, zaidi ya hapo sina ukaribu nae wowote. na kwa sababu hapo zipo kama ofisi tatu nikajua amepotea anaenda kwenye moja ya ofisi. Hivyo nimekaa mkao wakuulizwa swali kwa habari ya ofisi anayoitafuta. Sikuwahi kuwaza kama hata anajua ofisi yangu ipo hapo. japo moyo wangu unamawazo nilianza kuuandaa ili mawazo yangu yasimuhusu mgeni ( rejea nilipojifunza kujitegemea bila kutegemea akili ya mtu mwingine  (TUWE NA KIASI CHA MATARAJIO)

Mara nikamsikia akiniambia huku akinipatia lile UA  akisema, nilikuwa nafanya shopping mara nikasikia moyoni ninunue ua nije nikutie moyo,  kuna sifa nyingi hapo alinimwagia akili yangu ikawa bado hailewi!!!!!! nilijikuta natoa chozi  aisee, kati ya watu ambao hawaelewagi thamani ya maua  mimi ni namba moja !!!!!!!kwanza huwa naona wananichanganya tuu, mtu akinilitea UA, Lakini Ua hili liliniletea maana kubwa, Binafsi mimi niliamini Mungu kamtuma maana alikuja kwa muda sahihi( Wapendwa mnanielewa hapa) lakini kilichonishangaza  ni zile sifa ambazo kwanza sikuwahi kujua mtu kama yeye anaviona ndani yangu,Pili sikuwaza kama vinaonekana hivyo kwa wanadam zaidi ya familia yangu, Na vingine,hapo kale  ndivyo nilivyokuwa nahitaji labda mwanadam aelewe lakini mapokeo yake  yalinijeruhi, ki ukweli!!!!chozi langu lilijiuliza  meeeengi!!! Ilibidi nifunguke maana naona hakunielewa kwa nini nalia vile. Aiseee kwa sababu ni mfanya biashara wa siku nyingi alinipa experience zake nikajikuta mbona langu cha mtoto???? Nilipata faraja mnooooo.!!!!

Nilichotaka tujikumbushe na tujifunze kuna kitu unaweza ukawa unakipitia ukadhani ndivyo kinavyotakiwa kiwe kumbe sivyo, mara nyingi jaribu kujiangalia mwenyewe ujue ni namna gani unaweza kujitoa (hekima itumike) bila kupoteza uhalisia. Mara nyingi Shetani huwa anatumia kile cha thamani ulichonacho kwa namna nyingine.

Guess what??? 

Baada ya hayo Tuligundua The boss aliweka pesa kwenye account ya mtu, na huyo mtu kajichunisha akidhani muujiza (kwi! kwi! Kwi!) The boss mwenyewe, alihakikisha pesa imeingizwa tena kwenye bank account yangu, Jamani hakusema samahani ila kule kushuka alivyoshuka na kujieleza kwenye simu. kwangu ilitosha nanilimshangaa sana Mungu kwa hilo .

Halafu unajua nini liliruhusiwa kwa sababu eti eeh??? na cha mwisho kikubwa wale ndugu,jamii,rafiki nimejikuta mahusiano yapo,tunapendana na kuheshimiana (niaminivyo mimi). kwani kwa sasa nahisi i expect only less or non!! na ninathamini na kuheshimu vyovyote itakavyo kuwa maana Wanadamu Tunatofautiana.

Duuu!! nimeridhika sasa maana hata leo nilitaka niwachunie ila hayo masumbuko ya moyoni nisinge lala.

Nawapenda

Monday, July 21, 2014

WITH MY BEST FRIEND................

You all know Am married to my best friend si eti eeh!!!! halafu niwambie kitu lkuna muda tunazinguana mnoooooooo!!! kawaida sana coz we are not fake to each other na niwatu wawili ambao no matter what hamuwezi kuwa sawa 100%  lakini mwisho wa siku we all admit hakunaga........(NI KWA NEEMA!!!)
 Baba na Mama wa my wawili............



tumo na sisi kwa mapozi kwi! kwi! kwi! kweli uzee mawazo mwee!!


spotted!!


aliyetupiga picha ana walakini mmeona eeeh!!

Jamani mwenzenu ubusy!!! nimeona nipite tuu ni wambie nawapenda mnoooo

Wednesday, July 16, 2014

MAMA WAWILI

Nipogo wandugu.......

 Huu unyayo bwana wa mwenyewe CL(ukibisha  ntakuletea risit ujue???ha! ha! ha!) halafu ndo sijamvaa ki hivyo hebu angalia sasa alivyoanza kunikataa ,anakunjika hapo mbele halafu ameanza kuniumiza fulani hapo kwenye mkunjo  sasa sijui ndo guu la muosha magari limekomaa au na wenyewe siku zingine wanatufekilisha?? au nimekariri jina kubwa haongopi?? wenye $$$ za mawazo utatujua tuu kwi! kwi! kwi!
a.k.a Rose wa mbeyela
NAWAPENDA MNOOOO

Monday, July 14, 2014

ULOKOLE NA MAMA WAWILI..................


 Haya wandugu ngoja nifunguke kwa haka kaji ufahamu nilikonako kwa habari ya nini maana ya ulokole .

Nijuavyo mimi mlokole ni Binadam kama alivyo binadamu yeyote aliyepo dunia.................. moja ya sifa inayomtofautisha na mwanadamu mwingine yeye anaamini NENO LA MUNGU, KWELI nikimaanisha BIBLIA. na hiyo haina ubishi BIBLIA imebeba maandiko matakatifu ya MUNGU.Kama hukubali hili kuendelea kunisoma huku chini unapoteza muda.

 Kama umekubaliana na mimi hapo , basi nielewe kuwa Mlokole ni mtoto mzuri, mtoto mzuri siku zote ana muongozo, pamoja na kwamba hapakosekani makosa ambayo kwa namna moja ama nyingine makosa hayo yanamsaidia kukua na kukomaa zaidi, kutambua lipi lililo jema na lipi baya. Na ndio maana imeandika TUKISEMA HATUNA DHAMBI KWELI HAIPO NDANI YETU...............Lakini, hili neno halimpi msamaha wakufanya dhambi za kukusudia..Niongeze kwa kusema Ulokole  ni mtu na uhalisia wake (BE YOURSELF) Usifanye kama kilemba chakufichia maovu maana siku ya umbuko lako inakuja........... ni bora ukaonyesha uhalisia wako ili uweze kukosolewa..........Asikwambie mtu ulokole pia una hatua za ukuaji , unatoka kwenye utufu kwenda kwenye utukufu zaidi..............Sifa moja ambayo huwa naipenda Mtu akinishangaa!!!! kwa kuniuliza hivi kweli Rose ndo wewe???!!!!! Sikutegemea kama Rose wewe wa miaka ile utaniambia Hivi, halafu unaambiwa kwa mazingira ambayo hujategemea....... yaani huna wazo kama kuna kilemba cha ulokole, lakini ndani yako una ufaham wa muongozo yaani we unafanya tuuu.............na hata anapokwambia hata wewe unastuka nakuanza kukumbuka miaka ile ilivyokuwa , Nielewe kuna vitu ambavyo Bado nilifanya nikiwa ndani ya ulokole ambavyo labda havikutoa picha kamili ya ulokole  lakini nilichotambua ni kwamba ulokole  sio kuwa fake,  Na leo hii ndo maana umekuwa shahidi kile ulichoshudia nilikifanya hata sasa sifanyi tena kwa maana niliingia mimi kama mimi nakuruhusu Neema ya kunitengeneza na kuniponda ponda ili niwe hivi nilivyo leo.................Inawezekana kabisa  bado niko kwenye kunolewa, safari ndo kwanza inaanza lakini, nina kila sababu yakumshukuru Mungu  kwa hapa nilipo, SIFA ZIMRUDIE YEYE ALINIWEZESHA.

Utaniambia kila mzazi ana muongozo wake hivyo na malezi yanatofautiana.... Sawa kwani siumekubaliana na mimi hapo juu???? BIBLIA inatuambia MUNGU NI BABA WA BABA  kwa mlokole huyo ndio mzazi wake na Muongozo unaanza hapa.................

Usiwe na miungu mingine ila mimi.

                        Usijifanyie sanamu ya kuchonga.

Usilitaje bure jina la BWANA, Mungu wako.

Ikumbuke siku ya Sabato uitakase.

Waheshimu baba yako na mama yako

Usiue

Usizini

Usiibe.

 Usimshuhudie jirani yako uongo.

Usitamani…cho chote alicho nacho jirani yako.


Nielewavyo mimi huo muongozo hapo juu, mlolole yeyote wa kweli sio kilemba atakayejikuta amefanya lazima kutakuwa namaandalizi...... yaani kuna nafasi ambayo huwa inakupa muda wa kujiuliza ufanye au usifanye ........ Mlokole kweli naweza sema asilimia 90 itampa masumbuko ya moyo kabla yakufanya hilo tendo...........Masumbuko hayo hayatampa amani yakuyafanya hilo tendo na hata kama ikitokea amefanya mara baada ya tendo  roho ya toba humjia na wakati mwingine huwa anajikuta alichokifanya hakiwezi kusameheka, ana kuwa na moyo wakugua  mno, hawezi kuchukulia kawaida hata kidogo na hainaga marudio marudio hiyo ukiona  kuna marudio  marudio hata masukumbuko ya toba hayapo MMMMMH!!! kuna shida somewhere aisee. ukitaka kunielewa Msome Yuda msaliti unahisi kwa nini aliishia kujinyonga??? japo andiko lilitakiwa kutimia??? Acha turinge leo maana yote yalimalizwa msalabani !!!!!!!!Damu iliyomwagika pale msalabani ni ondoleo la dhambi zetu kama tukirudi  kwa moyo wakuugua na kupondeka vinginevyo tungekuwa tushaji Yuda sana tuuuuu!!!!( Ni shiida!!!)

Mlokole huyu sasa ambaye yuko sawa hapo juu, kama msomaje kasome Habari ya yule Tajiri aliyesema hayo yote nimeshayafanya tangu utoto wangu(Luka 18:18..............

  Unaweza kufanya yote lakini tuna mapungufu,Kuna vimapungufu vya papo kwa papo, yaani shetani analetaga tuu, labda kwa sababu ya mazingira tuliyonayo, au nafasi tulizo nazo, au vyovyote vile.........Yawezekana yule Tajiri angepewa muda angeweza kuwaza hivi,  huyu Mtu anayeniambia ndie mtoaji mwenyewe hivyo hata nisivyofanya atakavyo akitaka kuchukua atachukua tuu,Au labda angevuta picha ya Ayubu basi eeeh!!!( haya ni mawazo ya Mama Wawili),
 lakini iliruhusiwa iwe kama ilivyo ili tuwe na moyo wa unyenyekevu, japo kuwa wengi wamelelewa ndani ya muongozo ambao labda umekuwa kama sheria Ukisoma zaidi utakuta hata wanafunzi wameshtuka fulani (Ni nani basi awezaye kuokoka???? Yasiyowezekana kwa mwanadam...........)

Ninachosikitika ni kwamba kipengele hichi, Wengi wanatumia kama njia yakuwakatisha tamaa,Shetani huwa anatumia sana kupiga upofu watu nakuwanyima ufahamu kupitia kipengele hichi,kipengele hichi kimetoa sura tofauti ya ulokole labda niseme kwa sababu tumejipa unyonge sanaaaaa, nakushindwa kuelewesha .Lakini, mwisho wa siku ndugu naomba tuu uelewe Tatizo sio ulokole wangu ila kwa sababu umekaririshwa kwa habari ya ulokole na kupigwa upofu usione , usisome, wala usitambue sio rahisi ukanielewa..................Na kwakusema hivi Basi, sijasema kila anachofanya mlokole kiko sawa No! no! no! Tatizo ni vile wewe unavyokichukilia na kukitolea Hukumu.( Walokole wanafiki nyieeeeee!! Eti si ndio mnavyosemaga???Shushu kaimba Thamani ya ulokole wake anayejua muumba kama fake au sio  acha vijisababu endelea kutengeneza na Mungu wako..... hivi unajua wokovu ni wa mtu binafsi???? tutakusaidia kukuongoza toba ya kukiri na kukupa misingi ya neno la Mungu mwisho wa siku ni wewe na Mungu.)

Nikiendelea kusisitiza kwa habari ya huyu Mlokole Mimi na wewe tutakubaliana wanadamu tunatofautiana kuna wacheza sinema,wakulima,wafalme,mafashonista,......... yaani hizo zote ni nafasi za mtu ndivyo alivyo mlokole.Wengi tumekariri tunategemea kumuona mlokole masikini  (wa mali),hana hadhi,yaani hafanyi ilivyo kawaida zaidi ya unyonge...... Sikiliza nikwambie Tumeambiwa Tutakuwa vichwa na wala sio mikia, Tutaketishwa na wakuu, maana Bwana Atatupa kibali, ukisoma Biblia yako, utakutana na wafalme pia waliongoza kwa hekima, yaani kila nafasi iliyopo duniani iliyo halali ni haki ya mlokole kikubwa ni kwamba hiyo ndio nafasi uliyoruhusiwa kuwepo na mara nyingi huwa inakupa amani badala yakutafuta kuhurumiwa au kutukuzwa. (Naweza nisieleweke hapa Aliyekusudiwa atanielewa)

Na Mwisho naomba niseme hivi unaweza ukasema kama ni hivyo, basi wewe ni mtoto mzuri kwa maana upo kwenye kila kipengele hapo juu isipokuwa hujiiti mlokole ngoja ni kwambie

Tofauti ambayo ndo inakamilisha yooote hapo juu ni KUKIRI KUWA YESU NI MWOKOZI WA MAISHA YAKO KWA AKILI ZAKO TIMAMU  NA YEYE NDIO TUMAINI PEKEE.

kwani siumekubaliana na mimi unaamini maandiko, sasa maandiko hayo hayo siyamesema mtu haji kwa Baba kama hajapitia.......... ???????Na aminie na kubatizwa ...................????????? Na mtu akinikana mbele za watu ...........???? sasa unaogopa nini kumkiri?????? We ingia tuu mzima mzima bila kuwaza itakuwaje??? na ukubali kutengenezwa bila mipaka mambo mengi mwachie mwenyewe....Ha!Ha!Ha! nimekumbuka enzi hizo na Baba wawili Wangu Mweee!!!! Baada yakusahau mlango wa Kanisa kwa miaka miiingi!!!!hata hivyo  nilikuwa naenda kwa sheria, sasa basi!!! ile Siku Mungu alivyoamua kunivuruga  sasa duu!!!!! kwanza alinisahaulisha kama kuna Baba wawili ( enzi hizo Suleiman a.k.a Slay) Mara Baada ya kukiri ndo nikaanza kukumbuka sasa itakuwaje????? Halafu sasa ndo tulikuwa ndo malove yamechanganya mnoooo...... hatusikii wala kuambiwa Ha! ha! ha! mweeeeee!!!!! alikuwa kasafiri jioni Simu ya malove love lazima ipigwe kwi! kwi! kwi! unahisi niliipokeaje???? au ilikuwa wewe pepo kwa jiiiiina la Yesu toooooooka!!!!Nyie bwana acheni Mungu aitwe Mungu!!!!!Leo tupo hapa tulipo aisee acha niseme ni Neema!!!!!!!  ninaushahidi ujue???aiseee duuuu!!! we endelea kuniona chizi hivyo hivyo sauli sako, hiso ni sambi sako mwenyewe(in hehe accent)

halafu unajua nini laiti watu tungelijua safari ya ulokole is a sweetest journey ever!!!!!! haicomplicate aiseee,Lolote linalokupata unajua nina Tumaini yaani nina Baba wa MaBaba, Mshindi  wa Yote.HAKUNAGA KAMA YEYE

 Nyie ujue sipendi maswali??? ndo mi nishakupa nilichonacho.............. hivi tungekuwa tunaruhusu maswali madhabauni ingekuwaje kwi! kwi! kwi! ( joke)
 na mnikome hilo gazeti mmeliomba wenyeweeeeeee























Wednesday, July 9, 2014



Haya wandugu wiki hii tutazungumzia ULOKOLE na Mama wawili anavyouelewa.........  hii ni kutokana na wengi mmenitaka nifanye hivyo japo namawazo kidogo.... ni kweli na ruhusiwa kuuzungumzia?? mapokeo yake yatajenga au kubomoa??  nitawezaje kulileta likapokelewa kama vile linavyotakiwa kupokelewa???  

Kazi kwenu wana maombi piga upofu kwa yule asiekusudiwa,zibua masikio ya rohoni kwa aliyekusudiwa apate kuelewa............. zaidi ikalete ufahamu ndani yao.

Tusindikizwe na wimbo huu



Tuesday, July 8, 2014

CONFERENCE 2014

Haya wapendwa wangu wa pande hizo hii siyakukosa!!!! Namkubali sana huyu Mtumishi .............yaani ni one of my best huwa napenda sana anavyonipa neno na kunirudisha jinsi gani linaendana na maisha............. wanaomjua mtakubaliana na mimi.



Monday, July 7, 2014

MUONEKANO................

 Mpo poua eeeeh wapenzi wangu???? Mimi mwenzenu mambo mengi mnooo kichwani, si mnajua mwisho wa mwaka wa mahesabu tayari ????? paper work kibao mweeee... ninachomshukuru Mungu ninafanya huku naenjoy, yaani i love everything!!!! kujifunza kwingi,makosa ndo usiseme nahisi leo nimemkera hadi accountant wangu  kwi! kwi! kwi! ye anataka ajifanyie kazi yake kwa nafasi, mi nimekaza nataka kumsaidia ili nijifunze hata kama ananichaji same amount.......... hizo simu nilizompigia leo nahisi alikuwa akiona namba yangu anatamani kunikatia ha! ha! ha! ha!

Kitu kingine kilichonichanganya nilikuwa sijaanda group certificate za wafanyakazi, mwisho wa wiki jana  nilipigiwa simu karibu nne wote wanataka certificate zao ili waclaim tax, weee walinipanikishaje!!! nikajua nimechelewesha na ushamba wangu....... ninavyoiogopa hii serikali mmmmh!!! nikahisi ntakuja kufungiwa biashara kwakutowatendea wafanyakazi haki yao, Leo nimeongea na accountant kanitiaje moyo........ kumbe kisheria bado nina karibu mwezi mzima kuziandaa, japo i know kuna watu wameninunia huko hatari............... 


PATA MUONEKANO

 Aliniambia anataka kunifundisha mapozi haya ndo nafundishwa hapo........
Muonekano huu ulikuwa unaelekea play ground kulikuwa nakajishughuli fulani................ (happy moment)
 Muke wa nani huyu????
 hizi kajagio ninazo km nne sasa huwa namkumbuka sana marehemu Bibi yangu nikivivaa, alikuwa navyo vyakidizani,alikuwa mfupi fulani plus matege anavyotembea sasa utampendaje????RIP my Bibi wa mimi Mama wa Mama yangu......
Heading...........

Thursday, July 3, 2014

NIGHT OUT............

I Thank God for you ladies, You just don't know ,how much you add in my life ............ I know! sometimes am crazy........ kwi! kwi! kwi!  but, you still love me as i am......( I love you Rose Mbeyela,  i see God working in you in your craziest style.......................... in ma mfundisi voice)  to me working in you means,  Am not perfect, my today's spiritual life is not same as yesterday and I still need to draw closer, and closer, and closer ......... Wow! you are so Truly to me, that is all i need........... 

 What a blessing??????

 As for you all, who we Hang out most of the time,I just wanna say i love you all and Thank you...............its only  that, i had to pick one group from my big Camera and this is what i found!!!

By saying that please allow me to gossip with my people back home (kwi! kwi! kwi! swahili dictionary to English is available on google) 

 Haya Wandugu, mwenzenu nimetoka kwenye kikao fulani  fulani.......  yaani kila mwezi ninavikao na watu tofauti tofauti, sio vyakubeba mabox it is about good time and share.............nimejikuta namtukuza Mungu sana kwa jinsi alivyonipa watu wa dizaini tofauti tofauti na jinsi wanavyotumika kwa ajili ya maisha yangu aisee..... kikao cha leo hakikuwa cha hawa mnaowaona....... baada ya mawazo haya nimeona nije nimtukuze Mungu kwa kutafuta picha za one of my groups, kumwambia Mungu ahsante!!!!! Wanadam tunahitajiana aiseee, inategemeana lakini, usijekurupuka maana hata shetani anakuhitaji!!! Cha kweli kinakuja na amani na utulivu, hutumii nguvu zako nyingiiii ila ni kitu ambacho you cant wait maana unaamini kila kinapotokea unajengeka. Kama hii ya leo nasikitika tutachukua break kwa muda kidogo maana baadhi wanaenda holiday. Ninachotaka kuwatia moyo msifikiri Duniani kuwa watu wabaya tuuu, aise God has people bwana duuu!!!!  na anawatumia vizuri sana katika kujenga ufalme wake............sijui nikwambiaje ntarudi tena katika hili kwa namna nyingine kama Mungu atatupa kibali yakulizungumzia..................

Hii week Mungu anasema na mimi mnoo kwa habari ya watu.


Pat & Magreth

 Melody & Joyce
Team
the joy in them..........
 we do both........ the story behind ( kwi! kwi! kwi!)



                                     Thank you,Waita zvako,Ndinokuda ladies.

Tuesday, July 1, 2014

DOBOLILOOOO.........

 Niliwambia mwanangu mie ana kipaji cha riadha........... ana medali ya Gold mjue ,yaani mshindi wa kwanza kwa wasichana!!!!! ndani ya wiki hiyo hiyo nimeletewa na hiyo certificate!!!! yaani tupogo kote kote!!!!! NIMRUDISHIE NINI HUYU MUNGU WANGU JAMANIIIIII!!!!! Kweli naringaje mwenzenu halafu unajua nini????? hiki kichwa cha Mama mtu yaani huwa hatuaminiki kama tunaweza........ kwa nini nasema hivyo niliosoma nao watanielewa hapa........  sio hao tu hata ndugu zangu wanafamilia wanalielewa hili........ Nilikuja kuaminiwa too late  aiseeeee,baada yakuwasuprise mara kibao Kwi! kwi! kwi! lakini pia ilinisaidia mnooo ..............  ndivyo ilivyo kwa Mwanangu hata Mama yake sometimes huwa namawazo nae Ha! ha! ha! ......................ni  full fujo fujo fulani.......mpaka huwa namuonea huruma na mwalimu wake darasani, Mwalimu wake huwa anasema she is born to be a leader ( tunaliweka mikononi mwa Bwana maana yeye ndie ajuaye) halafu  akiletaga hizo fujo zake , mtu anambie hako katabia kako weeee, ntakavyombadilikia sasa......  Muulizeni Baba wawili na Mama yenu alivyokuja huku ugomvi wake si mdogo kwi! kwi! kwi!

Tunaamini Mungu wetu ataendelea kututetea maana huu ni mwanzo ( TUTAKUWA VICHWA NA WALA SIO MKIA)

OUR WINNERS............ Washindi wa kwanza wa kike na wakiume hao katikati wenye medali ya gold Careen na Mwenzie hao wapembeni washindi wa pili
These two have been very good friends tangu  Careen ana 7months & Declan was 4months( tulivyofika tuu huku)

Careen with friends

SIFA NA UTUKUFU ZIMRUDIE MUNGU WETU MAANA BILA YEYE HAMNA KITU.......